< Danieli 6 >

1 Ilimpendeza Dario kuteua wakuu 120 kutawala katika ufalme wake wote,
Et il plut à Darius d'instituer cent vingt satrapes pour être en tout son royaume;
2 pamoja na wasimamizi watatu juu yao, ambao mmoja wao alikuwa Danieli. Wakuu walitoa hesabu kwa hao wasimamizi ili mfalme asipate hasara.
Et au-dessus d'eux, trois gouverneurs, dont l'un fut Daniel, pour que les satrapes leur rendissent compte, et que lui-même n'en fût pas surchargé.
3 Basi Danieli alijidhihirisha, miongoni mwa wasimamizi na wakuu kwa sifa zake za kipekee hata mfalme akapanga kumweka juu ya ufalme wote.
Et Daniel fut au-dessus d'eux, parce qu'il y avait en lui un esprit supérieur, et le roi le mit à la tête de tout son royaume.
4 Walipofahamu hilo, wakuu na wasimamizi wakajaribu kutafuta sababu za kumshtaki Danieli kuhusu usimamizi wake wa shughuli za serikali, lakini hawakuweza kufanikiwa. Hawakuweza kupata kosa kwake, kwa sababu alikuwa mwaminifu, wala hakupatikana na upotovu au uzembe.
Or les autres gouverneurs et les satrapes s'efforcèrent de trouver un sujet d'accusation contre Daniel, et ils ne purent trouver contre lui ni grief, ni délit, ni soupçon, parce qu'il était fidèle.
5 Mwishoni watu hawa walisema, “Kamwe hatutapata msingi wa mashtaka dhidi ya huyu Danieli isipokuwa iwe inahusiana na sheria ya Mungu wake.”
Et les gouverneurs se dirent: Nous ne trouverons pas de sujet d'accusation contre Daniel, sinon à cause des lois de son Dieu.
6 Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!
Alors les gouverneurs et les satrapes comparurent devant le roi, et lui dirent: Ô roi Darius, vis à jamais!
7 Wasimamizi wa ufalme, wasaidizi, wakuu, washauri na watawala wote wamekubaliana kwamba mfalme atoe sheria na kukazia amri kuwa yeyote atakayetoa dua kwa mungu au mwanadamu yeyote katika muda huu wa siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, ee mfalme, atupwe ndani ya tundu la simba.
Tous les officiers de ton royaume, généraux et satrapes, magistrats et intendants, ont tenu conseil pour qu'il fût rendu un édit royal, et formellement ordonné que tout homme qui durant trente jours fera une demande soit à un dieu, soit à un homme autre que le roi, sera jeté dans la fosse aux lions.
8 Sasa, ee mfalme, toa amri na uiandike ili isiweze kubadilishwa: kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Maintenant, ô roi, rends l'édit, et publie-le, afin que rien ne soit changé à ce qu'ont résolu les Perses et les Mèdes.
9 Hivyo Mfalme Dario akaiweka amri hiyo katika maandishi.
Et le roi Darius fit publier l'édit.
10 Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni.
Or Daniel, aussitôt qu'il sut ce que prescrivait l'édit, entra dans sa maison, à l'étage supérieur, les fenêtres ouvertes; tourné vers Jérusalem, trois fois par jour il se mit à genoux, priant son Dieu, et lui rendant grâces, comme il avait coutume de le faire auparavant.
11 Ndipo watu hawa wakaenda kama kikundi na kumkuta Danieli akiomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msaada.
Cependant ces hommes l'épièrent, et ils surprirent Daniel rendant grâces à son Dieu et lui faisant sa prière.
12 Basi wakaenda kwa mfalme na kusema naye kuhusu amri ya mfalme: “Je, hukutangaza amri kwamba kwa muda huu wa siku thelathini zijazo mtu yeyote ambaye atamwomba mungu au mwanadamu yeyote isipokuwa wewe, ee mfalme, angetupwa ndani ya tundu la simba?” Mfalme akajibu, “Amri ndivyo ilivyo, kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Et s'approchant du roi, ils lui dirent: Ô roi, n'as-tu point rendu cet édit, que tout homme qui, durant trente jours, fera une demande à un dieu ou à un homme autre que le roi, soit jeté dans la fosse aux lions? Et le roi répondit: Ce que vous dites est véritable, et l'édit des Perses et des Mèdes ne sera pas violé.
13 Ndipo wakamwambia mfalme, “Danieli, ambaye ni mmoja wa mahamisho kutoka Yuda, hakuheshimu, ee mfalme, wala hajali amri uliyoiweka kwa maandishi. Bado anaomba mara tatu kwa siku.”
Et ils reprirent, disant au roi: Daniel, l'un des fils des captifs de la Judée, ne s'est point soumis à ton édit, et trois fois par jour il demande à son Dieu ce qu'il veut lui demander.
14 Wakati mfalme aliposikia hili, akahuzunika mno. Akakusudia kumwokoa Danieli, hivyo akafanya kila jitihada ya kumwokoa hadi jua likatua.
Aussitôt que le roi eut oui ces paroles, il en fut fort contristé, et il fut combattu par le désir de sauver Daniel, et jusqu'au soir il fut combattu par le désir de le sauver.
