< Danieli 7 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Belshaza mfalme wa Babeli, Danieli aliota ndoto, nayo maono yakapita mawazoni yake alipokuwa amelala kitandani mwake. Akayaandika mambo aliyoyaona katika ndoto yake.
In the first year of Belshazzar, king of Babylon, Daniel saw a dream, and visions of his head upon his bed. Then he wrote the dream, and related the sum of the matters.
2 Danieli akasema: “Katika maono yangu usiku nilitazama, na hapo mbele yangu kulikuwepo na upepo kutoka pande nne za mbingu, ukivuruga bahari kuu.
Daniel spake and said: —I saw in my vision by night, and behold, the four winds of heaven burst forth upon the great sea.
3 Wanyama wanne wakubwa, kila mmoja tofauti na mwenzake, wakajitokeza kutoka bahari.
And four great beasts came up out of the sea, diverse one from another.
4 “Mnyama wa kwanza alifanana na simba, naye alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikatazama mpaka mabawa yake yalipongʼolewa, naye akainuliwa katika nchi, akasimama kwa miguu miwili kama mwanadamu, naye akapewa moyo wa binadamu.
The first was like a lion, and had the wings of an eagle; I beheld till its wings were plucked from it, and it was lifted up from the earth, and made to stand upon its feet like a man, and a man's heart was given to it.
5 “Hapo mbele yangu kulikuwa na mnyama wa pili, ambaye alionekana kama dubu. Upande wake mmoja ulikuwa umeinuka, na alikuwa na mbavu tatu katika kinywa chake kati ya meno yake. Akaambiwa, ‘Amka, ule nyama mpaka ushibe!’
And behold, another beast, the second, like to a bear; and it stood up on one side, and it had three ribs in its mouth between its teeth; and they spake thus to it: Arise, devour much flesh!
6 “Baada ya huyo, nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama mwingine, aliyefanana na chui. Juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege. Mnyama huyu alikuwa na vichwa vinne, naye akapewa mamlaka ya kutawala.
After this I beheld, and lo, another, like a leopard, which had upon its back four wings of a bird; the beast also had four heads, and dominion was given to it.
7 “Baada ya huyo, katika maono yangu usiku nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama wa nne, mwenye kutisha na kuogofya, tena mwenye nguvu nyingi. Alikuwa na meno makubwa ya chuma; akapondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chini ya nyayo zake chochote kilichosalia. Alikuwa tofauti na wanyama wote waliotangulia, naye alikuwa na pembe kumi.
After this I saw in the night visions, and behold, a fourth beast, dreadful, and terrible, and exceedingly strong; and it had great iron teeth; it devoured, and broke in pieces, and stamped the residue with its feet, and it differed from all the beasts that were before it; and it had ten horns.
8 “Wakati nilipokuwa ninafikiri kuhusu pembe hizo, mbele yangu kulikuwa na pembe nyingine, ambayo ni ndogo, iliyojitokeza miongoni mwa zile kumi; pembe tatu za mwanzoni zilingʼolewa ili kuipa nafasi hiyo ndogo. Pembe hii ilikuwa na macho kama ya mwanadamu, na mdomo ulionena kwa majivuno.
I gave heed to the horns, and behold, there came up among them another little horn, before which three of the first horns were plucked up by the roots; and behold, in this horn were eyes like the eyes of a man, and a mouth speaking great things.
9 “Nilipoendelea kutazama, “viti vya enzi vikawekwa, naye Mzee wa Siku akaketi. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji; nywele za kichwa chake zilikuwa nyeupe kama sufu. Kiti chake cha enzi kilikuwa kinawaka kwa miali ya moto, nayo magurudumu yake yote yalikuwa yanawaka moto.
I beheld, till thrones were placed, and an aged one seated himself, his garment white like snow, and the hair of his head like pure wool; his throne like a fiery flame, and its wheels like burning fire.
10 Mto wa moto ulikuwa unatiririka, ukipita mbele yake. Maelfu elfu wakamhudumia; kumi elfu mara kumi elfu wakasimama mbele zake. Mahakama ikakaa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.
A fiery stream issued and came forth from before him; thousands of thousands ministered to him, and ten thousand times ten thousand stood before him; the tribunal sat, and the books were opened.
11 “Kisha nikaendelea kutazama kwa sababu ya yale maneno ya majivuno yaliyosemwa na ile pembe. Nikaendelea kuangalia mpaka yule mnyama alipouawa, na mwili wake ukaharibiwa na kutupwa katika ule moto uliowaka.
I beheld; and because of the great words which the horn spake, I beheld till the beast was slain, and his body destroyed and given to the burning flame.
12 (Wanyama wengine walikuwa wamevuliwa mamlaka yao, lakini waliruhusiwa kuishi kwa muda fulani.)
As to the rest of the beasts, they had their dominion taken away, for the duration of their lives had been appointed for a season and a time.
13 “Katika maono yangu ya usiku nilitazama, na mbele yangu nikamwona anayefanana na mwanadamu, akija pamoja na mawingu ya mbinguni. Akamkaribia huyo Mzee wa Siku, na akaongozwa mbele zake.
