< Danieli 7 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Belshaza mfalme wa Babeli, Danieli aliota ndoto, nayo maono yakapita mawazoni yake alipokuwa amelala kitandani mwake. Akayaandika mambo aliyoyaona katika ndoto yake.
Léta prvního Balsazara krále Babylonského Daniel měl sen a vidění svá na ložci svém, i napsal ten sen krátkými slovy.
2 Danieli akasema: “Katika maono yangu usiku nilitazama, na hapo mbele yangu kulikuwepo na upepo kutoka pande nne za mbingu, ukivuruga bahari kuu.
Mluvil Daniel a řekl? Viděl jsem u vidění svém v noci, a aj, čtyři větrové nebeští bojovali na moři velikém.
3 Wanyama wanne wakubwa, kila mmoja tofauti na mwenzake, wakajitokeza kutoka bahari.
A čtyři šelmy veliké vystupovaly z moře, jedna od druhé rozdílná.
4 “Mnyama wa kwanza alifanana na simba, naye alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikatazama mpaka mabawa yake yalipongʼolewa, naye akainuliwa katika nchi, akasimama kwa miguu miwili kama mwanadamu, naye akapewa moyo wa binadamu.
První podobná lvu, a křídla orličí měla. Hleděl jsem, až vytrhána byla křídla její, jimiž se vznášela od země, tak že na nohách jako člověk státi musila, a srdce lidské dáno jest jí.
5 “Hapo mbele yangu kulikuwa na mnyama wa pili, ambaye alionekana kama dubu. Upande wake mmoja ulikuwa umeinuka, na alikuwa na mbavu tatu katika kinywa chake kati ya meno yake. Akaambiwa, ‘Amka, ule nyama mpaka ushibe!’
A aj, jiná šelma druhá podobná nedvědu, kteráž panství jedno vyzdvihla, a tři žebra v ústech jejích, mezi zuby jejími, a tak mluveno bylo k ní: Vstaň, nažer se hojně masa.
6 “Baada ya huyo, nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama mwingine, aliyefanana na chui. Juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege. Mnyama huyu alikuwa na vichwa vinne, naye akapewa mamlaka ya kutawala.
Potom jsem viděl, a aj, jiná podobná pardovi, kteráž měla čtyři křídla ptačí na hřbetě svém, a čtyřhlavá byla šelma ta, jíž moc dána byla.
7 “Baada ya huyo, katika maono yangu usiku nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama wa nne, mwenye kutisha na kuogofya, tena mwenye nguvu nyingi. Alikuwa na meno makubwa ya chuma; akapondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chini ya nyayo zake chochote kilichosalia. Alikuwa tofauti na wanyama wote waliotangulia, naye alikuwa na pembe kumi.
Potom viděl jsem u viděních nočních, a aj, šelma čtvrtá strašlivá a hrozná a velmi silná, mající zuby železné veliké, kteráž zžírala a potírala, ostatek pak nohama svýma pošlapávala; a ta byla rozdílná ode všech šelm, kteréž byly před ní, a měla rohů deset.
8 “Wakati nilipokuwa ninafikiri kuhusu pembe hizo, mbele yangu kulikuwa na pembe nyingine, ambayo ni ndogo, iliyojitokeza miongoni mwa zile kumi; pembe tatu za mwanzoni zilingʼolewa ili kuipa nafasi hiyo ndogo. Pembe hii ilikuwa na macho kama ya mwanadamu, na mdomo ulionena kwa majivuno.
Pilně jsem šetřil těch rohů, a hle, roh poslední malý vyrostal mezi nimi, a tři z těch rohů prvních vyvráceni jsou před ním; a aj, oči podobné očím lidským v rohu tom, a ústa mluvící pyšně.
9 “Nilipoendelea kutazama, “viti vya enzi vikawekwa, naye Mzee wa Siku akaketi. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji; nywele za kichwa chake zilikuwa nyeupe kama sufu. Kiti chake cha enzi kilikuwa kinawaka kwa miali ya moto, nayo magurudumu yake yote yalikuwa yanawaka moto.
Hleděl jsem, až trůnové ti svrženi byli, a Starý dnů posadil se, jehož roucho jako sníh bílé, a vlasové hlavy jeho jako vlna čistá, trůn jako jiskry ohně, kola jeho jako oheň hořící.
10 Mto wa moto ulikuwa unatiririka, ukipita mbele yake. Maelfu elfu wakamhudumia; kumi elfu mara kumi elfu wakasimama mbele zake. Mahakama ikakaa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.
Potok ohnivý tekl a vycházel od něho, tisícové tisíců sloužili jemu, a desetkrát tisíckrát sto tisíců stálo před ním; soud zasedl, a knihy otevříny byly.
11 “Kisha nikaendelea kutazama kwa sababu ya yale maneno ya majivuno yaliyosemwa na ile pembe. Nikaendelea kuangalia mpaka yule mnyama alipouawa, na mwili wake ukaharibiwa na kutupwa katika ule moto uliowaka.
Patřil jsem tehdáž, hned jakž se začal zvuk té řeči pyšné, kterouž roh mluvil; patřil jsem, dokudž ta šelma nebyla zabita, a vyhlazeno tělo její, a dáno k spálení ohni.
12 (Wanyama wengine walikuwa wamevuliwa mamlaka yao, lakini waliruhusiwa kuishi kwa muda fulani.)
A i ostatkům šelm odjali panství; nebo dlouhost života jim odměřena byla až do času, a to uloženého času.
13 “Katika maono yangu ya usiku nilitazama, na mbele yangu nikamwona anayefanana na mwanadamu, akija pamoja na mawingu ya mbinguni. Akamkaribia huyo Mzee wa Siku, na akaongozwa mbele zake.