15 Ndipo wale watu wakamwendea mfalme kama kikundi na kumwambia, “Ee mfalme, kumbuka kwamba kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, hakuna amri wala sheria ambayo mfalme ameitoa inayoweza kubadilishwa.”
Mais ces hommes dirent à Darius: Sache, ô roi, qu'il est réglé chez les Mèdes et les Perses que nul changement ne peut être fait à un édit, à un décret du roi.
16 Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, na wakamtupa ndani ya tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako unayemtumikia daima na akuokoe!”
Et le roi donna ses ordres, et l'on emmena Daniel, et on le jeta dans la fosse aux lions, et le roi dit à Daniel: Ton Dieu que tu sers avec constance, lui-même te délivrera.
17 Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.
Et l'on apporta une pierre, et on la posa sur l'ouverture de la fosse, et le roi la scella de son anneau et de l'anneau de ses grands, afin que rien concernant Daniel ne fût changé.
18 Kisha mfalme akarudi kwenye jumba lake la kifalme, naye usiku kucha hakula chakula wala kutumia viburudisho alivyoletewa. Lakini hakuweza kulala.
Et le roi rentra dans son palais; mais il se coucha sans avoir soupé; on ne lui présenta point d'aliments, et le sommeil s'éloigna de lui. Et Dieu ferma la gueule des lions, et ils ne firent aucun mal à Daniel.
19 Asubuhi na mapema, mfalme akaondoka na kuharakisha kwenda kwenye tundu la simba.
Et le roi se leva de grand matin, dès les premières lueurs du jour, et il alla en toute hâte à la fosse aux lions.
20 Wakati alipokaribia lile tundu, akamwita Danieli kwa sauti ya uchungu, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima, ameweza kukuokoa kwa simba?”
Et, quand il fut près de la fosse, il cria à haute voix: Daniel, serviteur du Dieu vivant, ton Dieu, que tu sers avec constance, a-t-il pu te sauver de la gueule des lions?
21 Danieli akajibu, “Ee mfalme, uishi milele!
Et Daniel dit à Darius: Roi, vis à jamais
22 Mungu wangu alimtuma malaika wake, naye akafunga vinywa vya hawa simba. Hawajanidhuru, kwa sababu nilionekana sina hatia mbele zake. Wala kamwe sijafanya jambo lolote baya mbele yako, ee mfalme.”
Mon Dieu m'a envoyé son ange, et il a fermé la gueule des lions, et ils ne m'ont fait aucun mal, parce qu'à ses yeux j'ai été trouvé juste, et qu'à ton égard, ô roi, je n'ai fait aucune offense.
23 Mfalme akafurahi mno, naye akatoa amri Danieli atolewe kutoka kwa lile tundu. Danieli alipotolewa kutoka kwa lile tundu, hakukutwa na jeraha lolote, kwa sababu alikuwa amemtumaini Mungu wake.
À ces mots le roi fut extrêmement réjoui, et il ordonna de retirer Daniel de la fosse, et il fut trouvé sain et sauf, parce qu'il avait mis sa confiance en Dieu.
24 Kwa amri ya mfalme, wale watu waliokuwa wamemshtaki Danieli kwa uongo waliletwa na kutupwa ndani ya lile tundu la simba, pamoja na wake zao na watoto wao. Nao kabla hawajafika chini kwenye sakafu ya lile tundu, simba wakawakamata na kusaga mifupa yao yote.
Et le roi donna ses ordres, et l'on amena les hommes qui avaient accusé Daniel, et on les jeta dans la fosse aux lions, eux, leurs fils et leurs femmes; et avant qu'ils eussent touché le fond de la fosse, les lions s'en emparèrent et leur broyèrent tous les os.
25 Kisha Mfalme Dario akawaandikia kabila zote za watu, mataifa, na watu wa kila lugha katika nchi yote: “Ninyi na mstawi sana!
Alors le roi Darius écrivit à tous les peuples, aux tribus, aux hommes de toutes langues, à tous les habitants de la terre: Que la paix se multiplie parmi vous!
26 “Natoa amri hii, kwamba katika kila sehemu ya ufalme wangu, lazima watu wamwogope na kumheshimu Mungu wa Danieli. “Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai, naye hudumu milele, ufalme wake hautaangamizwa, nao utawala wake hauna mwisho.
Le présent édit est rendu par moi pour toutes les principautés de mon royaume, afin que chacun soit plein de crainte et de tremblement devant la force du Dieu de Daniel; car lui seul est le Dieu vivant, et il demeure dans tous les siècles, et son royaume ne périra jamais, et son règne durera jusqu'à la fin des temps.
27 Huponya na kuokoa; hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani. Amemwokoa Danieli kutoka nguvu za simba.”
Il protège et il sauve, et il fait des signes et des miracles dans le ciel et sur la terre; c'est lui qui a tiré Daniel de la griffe des lions.
28 Hivyo Danieli akastawi wakati wa utawala wa Dario, na utawala wa Koreshi Mwajemi.
Et Daniel vécut plein de prospérité, sous le règne de Darius et sous le règne de Cyrus le Perse.

< Danieli 6 >