< Torati 1 >

1 Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
These [are] the words which Moses spoke to all Israel on the east side of Jordan in the wilderness, in the plain over against Suf, between Paran, and Tophel, and Laban, and Hazeroth, and Dizahab.
2 (Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
([There are] eleven days [journey] from Horeb by the way of mount Seir to Kadesh-barnea.)
3 Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
And it came to pass in the fortieth year, in the eleventh month, on the first [day] of the month, [that] Moses spoke to the children of Israel, according to all that the LORD had given him in commandment to them;
4 Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
After he had slain Sihon the king of the Amorites, who dwelt in Heshbon, and Og the king of Bashan, who dwelt at Astaroth in Edrei:
5 Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
On the east side of Jordan, in the land of Moab, began Moses to declare this law, saying,
6 Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
The LORD our God spoke to us in Horeb, saying, Ye have dwelt long enough in this mount:
7 Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
Turn you, and take your journey, and go to the mount of the Amorites, and to all [the places] nigh to it, in the plain, on the hills, and in the vale, and in the south, and by the sea-side, to the land of the Canaanites, and to Lebanon, to the great river, the river Euphrates.
8 Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
Behold, I have set the land before you: go in and possess the land which the LORD swore to your fathers, Abraham, Isaac, and Jacob, to give to them and to their seed after them.
9 Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
And I spoke to you at that time, saying, I am not able to bear you myself alone:
10 Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
The LORD your God hath multiplied you, and behold, ye [are] this day as the stars of heaven for multitude.
11 Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
(The LORD God of your fathers make you a thousand times so many more as ye [are], and bless you, as he hath promised you!)
12 Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
How can I alone bear your encumbrance, and your burden, and your strife?
13 Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
Take ye wise men, and understanding, and known among your tribes, and I will make them rulers over you.
14 Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
And ye answered me, and said, The thing which thou hast spoken [is] good [for us] to do.
15 Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
So I took the chief of your tribes, wise men, and known, and made them heads over you, captains over thousands, and captains over hundreds, and captains over fifties, and captains over tens, and officers among your tribes.
16 Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
And I charged your judges at that time, saying, Hear [the causes] between your brethren, and judge righteously between [every] man and his brother, and the stranger [that is] with him.
17 Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
Ye shall not respect persons in judgment; [but] ye shall hear the small as well as the great; ye shall not be afraid of the face of man; for the judgment [is] God's: and the cause that is too hard for you, bring to me, and I will hear it.
18 Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
And I commanded you at that time all the things which ye should do.
19 Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
And when we departed from Horeb, we went through all that great and terrible wilderness, which ye saw by the way of the mountain of the Amorites, as the LORD our God commanded us; and we came to Kadesh-barnea.
20 Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
And I said to you, Ye have come to the mountain of the Amorites, which the LORD our God doth give to us.
21 Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
Behold, the LORD thy God hath set the land before thee: go up [and] possess [it], as the LORD God of thy fathers hath said to thee; fear not, neither be discouraged.
22 Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
And ye came near to me every one of you, and said, We will send men before us, and they shall explore the land for us, and bring us word again by what way we must go up, and into what cities we shall come.
23 Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
And the saying pleased me well: and I took twelve men of you, one of a tribe:
24 Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
And they turned and ascended the mountain, and came to the valley of Eshcol, and explored it.
25 Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
And they took of the fruit of the land in their hands, and brought [it] down to us, and brought us word again, and said, [It is] a good land which the LORD our God doth give us.
26 Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
Notwithstanding, ye would not go up, but rebelled against the commandment of the LORD your God:
27 Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
And ye murmured in your tents, and said, Because the LORD hated us, he hath brought us forth from the land of Egypt, to deliver us into the hand of the Amorites, to destroy us.
28 Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
Whither shall we go up? our brethren have discouraged our heart, saying, The people [are] greater and taller than we; the cities [are] great and walled up to heaven; and moreover, we have seen the sons of the Anakims there.
29 Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
Then I said to you, Dread not, neither be afraid of them.
30 Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
The LORD your God who goeth before you; he shall fight for you, according to all that he did for you in Egypt before your eyes;
31 na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
And in the wilderness, where thou hast seen how the LORD thy God bore thee, as a man doth bear his son, in all the way that ye went, until ye came into this place.
32 Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
Yet in this thing ye did not believe the LORD your God,
33 ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
Who went in the way before you, to search out for you a place to pitch your tents [in], in fire by night, to show you by what way ye should go, and in a cloud by day.
34 Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
And the LORD heard the voice of your words, and was wroth, and swore, saying,
35 “Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
Surely there shall not one of these men of this evil generation see that good land, which I swore to give to your fathers,
36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
Save Caleb the son of Jephunneh; he shall see it, and to him will I give the land that he hath trod upon, and to his children, because he hath wholly followed the LORD.
37 Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
Also the LORD was angry with me for your sakes, saying, Thou also shalt not go in thither.
38 Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
[But] Joshua the son of Nun, who standeth before thee, he shall go in thither. Encourage him: for he shall cause Israel to inherit it.
39 Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
Moreover, your little ones, which ye said should be a prey, and your children, which in that day had no knowledge between good and evil, they shall go in thither, and to them will I give it, and they shall possess it.
40 Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
But [as for] you, turn ye, and take your journey into the wilderness by the way of the Red sea.
41 Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
Then ye answered and said to me, We have sinned against the LORD, we will go up and fight, according to all that the LORD our God commanded us. And when ye had girded on every man his weapons of war, ye were ready to ascend the hill.
42 Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
And the LORD said to me, Say to them, Go not up, neither fight; for I [am] not among you; lest ye be smitten before your enemies.
43 Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
So I spoke to you; and ye would not hear, but rebelled against the commandment of the LORD, and presumptuously ascended the hill.
44 Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
And the Amorites, who dwelt on that mountain, came out against you, and chased you, as bees do, and destroyed you in Seir, [even] to Hormah.
45 Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
And ye returned and wept before the LORD; but the LORD would not hearken to your voice, nor give ear to you.
46 Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.
So ye abode in Kadesh many days, according to the days that ye abode [there].

< Torati 1 >