Viděl jsem u vidění nočním, a aj, s oblaky nebeskými podobný Synu člověka přicházel; potom až k Starému dnů přišel, a před něj postaven byl.
14 Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme wenye nguvu; nao watu wa kabila zote, mataifa, na watu wa kila lugha wakamwabudu. Utawala wake ni utawala wa milele ambao hautapita, nao ufalme wake ni ule ambao kamwe hautaangamizwa.
I dáno jest jemu panství a sláva i království, aby všickni lidé, národové a jazykové sloužili jemu; jehož panství jest panství věčné, kteréž nepomíjí, a království jeho, kteréž se neruší.
15 “Mimi, Danieli, nilipata mahangaiko rohoni, nayo maono yale yaliyopita ndani ya mawazo yangu yalinisumbua.
I zhrozil se duch můj ve mně Danielovi u prostřed těla, a vidění má předěsila mne.
16 Nikamkaribia mmoja wa wale waliosimama pale na kumuuliza maana halisi ya haya yote. “Basi akaniambia na kunipa tafsiri ya vitu hivi:
Tedy přistoupil jsem k jednomu z přístojících, a ptal jsem se ho na jistotu vší té věci. I pověděl mi, a výklad řečí mi oznámil:
17 ‘Hao wanyama wanne wakubwa ni falme nne zitakazoinuka duniani.
Ty šelmy veliké, kteréž jsou čtyry, jsou čtyři králové, kteříž povstanou z země,
18 Lakini watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana watapokea ufalme na kuumiliki milele: naam, milele na milele.’
A ujmou království svatých výsostí, kteříž obdržeti mají království až na věky, a až na věky věků.
19 “Kisha nilitaka kufahamu maana ya kweli ya mnyama yule wa nne, ambaye alikuwa tofauti na wale wengine wote, tena wa kutisha sana, na meno yake ya chuma na makucha ya shaba: mnyama ambaye alipondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chochote kilichosalia.
Tedy žádostiv jsem byl zprávy o šelmě čtvrté, kteráž rozdílná byla ode všech jiných, hrozná velmi; zubové její železní, a pazoury její ocelivé, kteráž zžírala, potírala, ostatek pak nohama svýma pošlapávala.
20 Pia mimi nilitaka kujua kuhusu zile pembe kumi juu ya kichwa chake, na pia kuhusu ile pembe nyingine iliyojitokeza, ambayo mbele yake zile tatu za mwanzoni zilianguka, ile pembe ambayo ilionekana kuvutia macho zaidi kuliko zile nyingine, na ambayo ilikuwa na macho na kinywa kilichonena kwa majivuno.
Tolikéž o rozích desíti, kteříž byli na hlavě její, a o posledním, kterýž vyrostl, a před ním spadli tři; o tom rohu, pravím, kterýž měl oči a ústa mluvící pyšně, a byl na pohledění větší než jiní.
21 Nilipoendelea kutazama, pembe hii ilikuwa inapigana vita dhidi ya watakatifu na kuwashinda,
Viděl jsem, an roh ten válku vedl s svatými, a přemáhal je,
22 mpaka huyo Mzee wa Siku alipokuja na kutamka hukumu kwa kuwapa ushindi watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana, na wakati ukawadia walipoumiliki ufalme.
Až přišel Starý dnů, a oddán jest soud svatým výsostí, a čas přišel, aby to království svatí obdrželi.
23 “Alinipa maelezo haya: ‘Mnyama wa nne ni ufalme wa nne ambao utatokea duniani. Utakuwa tofauti na falme nyingine zote, nao utaharibu dunia nzima, ukiikanyaga chini na kuipondaponda.
Řekl takto: Šelma čtvrtá znamená království čtvrté na zemi, kteréž rozdílné bude ode všech království, a zžíře všecku zemi, a zmlátí ji a potře ji.
24 Zile pembe kumi ni wafalme kumi watakaotokana na ufalme huu. Baada yao mfalme mwingine atainuka, ambaye atakuwa tofauti na wale waliotangulia, naye atawaangusha wafalme watatu.
Rohů pak deset znamená, že z království toho deset králů povstane, a poslední povstane po nich, kterýž bude rozdílný od prvních, a poníží tří králů.
25 Atanena maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu Sana na kuwaonea watakatifu wake, huku akijaribu kubadili majira na sheria. Watakatifu watatiwa chini ya mamlaka yake kwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati.
A slova proti Nejvyššímu mluviti bude, a svaté výsostí potře; nadto pomýšleti bude, aby proměnil časy i práva, když vydáni budou v ruku jeho, až do času a časů, i do částky časů.
26 “‘Lakini mahakama itakaa kuhukumu, nayo mamlaka yake yataondolewa na kuangamizwa kabisa milele.
V tom bude soud osazen, a panství jeho odejmou, vypléní a vyhladí je docela.
27 Ndipo ufalme, mamlaka na ukuu wa falme chini ya mbingu yote utakabidhiwa kwa watakatifu, watu wa Yeye Aliye Juu Sana. Ufalme wake utakuwa ufalme wa milele, nao watawala wote watamwabudu na kumtii yeye.’
Království pak i panství, a důstojnost královská pode vším nebem dána bude lidu svatých výsostí; jehož království bude království věčné, a všickni páni jemu sloužiti a jeho poslouchati budou.
28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Mimi Danieli nilitaabika sana katika mawazo yangu, nao uso wangu ukabadilika, lakini nililiweka jambo hilo moyoni mwangu.”
Až potud konec té řeči. Mne pak Daniele myšlení má velice zkormoutila, a krása má proměnila se při mně, slovo však toto v srdci svém zachoval jsem.

< Danieli 7 >