< Danieli 6 >
1 Ilimpendeza Dario kuteua wakuu 120 kutawala katika ufalme wake wote,
Il parut bon à Darius de préposer au royaume cent vingt préfets, pour gouverner tout le royaume.
2 pamoja na wasimamizi watatu juu yao, ambao mmoja wao alikuwa Danieli. Wakuu walitoa hesabu kwa hao wasimamizi ili mfalme asipate hasara.
Au-dessus d’eux il y avait trois ministres, dont était Daniel; c’est à eux que ces préfets devaient rendre des comptes, en sorte que le roi ne subît aucun dommage.
3 Basi Danieli alijidhihirisha, miongoni mwa wasimamizi na wakuu kwa sifa zake za kipekee hata mfalme akapanga kumweka juu ya ufalme wote.
Bientôt ce Daniel prit le dessus sur les ministres et les préfets, étant doué d’un esprit supérieur, et le roi projetait de le mettre à la tête de tout le royaume.
4 Walipofahamu hilo, wakuu na wasimamizi wakajaribu kutafuta sababu za kumshtaki Danieli kuhusu usimamizi wake wa shughuli za serikali, lakini hawakuweza kufanikiwa. Hawakuweza kupata kosa kwake, kwa sababu alikuwa mwaminifu, wala hakupatikana na upotovu au uzembe.
Alors les ministres et les préfets s’appliquèrent à trouver un grief contre Daniel, du chef de son gouvernement, mais ils ne purent découvrir ni grief, ni méfait, parce qu’il était loyal, de sorte que ni erreur ni faute ne purent être surprises chez lui.
5 Mwishoni watu hawa walisema, “Kamwe hatutapata msingi wa mashtaka dhidi ya huyu Danieli isipokuwa iwe inahusiana na sheria ya Mungu wake.”
Aussi ces hommes-là dirent: "Nous ne trouverons aucun grief contre ce Daniel, à moins que nous ne le prenions en défaut dans les choses de sa religion."
6 Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!
Aussitôt les ministres et les préfets se précipitèrent chez le roi et lui parlèrent ainsi: "Vive à jamais le roi Darius!
7 Wasimamizi wa ufalme, wasaidizi, wakuu, washauri na watawala wote wamekubaliana kwamba mfalme atoe sheria na kukazia amri kuwa yeyote atakayetoa dua kwa mungu au mwanadamu yeyote katika muda huu wa siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, ee mfalme, atupwe ndani ya tundu la simba.
Tous les ministres du royaume, les préfets, les satrapes, les conseillers et les gouverneurs se sont concertés pour faire établir une ordonnance royale et promulguer une défense déclarant que quiconque, durant trente jours, adresserait une prière à tout autre Dieu ou homme qu’à toi-même, ô roi, serait jeté dans la fosse aux lions.
8 Sasa, ee mfalme, toa amri na uiandike ili isiweze kubadilishwa: kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Donc, ô roi, établis la défense et rédige l’édit qui ne puisse être modifié, conformément à la loi immuable de Médie et de Perse."
9 Hivyo Mfalme Dario akaiweka amri hiyo katika maandishi.
En conséquence, le roi Darius rédigea l’édit et la défense.
10 Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni.
Or, Daniel, dès qu’il apprit que l’édit avait été rédigé, rentra chez lui. II avait, dans sa chambre supérieure, des fenêtres ouvertes dans la direction de Jérusalem, et trois fois par jour il se mettait à genoux, priant et louant Dieu tout comme il avait fait auparavant.
11 Ndipo watu hawa wakaenda kama kikundi na kumkuta Danieli akiomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msaada.
Cependant, ces mêmes hommes se précipitèrent et surprirent Daniel priant et implorant son Dieu.
12 Basi wakaenda kwa mfalme na kusema naye kuhusu amri ya mfalme: “Je, hukutangaza amri kwamba kwa muda huu wa siku thelathini zijazo mtu yeyote ambaye atamwomba mungu au mwanadamu yeyote isipokuwa wewe, ee mfalme, angetupwa ndani ya tundu la simba?” Mfalme akajibu, “Amri ndivyo ilivyo, kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Aussitôt ils se présentèrent devant le roi et l’entretinrent de la défense royale: "N’As-tu pas dirent-ils édicté une défense en vertu de laquelle tout homme qui, durant trente jours, adresserait une prière à tout autre Dieu ou homme que toi-même, ô roi, serait jeté dans la fosse aux lions?" Le roi répondit: "La chose est constante, conformément à la loi immuable de Médie et de Perse."
