< Torati 1 >

1 Haya ni maneno Mose aliyoyasema kwa Israeli yote jangwani mashariki ya Yordani, ambayo iko Araba, inayokabiliana na Sufu, kati ya Parani na Tofeli, Labani, Haserothi na Dizahabu.
These are the words which Moses spoke unto all Israel on this side of the Jordan, in the wilderness, in the plain opposite Suph, between Paran, and Tophel, and Laban, and Chazeroth, and Di-zahab.
2 (Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya Mlima Seiri mpaka Kadesh-Barnea.)
It is a journey of eleven days from Horeb by the way of mount Seir unto Kadesh-barnea'.
3 Katika mwaka wa arobaini, siku ya kwanza ya mwezi wa kumi na moja, Mose aliwatangazia Waisraeli yale yote Bwana aliyomwamuru kuwahusu.
And it came to pass in the fortieth year, in the eleventh month, on the first day of the month, that Moses spoke unto the children of Israel, according to all that the Lord had commanded him concerning them;
4 Hii ilikuwa baada ya kumshinda Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala Heshboni, na pia huko Edrei alikuwa amemshinda Ogu mfalme wa Bashani, ambaye alitawala huko Ashtarothi.
After he had smitten Sichon the king of the Emorites, who dwelt in Cheshbon, and 'Og the king of Bashan, who dwelt at 'Ashtaroth in Edre'i.
5 Huko mashariki ya Yordani katika nchi ya Moabu, Mose alianza kuielezea sheria hii, akisema:
On this side of the Jordan, in the land of Moab, began Moses to explain this law, saying,
6 Bwana Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, “Mmekaa vya kutosha katika mlima huu.
The Lord our God spoke unto us in Horeb, saying, Ye have tarried long enough at this mount;
7 Vunjeni kambi, msonge mbele kuelekea nchi ya vilima ya Waamori; nendeni kwa watu wote ambao ni majirani wa Araba, katika milima, upande wa magharibi chini ya vilima, katika Negebu na kandokando ya pwani, mpaka nchi ya Wakanaani hadi Lebanoni, na kufika mto mkubwa Frati.
Turn you, and take your journey, and go to the mountain of the Emorites, and unto all its neighboring places, in the plain, in the mountain, and in the lowlands, and in the southern country, and by the coast of the sea, to the land of the Canaanites, and unto the Lebanon, up to the great river, the river Euphrates.
8 Tazama, nimewapa ninyi nchi hii. Ingieni mkaimiliki nchi ambayo Bwana aliapa kuwa angaliwapa baba zenu, Abrahamu, Isaki na Yakobo, pamoja na vizazi vyao baada yao.”
Behold, I have given up the land before you: go in and take possession of the land which the Lord hath sworn unto your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give it unto them and to their seed after them.
9 Wakati ule niliwaambia, “Ninyi mmekuwa mzigo mzito sana kwangu kuwachukua peke yangu.
And I said unto you at that time, as followeth, I am not able alone to bear you:
10 Bwana Mungu wenu ameongeza hesabu yenu, hivi kwamba leo ninyi ni wengi kama nyota za angani.
The Lord your God hath multiplied you, and, behold, ye are this day as the stars of heaven for multitude.
11 Naye Bwana, Mungu wa baba zenu na awaongeze mara elfu na kuwabariki kama alivyoahidi!
May the Lord the God of your fathers make you a thousand times as many more as ye are; and bless you, as he hath spoken unto you.
12 Lakini mimi nitawezaje kubeba matatizo yenu, na mizigo yenu, na magomvi yenu peke yangu?
How can I by myself alone bear your cumbrance, and your burden, and your strife!
13 Chagueni baadhi ya watu wenye hekima, wenye ufahamu na wanaoheshimika kutoka kila kabila lenu, nami nitawaweka juu yenu.”
Furnish for yourselves wise and understanding men, and those known among your tribes, and I will place them as chiefs over you.
14 Mlinijibu, “Shauri ulilolitoa ni zuri.”
And ye answered me, and said, The thing which thou hast spoken is good to do.
15 Kwa hiyo niliwachukua wanaume viongozi wa makabila yenu, wenye hekima na wanaoheshimika, nami nikawateua wawe na mamlaka juu yenu kama majemadari wa maelfu, wa mamia, wa hamsini, na wa makumi, na kama maafisa wa makabila.
And I took the chiefs of your tribes, wise and known men, and I set them as heads over you, captains over thousands, and captains over hundreds, and captains over fifties, and captains over tens, and as officers for your tribes.
