< Danieli 9 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario mwana wa Ahasuero (mzaliwa wa Umedi), ambaye alifanywa mtawala juu ya ufalme wa Babeli,
In the first year of Darius the son of Assuerus, of the seed of the Medes, who reigned over the kingdom of the Chaldeans,
2 katika mwaka wa kwanza wa utawala wake, mimi Danieli nilielewa kutokana na Maandiko, kulingana na neno la Bwana alilopewa nabii Yeremia, kwamba ukiwa wa Yerusalemu ungetimizwa kwa miaka sabini.
I Daniel understood by books the number of the years which was the word of the Lord to the prophet Jeremias, [even] seventy years for the accomplishment of the desolation of Jerusalem.
3 Kwa hiyo nikamgeukia Bwana Mungu na kumsihi katika maombi na dua, katika kufunga, na kuvaa nguo ya gunia na kujipaka majivu.
And I set my face toward the Lord God, to seek [him] diligently by prayer and supplications, with fastings and sackcloth.
4 Nikamwomba Bwana Mungu wangu na kutubu: “Ee Bwana, Mungu mkuu na unayetisha, anayeshika agano lake la upendo kwao wanaompenda na kutii maagizo yake,
And I prayed to the Lord my God, and confessed, and said, O Lord, the great and wonderful God, keeping thy covenant and thy mercy to them that love thee, and to them that keep thy commandments; we have sinned,
5 tumetenda dhambi na kufanya mabaya. Tumekuwa waovu na tumeasi; tumegeuka mbali na maagizo yako na sheria zako.
we have done iniquity, we have transgressed, and we have departed and turned aside from thy commandments and from thy judgments:
6 Hatukuwasikiliza watumishi wako manabii, ambao kwa jina lako walisema na wafalme wetu, wakuu wetu, baba zetu, na watu wote wa nchi.
and we have not hearkened to thy servants the prophets, who spoke in thy name to our kings, and our princes, and our fathers, and to all the people of the land.
7 “Bwana, wewe ni mwenye haki, lakini siku hii ya leo tumefunikwa na aibu: tukiwa wanaume wa Yuda, na watu wa Yerusalemu, na Israeli yote, wote walio karibu na walio mbali, katika nchi zote ulikotutawanya kwa sababu ya kukosa uaminifu kwako.
To thee, O Lord, [belongs] righteousness, and to us confusion of face, as at this day; to the men of Juda, and to the dwellers in Jerusalem, and to all Israel, to them that are near, and to them that are far off in all the earth, wherever thou hast scattered them, for the sin which they committed.
8 Ee Bwana, sisi na wafalme wetu, wakuu wetu na baba zetu tumefunikwa na aibu kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
In thee, O Lord, is our righteousness, and to us [belongs] confusion of face, and to our kings, and to our princes, and to our fathers, forasmuch as we have sinned.
9 Bwana Mungu wetu ni mwenye rehema na anayesamehe, hata ingawa tumefanya uasi dhidi yake.
To thee, the Lord our God, [belong] compassions and forgivenesses, whereas we have departed [from thee];
10 Hatukumtii Bwana Mungu wetu wala kuzishika sheria alizotupa kupitia kwa watumishi wake manabii.
neither have we hearkened to the voice of the Lord our God, to walk in his laws, which he set before us by the hands of his servants the prophets.
11 Israeli yote imekosea sheria yako na kugeuka mbali, nao wamekataa kukutii. “Kwa hiyo laana na viapo vya hukumu vilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, mtumishi wa Mungu, vimemiminwa juu yetu, kwa sababu tumefanya dhambi dhidi yako.
Moreover all Israel have transgressed thy law, and have refused to hearken to thy voice; so the curse has come upon us, and the oath that is written in the law of Moses the servant of God, because we have sinned against him.
12 Umetimiza maneno uliyosema dhidi yetu na dhidi ya watawala wetu, kwa kuleta maafa makubwa juu yetu. Chini ya mbingu yote kamwe hapajatendeka kitu kama kile kilichotendeka kwa Yerusalemu.
And he has confirmed his words, which he spoke against us, and against our judges who judged us, [by] bringing upon us great evils, such as have not happened under the whole heaven, according to what has happened in Jerusalem.
13 Kama vile ilivyoandikwa katika sheria ya Mose, misiba hii yote imekuja juu yetu, lakini hatujaomba fadhili kwa Bwana Mungu wetu kwa kugeuka kutoka dhambi zetu na kuwa wasikivu katika kweli yake.
As it is written in the law of Moses, all these evils have come upon us: yet we have not besought the Lord our God, that we might turn away from our iniquities, and have understanding in all thy truth.
14 Bwana hakusita kuleta maafa juu yetu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mwenye haki katika kila afanyalo; lakini hata hivyo hatujamtii.
The Lord also has watched, and brought the evils upon us: for the Lord our God is righteous in all his work which he has executed, but we have not hearkened to his voice.
15 “Sasa, Ee Bwana Mungu wetu, ambaye uliwatoa watu wako Misri kwa mkono wenye nguvu, na ambaye umejifanyia Jina linalodumu mpaka leo, tumetenda dhambi, tumefanya mabaya.
And now, O Lord our God, who broughtest thy people out of the land of Egypt with a mighty hand, and madest to thyself a name, as [at] this day; we have sinned, we have transgressed.
