< Danieli 8 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni.
In year three of [the] reign of Belshazzar the king a vision it appeared to me I Daniel after the [one] which it appeared to me at the beginning.
2 Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.
And I saw in the vision and it was when saw I and I [was] in Susa the citadel which [is] in Elam the province and I saw in the vision and I I was at [the] canal of Ulai.
3 Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye.
And I lifted up eyes my and I saw and there! - a ram one [was] standing before the canal and [belonged] to it two horns and the two horns [were] high and the one [was] high more than the second and the high [one] [was] growing up at the last.
4 Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.
I saw the ram thrusting west-ward and north-ward and south-ward and any living creatures not they stood before it and there not [was one] delivering from hand its and it did according to pleasure its and it magnified itself.
5 Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi.
And I - I was observing and there! [the] he-goat of the goats [was] coming from the west over [the] surface of all the earth and not [it was] touching the earth and the he-goat a horn of conspicuousness [was] between eyes its.
6 Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi.
And it came to the ram [the] possessor of the two horns which I had seen standing before the canal and it ran against it in [the] rage of strength its.
7 Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu.
And I saw it approaching - beside the ram and it was enraged against it and it struck the ram and it broke [the] two horns its and not it was strength in the ram to stand before it and it threw it [the] ground towards and it trampled it and not anyone was delivering the ram from hand its.
8 Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.
And [the] he-goat of the goats it magnified itself up to muchness and just as became mighty it it was broken the horn great and they grew up conspicuousness four in place its to [the] four [the] winds of the heavens.
9 Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza.
And from the one of them it came out a horn one from a small [thing] and it became great excess to the south and to the east and to the beauty.
10 Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga.
And it became great to [the] host of the heavens and it made fall [the] ground towards some of the host and some of the stars and it trampled them.
11 Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini.
And to [the] commander of the host it magnified itself and from him (it was removed *Q(K)*) the perpetual [offering] and it was thrown down [the] place of sanctuary his.
12 Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.
And an army it will be set over the perpetual [offering] in transgression and it will throw down truth [the] ground towards and it will act and it will succeed.
13 Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”
And I heard! one holy [one] speaking and he said one holy [one] to the certain [one] who was speaking until when? [will be] the vision the perpetual [offering] and the transgression desolate to give over and [the] sanctuary and an army trampling.
14 Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”
And he said to me until evening morning two thousand and three hundreds and it will be put right [the] sanctuary.
15 Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu.
And it was when saw I I Daniel the vision and I sought! understanding and there! [was] standing to before me like [the] appearance of a man.
16 Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”
And I heard [the] voice of a person between Ulai and he called and he said O Gabriel explain to this [one] the vision.
17 Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”
And he came beside standing place my and when came he I was terrified and I fell! on face my and he said to me understand O son of humankind that [is] for [the] time of [the] end the vision.
18 Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.
And when spoke he with me I was dazed on face my [the] ground towards and he touched me and he made stand me on standing place my.
19 Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa.
And he said here I [am] making known to you [that] which it will be at [the] end of the indignation for [it is] for [the] appointed time of [the] end.
20 Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi.
The ram which you saw [the] possessor of the two horns [is] [the] kings of Media and Persia.
21 Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
And the he-goat hairy [is] [the] king of Greece and the horn great which [is] between eyes its it [is] the king first.
22 Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.
And the broken [horn] and they arose four [horns] in place its four kingdoms from a nation they will arise and not with power its.
23 “Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila.
And at [the] end of reign their when are completed the rebels he will arise a king strong of face and understanding of intrigue.
24 Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu.
And it will be mighty power his and not by own power his and wonders he will destroy and he will succeed and he will act and he will destroy mighty [ones] and a people of holy [ones].
25 Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.
And on insight his and he will make successful deceit by hand his and in heart his he will magnify himself and in prosperity he will destroy many [people] and on a prince of princes he will stand and by not a hand he will be broken.
26 “Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”
And [the] vision of the evening and the morning which it has been told [is] truth it and you keep secret the vision for [it is] for days many.
27 Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.
And I Daniel I was done [in] and I was sick days and I arose and I did [the] work of the king and I was appalled on the vision and there not [was one] giving understanding.