< Danieli 7 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Belshaza mfalme wa Babeli, Danieli aliota ndoto, nayo maono yakapita mawazoni yake alipokuwa amelala kitandani mwake. Akayaandika mambo aliyoyaona katika ndoto yake.
В първата година на вавилонския цар Валтасар Даниил видя сън и видения на главата си върху леглото си. Тогава написа сънят и разказа същността на работите.
2 Danieli akasema: “Katika maono yangu usiku nilitazama, na hapo mbele yangu kulikuwepo na upepo kutoka pande nne za mbingu, ukivuruga bahari kuu.
Даниил проговаряйки, рече: Видях в нощното си видение, и ето, четирите небесни ветрища избухнаха върху голямото море.
3 Wanyama wanne wakubwa, kila mmoja tofauti na mwenzake, wakajitokeza kutoka bahari.
И четири големи зверове възлязоха из морето, различни един от друг.
4 “Mnyama wa kwanza alifanana na simba, naye alikuwa na mabawa kama ya tai. Nikatazama mpaka mabawa yake yalipongʼolewa, naye akainuliwa katika nchi, akasimama kwa miguu miwili kama mwanadamu, naye akapewa moyo wa binadamu.
Първият бе като лъв и имаше орлови крила; а, като го гледах, крилата му се изскубаха, и той се издигна от земята и биде заставен да се изправи на две нозе като човек, и даде му се човешко сърце.
5 “Hapo mbele yangu kulikuwa na mnyama wa pili, ambaye alionekana kama dubu. Upande wake mmoja ulikuwa umeinuka, na alikuwa na mbavu tatu katika kinywa chake kati ya meno yake. Akaambiwa, ‘Amka, ule nyama mpaka ushibe!’
След това, ето друг звяр, втори, приличен на мечка, който се повдигна от едната страна, и имаше три ребра в устата си между зъбите си; и му думаха така: Стани, изяж много месо.
6 “Baada ya huyo, nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama mwingine, aliyefanana na chui. Juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege. Mnyama huyu alikuwa na vichwa vinne, naye akapewa mamlaka ya kutawala.
Подир това, като погледнах, ето друг звяр, приличен на леопард, който имаше на гърба си четири птичи крила: тоя звяр имаше и четири глави; и даде му се власт.
7 “Baada ya huyo, katika maono yangu usiku nilitazama, na mbele yangu kulikuwa na mnyama wa nne, mwenye kutisha na kuogofya, tena mwenye nguvu nyingi. Alikuwa na meno makubwa ya chuma; akapondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chini ya nyayo zake chochote kilichosalia. Alikuwa tofauti na wanyama wote waliotangulia, naye alikuwa na pembe kumi.
Подир това, като погледнах в нощните видения, ето четвъртият звяр, страшен и ужасен и твърде як; той имаше големи железни зъби, с които пояждаше и сломяваше, като стъпкваше останалото с нозете си; той се различаваше от всичките зверове, които бяха преди него; и имаше десет рога.
8 “Wakati nilipokuwa ninafikiri kuhusu pembe hizo, mbele yangu kulikuwa na pembe nyingine, ambayo ni ndogo, iliyojitokeza miongoni mwa zile kumi; pembe tatu za mwanzoni zilingʼolewa ili kuipa nafasi hiyo ndogo. Pembe hii ilikuwa na macho kama ya mwanadamu, na mdomo ulionena kwa majivuno.
Като разглеждах роговете, ето, между тях излезе друг рог, малък, пред който три от първите рогове се изкорениха; и ето, в тоя рог имаше очи като човешки очи, и уста, които говореха надменно.
9 “Nilipoendelea kutazama, “viti vya enzi vikawekwa, naye Mzee wa Siku akaketi. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji; nywele za kichwa chake zilikuwa nyeupe kama sufu. Kiti chake cha enzi kilikuwa kinawaka kwa miali ya moto, nayo magurudumu yake yote yalikuwa yanawaka moto.
Гледах, додето се положиха престоли, и Древният по Дни седна, чието облекло беше бяло като сняг, и космите на главата му като чиста вълна, престолът му огнени пламъци, и колелата му пламенен огън.
10 Mto wa moto ulikuwa unatiririka, ukipita mbele yake. Maelfu elfu wakamhudumia; kumi elfu mara kumi elfu wakasimama mbele zake. Mahakama ikakaa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.
Огнена река излизаше и течеше изпред него; милион служители му слугуваха, и милиарди по милиарди стояха пред него; съдилището се откри, и книгите се отвориха.
11 “Kisha nikaendelea kutazama kwa sababu ya yale maneno ya majivuno yaliyosemwa na ile pembe. Nikaendelea kuangalia mpaka yule mnyama alipouawa, na mwili wake ukaharibiwa na kutupwa katika ule moto uliowaka.
Тогава погледнах по причина на гласа на надменните думи, които рогът изговаряше; гледах додето звярът биде убит, и тялото му погубено и предадено да се изгори с огън.
12 (Wanyama wengine walikuwa wamevuliwa mamlaka yao, lakini waliruhusiwa kuishi kwa muda fulani.)
А колкото за другите зверове, тяхното владичество биде отнето; животът им обаче се продължи до време и година.
13 “Katika maono yangu ya usiku nilitazama, na mbele yangu nikamwona anayefanana na mwanadamu, akija pamoja na mawingu ya mbinguni. Akamkaribia huyo Mzee wa Siku, na akaongozwa mbele zake.
Гледах в нощните видения, и ето, един като човешки син идеше с небесните облаци и стигна до Древния по Дни; и доведоха го пред Него.