16 Nami wakati ule nikawaagiza waamuzi wenu: Sikilizeni magomvi kati ya ndugu zenu na mwamue kwa haki, hata kama shauri ni kati ya ndugu wa Kiisraeli, au kati ya mmoja wa ndugu wa Kiisraeli na mgeni.
And I commanded your judges at that time, saying, Hear the causes between your brethren, and judge righteously, between a man and his brother, and between his stranger.
17 Msionyeshe upendeleo katika maamuzi; wasikilizeni wote sawasawa, wadogo kwa wakubwa. Msimwogope mtu yeyote, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Mniletee mimi shauri lolote lililo gumu sana kwenu, nami nitalisikiliza.
Ye shall not respect persons in judgment; the small as well as the great shall ye hear; ye shall not be afraid of any man; for the judgment belongeth to God: and the cause that is too hard for you shall ye bring unto me, and I will hear it.
18 Nami wakati ule niliwaambia kila kitu ambacho mngefanya.
And I commanded you at that time all the things which ye should do.
19 Kisha, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru, tuliondoka kutoka Horebu na kwenda kuelekea nchi ya vilima ya Waamori, kupitia jangwa lile kubwa lote la kutisha, lile mliloliona, nasi tukafika Kadesh-Barnea.
And we departed from Horeb, and we went through all that great and terrible wilderness, which ye have seen, by the way of the mountain of the Emorites, as the Lord our God had commanded us; and we came as far as Kadesh-barnea'.
20 Kisha niliwaambia, “Mmefika katika nchi ya vilima ya Waamori, ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.
And I said unto you, Ye are come unto the mountain of the Emorites, which the Lord our God doth give unto us.
21 Tazama, Bwana Mungu wenu amewapa nchi. Pandeni mkaimiliki kama Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaambia. Msiogope, wala msikate tamaa.”
Behold, the Lord thy God hath given up the land before thee: go up and take possession of it, as the Lord the God of thy fathers hath spoken unto thee; do not fear, and be not discouraged.
22 Ndipo ninyi nyote mkanijia na kusema, “Tupeleke watu watutangulie kuipeleleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea taarifa kuhusu njia tutakayopita, na miji tutakayoiendea.”
And ye all came near unto me and said, Let us send out men before us, that they may search out for us the land, and bring us word again concerning the way by which we must go up, and the cities to which we shall come.
23 Wazo hilo lilionekana zuri kwangu; kwa hiyo niliwachagua watu wenu kumi na wawili, mwanaume mmoja kutoka kila kabila.
And the thing was pleasing in my eyes; and I took of you twelve men, one man for every tribe:
24 Waliondoka na kukwea katika nchi ya vilima, wakafika katika Bonde la Eshkoli na kuipeleleza.
And they turned and went up into the mountain, and came unto the valley of Eshcol, and spied it out.
25 Wakachukua baadhi ya matunda ya nchi, wakatuletea na kutuarifu, “Ni nchi nzuri ambayo Bwana Mungu wetu anatupa.”
And they took in their hand some of the fruit of the land, and brought it down unto us; and they brought us word again, and said, The land which the Lord our God doth give us is good.
26 Lakini hamkuwa tayari kukwea, mkaasi dhidi ya amri ya Bwana Mungu wenu.
But you would not go up, and ye rebelled against the order of the Lord your God;
27 Mkanungʼunika ndani ya mahema yenu na kusema, “Bwana anatuchukia, kwa hiyo alitutoa Misri ili kututia mikononi mwa Waamori kutuangamiza.
And ye murmured in your tents, and said, On account of the hatred of the Lord toward us, hath he brought us forth out of the land of Egypt, to deliver us into the hand of the Emorites, to destroy us.
28 Twende wapi? Ndugu zetu wametufanya kufa moyo. Wanasema, ‘Watu wa huko wana nguvu zaidi na ni warefu kuliko sisi tulivyo; miji ni mikubwa, yenye kuta zilizofika juu angani. Zaidi ya hayo, tumewaona Waanaki huko.’”
Whither shall we go up? our brethren have made faint our heart, saying, The people is greater and taller than we; the cities are great and fortified up to heaven; and moreover the sons of the 'Anakim have we seen there.
29 Ndipo nikawaambia, “Msihofu, wala msiwaogope.
And I said unto you, Have no dread, nor be ye afraid of them.
30 Bwana Mungu wenu anayewatangulia, atawapigania, kama alivyofanya kwa ajili yenu huko Misri, mbele ya macho yenu hasa,
The Lord your God who goeth before you, he it is who will fight for you; all just as he did for you in Egypt before your eyes;
31 na pia huko jangwani. Huko mliona jinsi Bwana Mungu wenu alivyowachukua, kama baba amchukuavyo mwanawe, katika njia yote mliyoiendea mpaka mkafika mahali hapa.”
