< Danieli 9 >
1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario mwana wa Ahasuero (mzaliwa wa Umedi), ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli,
“In the first year of Darius, son of Ahasuerus, of the seed of the Medes, who has been made king over the kingdom of the Chaldeans,
2 katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mimi Danieli nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno la Bwana alilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini.
in the first year of his reign, I, Daniel, have understood by scrolls the number of the years (in that a word of YHWH has been to Jeremiah the prophet), concerning the fulfilling of the desolations of Jerusalem—seventy years;
3 Kwa hiyo nikamgeukia Bwana Mungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, na kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.
and I set my face toward the Lord God, to seek [by] prayer and supplications, with fasting, and sackcloth, and ashes.
4 Nikamwomba Bwana Mungu wangu na kutubu: “Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake,
And I pray to my God YHWH, and confess, and say: Ah, now, O Lord God, the great and the fearful, keeping the covenant and the kindness to those loving Him and to those keeping His commands;
5 tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi; tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako.
we have sinned, and done perversely, and done wickedly, and rebelled, to turn aside from Your commands, and from Your judgments:
6 Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu, na watu wote wa nchi.
and we have not listened to Your servants, the prophets, who have spoken in Your Name to our kings, our heads, and our fathers, and to all the people of the land.
7 “Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu: tukiwa wanaume wa Yuda, na watu wa Yerusalemu, na Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.
To You, O Lord, [is] the righteousness, and to us the shame of face, as [at] this day, to the men of Judah, and to the inhabitants of Jerusalem, and to all Israel, who are near, and who are far off, in all the lands to where You have driven them, in their trespass that they have trespassed against You.
8 Ee Bwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
O Lord, to us [is] the shame of face, to our kings, to our heads, and to our fathers, in that we have sinned against You.
9 Bwana Mungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake.
To the Lord our God [are] the mercies and the forgivenesses, for we have rebelled against Him,
10 Hatukumtii Bwana Mungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii.
and have not listened to the voice of our God YHWH, to walk in His laws, that He has set before us by the hand of His servants the prophets;
11 Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii. “Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
and all Israel has transgressed Your law, to turn aside so as not to listen to Your voice; and poured on us is the execration, and the oath, that is written in the Law of Moses, servant of God, because we have sinned against Him.
12 Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu, kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka kwa Yerusalemu.
And He confirms His words that He has spoken against us, and against our judges who have judged us, to bring great calamity on us, in that it has not been done under the whole heavens as it has been done in Jerusalem,
13 Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwa Bwana Mungu wetu kwa kugeuka kutoka dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake.
as it is written in the Law of Moses, all this evil has come on us, and we have not appeased the face of our God YHWH to turn back from our iniquities, and to act wisely in Your truth.
14 Bwana hakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo; lakini hata hivyo hatujamtii.
And YHWH watches for the evil, and brings it on us, for our God YHWH is righteous concerning all His works that He has done, and we have not listened to His voice.
15 “Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu, na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya.
And now, O Lord our God, who has brought forth Your people from the land of Egypt by a strong hand, and makes for Yourself a name as at this day, we have sinned, we have done wickedly.
16 Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.
O Lord, according to all Your righteous acts, please let Your anger and Your fury turn back from Your city Jerusalem, Your holy mountain, for by our sins, and by the iniquities of our fathers, Jerusalem and Your people [are] for a reproach to all our neighbors;
17 “Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako angalia kwa huruma ukiwa wa mahali pako patakatifu.
and now, listen, O our God, to the prayer of Your servant, and to his supplication, and cause Your face to shine on Your sanctuary that [is] desolate, for the Lord’s sake.
18 Ee Mungu, tega sikio na ukasikie; fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi.
Incline, O my God, Your ear, and hear, open Your eyes and see our desolations, and the city on which Your Name is called; for not for our righteous acts are we causing our supplications to fall before You, but for Your mercies that [are] many.
19 Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”
O Lord, hear, O Lord, forgive; O Lord, attend and do; do not delay, for Your own sake, O my God, for Your Name is called on Your city, and on Your people.
20 Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na nikifanya maombi yangu kwa Bwana Mungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu,
And while I am speaking, and praying, and confessing my sin, and the sin of my people Israel, and causing my supplication to fall before my God YHWH, for the holy mountain of my God,
21 wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibu wakati wa kutoa dhabihu ya jioni.
indeed, while I am speaking in prayer, then that one Gabriel, whom I had seen in vision at the commencement, being caused to fly swiftly, is coming to me at the time of the evening present.
22 Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu.
And he gives understanding, and speaks with me, and says, O Daniel, now I have come forth to cause you to consider understanding wisely;
23 Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:
at the commencement of your supplications the word has come forth, and I have come to declare [it], for you [are] greatly desired, and understand concerning the matter, and consider concerning the appearance.
24 “Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu, ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii, na pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.
Seventy periods of seven are determined for your people and for your holy city, to shut up the transgression, and to seal up sins, and to cover iniquity, and to bring in continuous righteousness, and to seal up vision and prophet, and to anoint the Holy of Holies.
25 “Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuwako majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu.
And you know, and consider wisely, from the going forth of the word to restore and to build Jerusalem until Messiah the Leader [is] seven periods of seven, and sixty-two periods of seven: the broad place has been built again, and the rampart, even in the distress of the times.
26 Baada ya majuma sitini na mawili, Mpakwa Mafuta atakatiliwa mbali, wala hatabaki na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa.
And after the sixty-two periods of seven, Messiah is cut off, but not for Himself, and the people of the leader who is coming destroy the city and the holy place; and its end [is] with a flood, and until the end [is] war, [and] desolations [are] determined.
27 Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”
And he has strengthened a covenant with many [for] one period of seven, and [in] the midst of the period of seven he causes sacrifice and present to cease, and by the wing of abominations he is making desolate, even until the consummation, and that which is determined is poured on the desolate one.”