I saw in the night visions, and behold, with the clouds of heaven came one like a son of man, and came to the aged one, and they brought him near before him.
14 Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme wenye nguvu; nao watu wa kabila zote, mataifa, na watu wa kila lugha wakamwabudu. Utawala wake ni utawala wa milele ambao hautapita, nao ufalme wake ni ule ambao kamwe hautaangamizwa.
And there was given him dominion, and glory, and a kingdom, that all people, nations, and languages should serve him; his dominion is an everlasting dominion, which shall not pass away, and his kingdom shall not be destroyed.
15 “Mimi, Danieli, nilipata mahangaiko rohoni, nayo maono yale yaliyopita ndani ya mawazo yangu yalinisumbua.
I Daniel was grieved in my spirit within me, and the visions of my head troubled me.
16 Nikamkaribia mmoja wa wale waliosimama pale na kumuuliza maana halisi ya haya yote. “Basi akaniambia na kunipa tafsiri ya vitu hivi:
I came near to one of them that stood by, and asked him the truth concerning all this. So he told me, and made known to me the interpretation of the things.
17 ‘Hao wanyama wanne wakubwa ni falme nne zitakazoinuka duniani.
These great beasts, which are four, are four kings, which shall arise out of the earth.
18 Lakini watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana watapokea ufalme na kuumiliki milele: naam, milele na milele.’
Then shall the saints of the Most High receive the kingdom, and possess the kingdom forever, even for ever and ever.
19 “Kisha nilitaka kufahamu maana ya kweli ya mnyama yule wa nne, ambaye alikuwa tofauti na wale wengine wote, tena wa kutisha sana, na meno yake ya chuma na makucha ya shaba: mnyama ambaye alipondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chochote kilichosalia.
Then I desired to know the truth concerning the fourth beast, which differed from all the others, exceedingly dreadful, whose teeth were of iron and his nails of brass, which devoured, brake in pieces, and stamped the residue with his feet;
20 Pia mimi nilitaka kujua kuhusu zile pembe kumi juu ya kichwa chake, na pia kuhusu ile pembe nyingine iliyojitokeza, ambayo mbele yake zile tatu za mwanzoni zilianguka, ile pembe ambayo ilionekana kuvutia macho zaidi kuliko zile nyingine, na ambayo ilikuwa na macho na kinywa kilichonena kwa majivuno.
and concerning the ten horns which were in his head, and the other which came up, and before which three fell, —even that horn which had eyes, and a mouth that spake very great things, and whose appearance was larger than that of his fellows.
21 Nilipoendelea kutazama, pembe hii ilikuwa inapigana vita dhidi ya watakatifu na kuwashinda,
I beheld, and the same horn made war with the saints and prevailed against them,
22 mpaka huyo Mzee wa Siku alipokuja na kutamka hukumu kwa kuwapa ushindi watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana, na wakati ukawadia walipoumiliki ufalme.
until the aged one came, and judgment was rendered to the saints of the Most High, and the time came that the saints should possess the kingdom.
23 “Alinipa maelezo haya: ‘Mnyama wa nne ni ufalme wa nne ambao utatokea duniani. Utakuwa tofauti na falme nyingine zote, nao utaharibu dunia nzima, ukiikanyaga chini na kuipondaponda.
He spake thus: The fourth beast is a fourth kingdom upon the earth, which shall differ from all kingdoms, and shall devour the whole earth, and shall tread it down, and break it in pieces.
24 Zile pembe kumi ni wafalme kumi watakaotokana na ufalme huu. Baada yao mfalme mwingine atainuka, ambaye atakuwa tofauti na wale waliotangulia, naye atawaangusha wafalme watatu.
And the ten horns are ten kings, which shall arise out of this kingdom; and another shall arise after them; and he shall differ from the former, and shall subdue three kings.
25 Atanena maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu Sana na kuwaonea watakatifu wake, huku akijaribu kubadili majira na sheria. Watakatifu watatiwa chini ya mamlaka yake kwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati.
And he will speak great words against the Most High, and will harass the saints of the Most High, and will resolve to change times and laws; and they shall be given into his hand a time, and times, and half a time.
26 “‘Lakini mahakama itakaa kuhukumu, nayo mamlaka yake yataondolewa na kuangamizwa kabisa milele.
But the tribunal shall sit, and his dominion shall be taken away, and consumed and destroyed forever.
27 Ndipo ufalme, mamlaka na ukuu wa falme chini ya mbingu yote utakabidhiwa kwa watakatifu, watu wa Yeye Aliye Juu Sana. Ufalme wake utakuwa ufalme wa milele, nao watawala wote watamwabudu na kumtii yeye.’
And the sovereignty and dominion and power over all kingdoms under the whole heaven shall be given to the people of the saints of the Most High; his kingdom is an everlasting kingdom, and all dominions shall serve and obey him.
28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Mimi Danieli nilitaabika sana katika mawazo yangu, nao uso wangu ukabadilika, lakini nililiweka jambo hilo moyoni mwangu.”
Here ended his words. As for me Daniel, my thoughts terrified me much, and my countenance changed; but I kept the matter in my heart.

< Danieli 7 >