And in the wilderness which thou hast seen, where the Lord thy God bore thee, as a man doth bear his son, on all the way that ye have gone, until ye came unto this place.
32 Pamoja na hili, hamkumtegemea Bwana Mungu wenu,
Yet in this thing do ye not believe in the Lord your God,
33 ambaye aliwatangulia katika safari yenu, kwa moto usiku na kwa wingu mchana, kuwatafutia mahali penu pa kupiga kambi na kuwaonyesha njia mtakayoiendea.
Who goeth before you on the way to seek out for you a place for your encamping, in fire by night, to cause you to see on the way in which ye are to go, and in a cloud by day.
34 Wakati Bwana aliposikia lile mlilosema, alikasirika, akaapa, akasema:
And the Lord heard the voice of your words; and he was wroth, and swore, saying,
35 “Hakuna mtu wa kizazi hiki kiovu atakayeona nchi nzuri niliyoapa kuwapa baba zenu,
Surely there shall not one of these men of this evil generation see that good land, which I have sworn to give unto your fathers;
36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, nami nitampa yeye na wazao wake nchi aliyoikanyaga kwa miguu, kwa sababu alimfuata Bwana kwa moyo wote.”
Save Caleb the son of Yephunneh, he shall see it, and to him will I give the land upon which he hath trodden, and to his children; because he hath wholly followed the Lord.
37 Kwa sababu yenu Bwana pia alinikasirikia mimi, akasema, “Hutaingia hiyo nchi pia.
also with me was the Lord angry for your sakes, saying, also thou shalt not go in thither.
38 Lakini msaidizi wako, Yoshua mwana wa Nuni, ataingia. Mtie moyo, kwa sababu atawaongoza Waisraeli kuirithi hiyo nchi.
Joshua the son of Nun, who standeth before thee, he shall go in thither: him encourage; for he shall cause Israel to inherit it.
39 Wale watoto ambao mliwasema wangelichukuliwa mateka, yaani watoto wenu ambao bado hawajui jema na baya, wataingia katika nchi. Nitawapa hiyo nchi, nao wataimiliki.
And your little ones, of whom ye said, They will become a prey, and your children who know not this day either good or evil, these shall go in thither; and unto them will I give it, and they shall possess it.
40 Bali ninyi geukeni, mwondoke kuelekea jangwani kwa kufuata njia ya Bahari ya Shamu.”
But as for you, turn you, and take your journey into the wilderness by the way of the Red Sea.
41 Ndipo mkanijibu, “Tumemtenda Bwana dhambi. Tutakwenda kupigana, kama Bwana Mungu wetu alivyotuamuru.” Hivyo kila mmoja wenu akachukua silaha zake, huku mkifikiri kuwa ni rahisi kukwea katika nchi ya vilima.
And ye answered and said unto me, We have sinned against the Lord; we indeed will go up and we will fight, according to all that the Lord our God hath commanded us; and ye girded on every man his weapons of war, and ye insisted to go up into the mountain.
42 Lakini Bwana aliniambia, “Waambie, ‘Msipande kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja nanyi. Mtashindwa na adui zenu.’”
And the Lord said unto me, Say unto them, Go not up, and do not fight; for I am not among you; lest ye be smitten before your enemies.
43 Hivyo niliwaambia, lakini hamkutaka kusikia. Mliasi dhidi ya amri ya Bwana, na katika kiburi chenu mlienda katika nchi ya vilima.
And I spoke unto you; but ye would not hear; and ye rebelled against the order of the Lord, and you were presumptuous, and went up into the mountain.
44 Waamori ambao waliishi katika vilima hivyo waliinuka dhidi yenu, wakawafukuza kama kundi la nyuki wakiwapiga njia yote ya Seiri mpaka Horma.
And the Emorites, who dwelt in that mountain: came out against you, and they pursued you, as the bees do, and they overthrew you in Seir, as far as Chormah.
45 Mlirudi na kulia mbele za Bwana, lakini Mungu hakusikiliza kilio chenu, wala hakuwajali.
And ye returned and wept before the Lord; but the Lord hearkened not to your voice, nor gave ear unto you.
46 Hivyo mlikaa Kadeshi kwa siku nyingi, kwa muda ule wote mliokaa huko.
And ye tarried in Kadesh many days, according unto the days that ye tarried there.

< Torati 1 >