14 Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme wenye nguvu; nao watu wa kabila zote, mataifa, na watu wa kila lugha wakamwabudu. Utawala wake ni utawala wa milele ambao hautapita, nao ufalme wake ni ule ambao kamwe hautaangamizwa.
И Нему се даде владичество, слава и царство, за да му слугуват всичките племена, народи и езици. Неговото владичество е вечно владичество, което няма да премине, и царството Му е царство, което няма да се разруши.
15 “Mimi, Danieli, nilipata mahangaiko rohoni, nayo maono yale yaliyopita ndani ya mawazo yangu yalinisumbua.
Колкото за мене Даниила, духът ми се наскърби дълбоко в тялото ми, и виденията на главата ми ме смутиха.
16 Nikamkaribia mmoja wa wale waliosimama pale na kumuuliza maana halisi ya haya yote. “Basi akaniambia na kunipa tafsiri ya vitu hivi:
Приближих се до едного от предстоящите и го попитах що е истинското значение на всичко това. И той ми разправи и ми даде да разбера значението на тия неща.
17 ‘Hao wanyama wanne wakubwa ni falme nne zitakazoinuka duniani.
Тия четири големи зверове, каза той, са четирима царе, които ще се издигнат от земята.
18 Lakini watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana watapokea ufalme na kuumiliki milele: naam, milele na milele.’
Но светиите на Всевишния ще приемат царството, и ще владеят царството до века и до вечни векове.
19 “Kisha nilitaka kufahamu maana ya kweli ya mnyama yule wa nne, ambaye alikuwa tofauti na wale wengine wote, tena wa kutisha sana, na meno yake ya chuma na makucha ya shaba: mnyama ambaye alipondaponda na kuangamiza wahanga wake, na kukanyaga chochote kilichosalia.
Тогава поисках да узная истината за четвъртия звяр, който се различаваше от всичките други и бе твърде страшен, чиито зъби бяха железни и ноктите му медни, който пояждаше и строшаваше, а останалото стъпкваше с нозете си,
20 Pia mimi nilitaka kujua kuhusu zile pembe kumi juu ya kichwa chake, na pia kuhusu ile pembe nyingine iliyojitokeza, ambayo mbele yake zile tatu za mwanzoni zilianguka, ile pembe ambayo ilionekana kuvutia macho zaidi kuliko zile nyingine, na ambayo ilikuwa na macho na kinywa kilichonena kwa majivuno.
и за десетте рога, които бяха на главата му, и за другия рог, който излезе, и пред който паднаха три, тоест, за оня рог, който имаше очи и уста, които говореха надменно, и който наглед бе по-як от другарите си.
21 Nilipoendelea kutazama, pembe hii ilikuwa inapigana vita dhidi ya watakatifu na kuwashinda,
Гледах същия рог като воюваше със светиите и превъзмогваше против тях,
22 mpaka huyo Mzee wa Siku alipokuja na kutamka hukumu kwa kuwapa ushindi watakatifu wa Yeye Aliye Juu Sana, na wakati ukawadia walipoumiliki ufalme.
докато дойде Древният по Дни, и се извърши съд за светиите на Всевишния, и настана времето, когато светиите завладяха царството.
23 “Alinipa maelezo haya: ‘Mnyama wa nne ni ufalme wa nne ambao utatokea duniani. Utakuwa tofauti na falme nyingine zote, nao utaharibu dunia nzima, ukiikanyaga chini na kuipondaponda.
Той каза така: Четвъртият звяр ще бъде четвърто царство на света, което ще се различава от всичките царства, и ще погълне целия свят, и ще го стъпче и разтроши.
24 Zile pembe kumi ni wafalme kumi watakaotokana na ufalme huu. Baada yao mfalme mwingine atainuka, ambaye atakuwa tofauti na wale waliotangulia, naye atawaangusha wafalme watatu.
А за десетте рога, те са десет царе, които ще се издигнат от това царство; и след тях ще се издигне друг, който ще се различава от първите, и ще покори трима царе.
25 Atanena maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu Sana na kuwaonea watakatifu wake, huku akijaribu kubadili majira na sheria. Watakatifu watatiwa chini ya mamlaka yake kwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati.
Той ще говори думи против Всевишния, ще изтощава светиите на Всевишния, и ще замисли да промени времена и закони; и те ще бъдат предаде в ръката му до време и времена и половина време.
26 “‘Lakini mahakama itakaa kuhukumu, nayo mamlaka yake yataondolewa na kuangamizwa kabisa milele.
Но когато съдилището ще заседава, ще му отнемат владичеството, за да го изтребят и погубят до край.
27 Ndipo ufalme, mamlaka na ukuu wa falme chini ya mbingu yote utakabidhiwa kwa watakatifu, watu wa Yeye Aliye Juu Sana. Ufalme wake utakuwa ufalme wa milele, nao watawala wote watamwabudu na kumtii yeye.’
А царството и владичеството и величието на царствата, които са под цялото небе, ще се дадат на людете, които са светиите на Всевишния, Чието царство е вечно царство, и на Когото всичките владичества ще служат и се покоряват.
28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Mimi Danieli nilitaabika sana katika mawazo yangu, nao uso wangu ukabadilika, lakini nililiweka jambo hilo moyoni mwangu.”
Тук е краят на това нещо. Колкото за мене, Даниила, размишленията ми ме смущават много, и изгледът на лицето ми се измени; но запазих това нещо в сърцето си.

< Danieli 7 >