< Danieli 7 >
1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Belshaza mfalme wa Babeli, Danieli aliota ndoto, nayo maono yakapita mawazoni yake alipokuwa amelala kitandani mwake. Akayaandika mambo aliyoyaona katika ndoto yake.
In the first year of Belshazzar, king of Babylon, Daniel saw a dream and a vision in his head on his bed. And, writing down the dream, he understood it in a concise manner, and so, summarizing it tersely, he said:
2 Danieli akasema: “Katika maono yangu usiku nilitazama, na hapo mbele yangu kulikuwepo na upepo kutoka pande nne za mbingu, ukivuruga bahari kuu.
I saw in my vision at night, and behold, the four winds of the heavens fought upon the great sea.
3 Wanyama wanne wakubwa, kila mmoja tofauti na mwenzake, wakajitokeza kutoka bahari.
And four great beasts, different from one another, ascended from the sea.
4 “Mnyama wa kwanza alifanana na simba, naye alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikatazama mpaka mabawa yake yalipongʼolewa, naye akainuliwa katika nchi, akasimama kwa miguu miwili kama mwanadamu, naye akapewa moyo wa binadamu.
The first was like a lioness and had the wings of an eagle. I watched as its wings were plucked off, and it was raised from the earth and stood on its feet like a man, and the heart of a man was given to it.
5 “Hapo mbele yangu kulikuwa na mnyama wa pili, ambaye alionekana kama dubu. Upande wake mmoja ulikuwa umeinuka, na alikuwa na mbavu tatu katika kinywa chake kati ya meno yake. Akaambiwa, ‘Amka, ule nyama mpaka ushibe!’
And behold, another beast, like a bear, stood to one side, and there were three rows in its mouth and in its teeth, and they spoke to it in this way: “Arise, devour much flesh.”
6 “Baada ya huyo, nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama mwingine, aliyefanana na chui. Juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege. Mnyama huyu alikuwa na vichwa vinne, naye akapewa mamlaka ya kutawala.
After this, I watched, and behold, another like a leopard, and it had wings like a bird, four upon it, and four heads were on the beast, and power was given to it.
7 “Baada ya huyo, katika maono yangu usiku nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama wa nne, mwenye kutisha na kuogofya, tena mwenye nguvu nyingi. Alikuwa na meno makubwa ya chuma; akapondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chini ya nyayo zake chochote kilichosalia. Alikuwa tofauti na wanyama wote waliotangulia, naye alikuwa na pembe kumi.
After this, I watched in the vision of the night, and behold, a fourth beast, terrible yet wondrous, and exceedingly strong; it had great iron teeth, eating yet crushing, and trampling down the remainder with his feet, but it was unlike the other beasts, which I had seen before it, and it had ten horns.
8 “Wakati nilipokuwa ninafikiri kuhusu pembe hizo, mbele yangu kulikuwa na pembe nyingine, ambayo ni ndogo, iliyojitokeza miongoni mwa zile kumi; pembe tatu za mwanzoni zilingʼolewa ili kuipa nafasi hiyo ndogo. Pembe hii ilikuwa na macho kama ya mwanadamu, na mdomo ulionena kwa majivuno.
I considered the horns, and behold, another little horn rose out of the midst of them. And three of the first horns were rooted out by its presence. And behold, eyes like the eyes of a man were in this horn, and a mouth speaking unnatural things.
9 “Nilipoendelea kutazama, “viti vya enzi vikawekwa, naye Mzee wa Siku akaketi. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji; nywele za kichwa chake zilikuwa nyeupe kama sufu. Kiti chake cha enzi kilikuwa kinawaka kwa miali ya moto, nayo magurudumu yake yote yalikuwa yanawaka moto.
I watched until thrones were set up, and the Ancient of days sat down. His garment was radiant like snow, and the hair of his head like clean wool; his throne was flames of fire, its wheels had been set on fire.
10 Mto wa moto ulikuwa unatiririka, ukipita mbele yake. Maelfu elfu wakamhudumia; kumi elfu mara kumi elfu wakasimama mbele zake. Mahakama ikakaa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.
A river of fire rushed forth from his presence. Thousands upon thousands ministered to him, and ten thousand times hundreds of thousands attended before him. The trial began, and the books were opened.
11 “Kisha nikaendelea kutazama kwa sababu ya yale maneno ya majivuno yaliyosemwa na ile pembe. Nikaendelea kuangalia mpaka yule mnyama alipouawa, na mwili wake ukaharibiwa na kutupwa katika ule moto uliowaka.
I watched because of the voice of the great words which that horn was speaking, and I saw that the beast had been destroyed, and its body was ruined and had been handed over to be burnt with fire.
12 (Wanyama wengine walikuwa wamevuliwa mamlaka yao, lakini waliruhusiwa kuishi kwa muda fulani.)
Likewise, the power of the other beasts was taken away, and a limited time of life was appointed to them, until one time and another.
13 “Katika maono yangu ya usiku nilitazama, na mbele yangu nikamwona anayefanana na mwanadamu, akija pamoja na mawingu ya mbinguni. Akamkaribia huyo Mzee wa Siku, na akaongozwa mbele zake.