16 Ee Bwana, wewe kwa kadiri ya matendo yako ya haki, ondoa hasira yako na ghadhabu yako juu ya Yerusalemu, mji wako, mlima wako mtakatifu. Dhambi zetu na maovu ya baba zetu yameifanya Yerusalemu na watu wako kitu cha kudharauliwa kwa wale wote wanaotuzunguka.
O Lord, thy mercy is over all: let, I pray thee, thy wrath turn away, and thine anger from thy city Jerusalem, [even] thy holy mountain: for we have sinned, and because of our iniquities, and those of our fathers, Jerusalem and thy people are become a reproach among all that are round about us.
17 “Basi Mungu wetu, sasa sikia maombi na dua ya mtumishi wako. Ee Bwana, kwa ajili yako angalia kwa huruma ukiwa wa mahali pako patakatifu.
And now, O Lord our God, hearken to the prayer of thy servant, and his supplications, and cause thy face to shine on thy desolate sanctuary, for thine [own] sake, O Lord.
18 Ee Mungu, tega sikio na ukasikie; fumbua macho yako ukaone ukiwa wa mji ule wenye Jina lako. Hatukutolei maombi yetu kwa sababu sisi tuna haki, bali kwa sababu ya rehema zako nyingi.
Incline thine ear, O my God, and hear; open thine eyes and behold our desolation, and that of thy city on which thy name is called: for we do not bring our pitiful case before thee on [the ground of] our righteousness, but on [the ground of] thy manifold compassions, O Lord.
19 Ee Bwana, sikiliza! Ee Bwana, samehe! Ee Bwana, sikia na ukatende! Kwa ajili yako, Ee Mungu wangu, usikawie, kwa sababu mji wako na watu wako wanaitwa kwa Jina lako.”
Hearken, O Lord; be propitious, O Lord; attend, O Lord; delay not, O my God, for thine own sake: for thy name is called upon thy city and upon thy people.
20 Basi, nilipokuwa bado nikinena na kuomba, nikiungama dhambi yangu na dhambi ya watu wangu Israeli, na nikifanya maombi yangu kwa Bwana Mungu wangu kwa ajili ya mlima wake mtakatifu,
And while I was yet speaking, and praying, and confessing my sins and the sins of my people Israel, and bringing my pitiful case before the Lord my God concerning the holy mountain;
21 wakati nilipokuwa bado katika maombi, Gabrieli, yule mtu niliyekuwa nimemwona katika maono hapo awali, alinijia kwa kasi karibu wakati wa kutoa dhabihu ya jioni.
yea, while I was yet speaking in prayer, behold the man Gabriel, whom I had seen in the vision at the beginning, [came] flying, and he touched me about the hour of the evening sacrifice.
22 Akanielimisha na kuniambia, “Danieli, sasa nimekuja kukupa akili na ufahamu.
And he instructed me, and spoke with me, and said, O Daniel, I am now come forth to impart to thee understanding.
23 Mara ulipoanza kuomba, jibu lilitolewa, ambalo nimekuja kukupasha habari, kwa maana wewe unapendwa sana. Kwa hiyo, tafakari ujumbe huu na uelewe maono haya:
At the beginning of thy supplication the word came forth, and I am come to tell thee; for thou art a man much beloved: therefore consider the matter, understand the vision.
24 “Majuma sabini yameamriwa kwa ajili ya watu wako na kwa ajili ya mji wako mtakatifu, ili kumaliza makosa, kukomesha dhambi, kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri maono na unabii, na pia kumtia mafuta yeye aliye mtakatifu sana.
Seventy weeks have been determined upon thy people, and upon the holy city, for sin to be ended, and to seal up transgressions, and to blot out the iniquities, and to make atonement for iniquities, and to bring in everlasting righteousness, and to seal the vision and the prophet, and to anoint the Most Holy.
25 “Ujue na kuelewa hili: Tangu kutolewa kwa amri ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu mpaka kuja kwa Mpakwa mafuta, aliye mtawala, kutakuwako majuma saba na majuma sitini na mawili. Barabara zitajengwa tena pamoja na mahandaki, lakini katika wakati wa taabu.
And thou shalt know and understand, that from the going forth of the command for the answer and for the building of Jerusalem until Christ the prince [there shall be] seven weeks, and sixty-two weeks: and then [the time] shall return, and the street shall be built, and the wall, and the times shall be exhausted.
26 Baada ya majuma sitini na mawili, Mpakwa Mafuta atakatiliwa mbali, wala hatabaki na kitu. Watu wa mtawala atakayekuja watauharibu mji pamoja na mahali patakatifu. Mwisho utakuja kama mafuriko: Vita vitaendelea mpaka mwisho, nao ukiwa umeamriwa.
And after the sixty-two weeks, the anointed one shall be destroyed, and there is no judgment in him: and he shall destroy the city and the sanctuary with the prince that is coming: they shall be cut off with a flood, and to the end of the war which is rapidly completed he shall appoint [the city] to desolations.
27 Mtawala huyo atathibitisha agano na watu wengi kwa juma moja. Katikati ya juma hilo atakomesha dhabihu na sadaka. Mahali pa dhabihu katika Hekalu atasimamisha chukizo la uharibifu, hadi mwisho ulioamriwa utakapomiminwa juu yake yeye aletaye uharibifu.”
And one week shall establish the covenant with many: and in the midst of the week my sacrifice and drink-offering shall be taken away: and on the temple [shall be] the abomination of desolations; and at the end of the time an end shall be put to the desolation.

< Danieli 9 >