< Danieli 9 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario mwana wa Ahasuero (mzaliwa wa Umedi), ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli,
در نخستین سال داریوش مادی (پسر خشایارشا) که بر بابِلی‌ها حکومت می‌کرد،
2 katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mimi Danieli nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno la Bwana alilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini.
بله، در نخستین سال سلطنت او، من، دانیال، با خواندن کتب مقدّس متوجۀ کلام خداوند به ارمیای نبی شدم که فرموده بود ویرانی اورشلیم هفتاد سال طول خواهد کشید.
3 Kwa hiyo nikamgeukia Bwana Mungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, na kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.
پس دست دعا و التماس به سوی خداوند دراز کردم و روزه گرفتم، پلاس پوشیدم و خاکستر بر سرم ریختم
4 Nikamwomba Bwana Mungu wangu na kutubu: “Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake,
و در دعا اعتراف کرده، گفتم: «ای خداوند، تو خدای بزرگ و مهیب هستی. تو همیشه به وعده‌هایت وفا می‌کنی و به کسانی که تو را دوست دارند و اوامر تو را اطاعت می‌کنند، رحمت می‌نمایی.
5 tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi; tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako.
ولی ما گناه کرده و مرتکب شرارت شده‌ایم، ما سرکش و خطاکاریم و از دستورهای تو سرپیچی نموده‌ایم.
6 Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu, na watu wote wa nchi.
به سخنان انبیا که خدمتگزاران تو بودند و پیام تو را به پادشاهان و بزرگان و اجداد و افراد قوم ما رساندند، گوش نداده‌ایم.
7 “Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu: tukiwa wanaume wa Yuda, na watu wa Yerusalemu, na Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.
«ای خداوند، عدالت از آن توست و شرمندگی از آن ما، ما که از اهالی یهودا و اورشلیم و تمام اسرائیل هستیم و به سبب خیانتی که به تو کرده‌ایم، در سرزمینهای دور و نزدیک پراکنده شده‌ایم.
8 Ee Bwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
آری، ای خداوند، ما و پادشاهان و بزرگان و اجداد ما رسوا شده‌ایم زیرا به تو گناه کرده‌ایم.
9 Bwana Mungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake.
اما تو بخشنده و مهربان هستی و کسانی را که به تو گناه کرده‌اند می‌بخشی.
10 Hatukumtii Bwana Mungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii.
ای خداوند، ای خدای ما، ما از تو سرپیچی کرده‌ایم و قوانین تو را که به‌وسیلۀ انبیایت به ما داده‌ای، زیر پا گذاشته‌ایم.
11 Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii. “Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
تمام بنی‌اسرائیل از احکام تو سرپیچی کرده، از تو برگشته‌اند و به صدایت گوش نداده‌اند. همهٔ ما به تو گناه کرده‌ایم و به همین سبب لعنتهایی که در کتاب تورات خدمتگزارت موسی نوشته شده، بر سر ما آمده است.
12 Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu, kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka kwa Yerusalemu.
هر چه درباره ما و رهبرانمان گفته بودی به وقوع پیوسته است. آن بلای عظیمی که در اورشلیم بر سر ما آمد در هیچ جای دنیا دیده نشده است.
13 Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwa Bwana Mungu wetu kwa kugeuka kutoka dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake.
این بلا طبق آنچه در تورات موسی نوشته شده بر سر ما آمد، ولی با وجود این باز نخواستیم از گناهانمان دست بکشیم و آنچه را درست است به جا آوریم تا تو از ما راضی شوی.
14 Bwana hakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo; lakini hata hivyo hatujamtii.
بنابراین، تو که مراقب کارهای ما بودی ما را تنبیه کردی زیرا تو ای خداوند، خدای ما، همیشه عادلانه عمل می‌کنی؛ با وجود این ما به تو گوش فرا ندادیم.
15 “Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu, na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya.
«ای خداوند، خدای ما، تو با قدرتت قوم خود را از مصر بیرون آوردی، و نام تو در میان قومها معروف شد چنانکه امروز می‌بینیم. هر چند ما گناه کرده‌ایم و پر از شرارت هستیم،
16 Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.