I watched, therefore, in the vision of the night, and behold, with the clouds of heaven, one like a son of man arrived, and he approached all the way to the Ancient of days, and they presented him before him.
14 Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme wenye nguvu; nao watu wa kabila zote, mataifa, na watu wa kila lugha wakamwabudu. Utawala wake ni utawala wa milele ambao hautapita, nao ufalme wake ni ule ambao kamwe hautaangamizwa.
And he gave him power, and honor, and the kingdom, and all peoples, tribes, and languages will serve him. His power is an eternal power, which will not be taken away, and his kingdom, one which will not be corrupted.
15 “Mimi, Danieli, nilipata mahangaiko rohoni, nayo maono yale yaliyopita ndani ya mawazo yangu yalinisumbua.
My spirit was terrified. I, Daniel, was fearful at these things, and the visions of my head disturbed me.
16 Nikamkaribia mmoja wa wale waliosimama pale na kumuuliza maana halisi ya haya yote. “Basi akaniambia na kunipa tafsiri ya vitu hivi:
I approached one of the attendants and asked the truth from him about all these things. He told me the interpretation of the words, and he instructed me:
17 ‘Hao wanyama wanne wakubwa ni falme nne zitakazoinuka duniani.
“These four great beasts are four kingdoms, which will rise from the earth.
18 Lakini watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana watapokea ufalme na kuumiliki milele: naam, milele na milele.’
Yet it is the saints of the Most High God who will receive the kingdom, and they will hold the kingdom from this generation, and forever and ever.”
19 “Kisha nilitaka kufahamu maana ya kweli ya mnyama yule wa nne, ambaye alikuwa tofauti na wale wengine wote, tena wa kutisha sana, na meno yake ya chuma na makucha ya shaba: mnyama ambaye alipondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chochote kilichosalia.
After this, I wanted to learn diligently about the fourth beast, which was very different from all, and exceedingly terrible; his teeth and claws were of iron; he devoured and crushed, and the remainder he trampled with his feet;
20 Pia mimi nilitaka kujua kuhusu zile pembe kumi juu ya kichwa chake, na pia kuhusu ile pembe nyingine iliyojitokeza, ambayo mbele yake zile tatu za mwanzoni zilianguka, ile pembe ambayo ilionekana kuvutia macho zaidi kuliko zile nyingine, na ambayo ilikuwa na macho na kinywa kilichonena kwa majivuno.
and about the ten horns, which he had on his head, and about the other, which had sprung up, before which three horns fell, and about that horn which had eyes and a mouth speaking great things, and which was more powerful than the rest.
21 Nilipoendelea kutazama, pembe hii ilikuwa inapigana vita dhidi ya watakatifu na kuwashinda,
I watched, and behold, that horn made war against the holy ones and prevailed over them,
22 mpaka huyo Mzee wa Siku alipokuja na kutamka hukumu kwa kuwapa ushindi watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana, na wakati ukawadia walipoumiliki ufalme.
until the Ancient of days came and gave judgment to the holy ones of the Supreme One, and the time arrived, and the holy ones obtained the kingdom.
23 “Alinipa maelezo haya: ‘Mnyama wa nne ni ufalme wa nne ambao utatokea duniani. Utakuwa tofauti na falme nyingine zote, nao utaharibu dunia nzima, ukiikanyaga chini na kuipondaponda.
And thus he said, “The fourth beast will be the fourth kingdom on earth, which will be greater than all the kingdoms, and will devour the whole earth, and will trample and crush it.
24 Zile pembe kumi ni wafalme kumi watakaotokana na ufalme huu. Baada yao mfalme mwingine atainuka, ambaye atakuwa tofauti na wale waliotangulia, naye atawaangusha wafalme watatu.
Moreover, the ten horns of the same kingdom will be ten kings, and another will rise up after them, and he will be mightier than the ones before him, and he will bring down three kings.
25 Atanena maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu Sana na kuwaonea watakatifu wake, huku akijaribu kubadili majira na sheria. Watakatifu watatiwa chini ya mamlaka yake kwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati.
And he will speak words against the Supreme One, and will exhaust the holy ones of the Most High, and he will think about what it would take to change the times and the laws, and they will be given into his hand until a time, and times, and half a time.
26 “‘Lakini mahakama itakaa kuhukumu, nayo mamlaka yake yataondolewa na kuangamizwa kabisa milele.
And a trial will begin, so that his power may be taken away, and be crushed, and be undone all the way to the end.
27 Ndipo ufalme, mamlaka na ukuu wa falme chini ya mbingu yote utakabidhiwa kwa watakatifu, watu wa Yeye Aliye Juu Sana. Ufalme wake utakuwa ufalme wa milele, nao watawala wote watamwabudu na kumtii yeye.’
Yet the kingdom, and the power, and the greatness of that kingdom, which is under all of heaven, shall be given to the people of the holy ones of the Most High, whose kingdom is an everlasting kingdom, and all kings will serve and obey him.”
28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Mimi Danieli nilitaabika sana katika mawazo yangu, nao uso wangu ukabadilika, lakini nililiweka jambo hilo moyoni mwangu.”
And here is the end of the message. I, Daniel, was greatly disturbed by my thoughts, and my mood was changed in me, but I preserved the message in my heart.