ولی ای خداوند، التماس می‌کنم به خاطر امانتت، خشم و غضبت را از شهر مقدّست اورشلیم برگردانی، زیرا قوم تو و شهر تو به سبب گناهان ما و شرارت اجداد ما مورد تمسخر همسایگان واقع گردیده‌اند.
17 “Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako angalia kwa huruma ukiwa wa mahali pako patakatifu.
«ای خدای ما، دعای خدمتگزار خود را بشنو! به التماس من توجه فرما! به خاطر خداوندیت بر خانهٔ مقدّست که ویران شده نظر لطف بینداز!
18 Ee Mungu, tega sikio na ukasikie; fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi.
ای خدای من، گوش بده و دعای ما را بشنو. چشمانت را باز کن و خرابی شهری را که نام تو بر آن است، ببین. ما به سبب شایستگی خود از تو درخواست کمک نمی‌کنیم، بلکه به خاطر رحمت عظیم تو!
19 Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”
«ای خداوند، دعای ما را بشنو و گناهان ما را ببخش. ای خداوند، به درخواست ما گوش بده و عمل نما و به خاطر خودت، ای خدای من، تأخیر نکن، زیرا نام تو بر این قوم و بر این شهر می‌باشد.»
20 Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na nikifanya maombi yangu kwa Bwana Mungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu,
زمانی که مشغول دعا بودم و به گناهان خود و گناهان قوم خود اسرائیل اعتراف می‌کردم و از خداوند، خدایم برای شهر مقدّسش اورشلیم التماس می‌نمودم،
21 wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibu wakati wa kutoa dhabihu ya jioni.
جبرائیل که او را در خواب قبلی دیده بودم، با سرعت پرواز کرد و هنگام قربانی عصر نزد من رسید
22 Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu.
و به من گفت: «دانیال، من آمده‌ام به تو فهم ببخشم تا بتوانی این اسرار را بفهمی.
23 Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:
همان لحظه که مشغول دعا شدی، جواب دعای تو داده شد و من آمده‌ام تو را از آن آگاه سازم، زیرا خدا تو را بسیار دوست دارد. پس، حال، دقت کن تا آنچه را که دربارهٔ خوابت می‌گویم، بفهمی.
24 “Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu, ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii, na pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.
«به امر خدا برای قوم تو و شهر مقدّس تو هفتاد”هفته“طول خواهد کشید تا طبق پیشگویی انبیا فساد و شرارت از بین برود، کفاره گناهان داده شود، عدالت جاودانی برقرار گردد و قدس‌الاقداس دوباره تقدیس شود.
25 “Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuwako majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu.
بدان و آگاه باش که از زمان صدور فرمان بازسازی اورشلیم تا ظهور مسیح رهبر، هفت”هفته“و شصت و دو”هفته“طول خواهد کشید و با وجود اوضاع بحرانی، اورشلیم با کوچه‌ها و حصارهایش بازسازی خواهد شد.
26 Baada ya majuma sitini na mawili, Mpakwa Mafuta atakatiliwa mbali, wala hatabaki na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa.
«پس از آن دورهٔ شصت و دو”هفته“، مسیح کشته خواهد شد، اما نه برای خودش. سپس پادشاهی همراه سپاهیانش به اورشلیم و معبد حمله برده، آنها را خراب خواهد کرد. آخر زمان مانند طوفان فرا خواهد رسید و جنگ و خرابیها را که مقرر شده، با خود خواهد آورد.
27 Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”
این پادشاه با اشخاص زیادی پیمان یک”هفته‌ای“می‌بندد، ولی وقتی نصف این مدت گذشته باشد، مانع تقدیم قربانیها و هدایا خواهد شد. سپس این خرابکار، خانهٔ خدا را آلوده خواهد ساخت، ولی سرانجام آنچه برای او مقرر شده بر سرش خواهد آمد.»

< Danieli 9 >