13 Ndipo wakamwambia mfalme, “Danieli, ambaye ni mmoja wa mahamisho kutoka Yuda, hakuheshimu, ee mfalme, wala hajali amri uliyoiweka kwa maandishi. Bado anaomba mara tatu kwa siku.”
Et eux de répliquer sur-le-champ au roi: "Daniel, qui fait partie des exilés de Judée, n’a tenu aucun compte de toi, ô roi, ni de la défense que tu as rédigée: trois fois par jour, il fait sa prière."
14 Wakati mfalme aliposikia hili, akahuzunika mno. Akakusudia kumwokoa Danieli, hivyo akafanya kila jitihada ya kumwokoa hadi jua likatua.
Dès que le roi entendit ces paroles, il en fut très peiné, et il prit à cœur de tirer Daniel d’affaire: jusqu’au coucher du soleil il avisa aux moyens de le sauver.
15 Ndipo wale watu wakamwendea mfalme kama kikundi na kumwambia, “Ee mfalme, kumbuka kwamba kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, hakuna amri wala sheria ambayo mfalme ameitoa inayoweza kubadilishwa.”
Mais alors ces gens firent irruption chez le roi et lui dirent: "Sache, ô roi, qu’une loi exige chez les Mèdes et les Perses que toute défense et tout édit établis par le roi soient immuables."
16 Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, na wakamtupa ndani ya tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako unayemtumikia daima na akuokoe!”
Là-dessus, le roi donna un ordre, on amena Daniel et on le jeta dans la fosse aux lions: "Puisse, lui dit le roi, ton Dieu que tu sers constamment te sauver!"
17 Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.
On apporta une pierre et on la posa sur l’orifice de la fosse; le roi la scella de son anneau et des anneaux de ses grands, pour qu’il n’y eût aucun revirement à l’égard de Daniel.
18 Kisha mfalme akarudi kwenye jumba lake la kifalme, naye usiku kucha hakula chakula wala kutumia viburudisho alivyoletewa. Lakini hakuweza kulala.
Ensuite, le roi rentra dans son palais et passa la nuit en jeûnant; il ne fit pas dresser la table devant lui, et le sommeil s’obstina à le fuir.
19 Asubuhi na mapema, mfalme akaondoka na kuharakisha kwenda kwenye tundu la simba.
Dès l’aube, quand le jour vint à poindre, le roi se leva et se rendit en toute hâte à la fosse aux lions.
20 Wakati alipokaribia lile tundu, akamwita Danieli kwa sauti ya uchungu, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima, ameweza kukuokoa kwa simba?”
Arrivé près de la fosse, il appela Daniel d’une voix attristée: "Daniel, serviteur du Dieu vivant, s’écria le roi en s’adressant à Daniel, ton Dieu que tu sers constamment a-t-il pu te préserver des lions?"
21 Danieli akajibu, “Ee mfalme, uishi milele!
Aussitôt Daniel parla au roi: "Vive, dit-il, le roi à jamais!
22 Mungu wangu alimtuma malaika wake, naye akafunga vinywa vya hawa simba. Hawajanidhuru, kwa sababu nilionekana sina hatia mbele zake. Wala kamwe sijafanya jambo lolote baya mbele yako, ee mfalme.”
Mon Dieu a envoyé son ange et fermé la gueule des lions, en sorte qu’ils ne m’ont fait aucun mal, parce que mon innocence a été reconnue par lui, de même qu’envers toi je n’ai commis aucun méfait."
23 Mfalme akafurahi mno, naye akatoa amri Danieli atolewe kutoka kwa lile tundu. Danieli alipotolewa kutoka kwa lile tundu, hakukutwa na jeraha lolote, kwa sababu alikuwa amemtumaini Mungu wake.
Alors le roi fut extrêmement content, et il ordonna de remonter Daniel de la fosse aux lions. Quand Daniel eut été remonté de la fosse, il ne portait aucune blessure, parce qu’il avait eu confiance en son Dieu.
24 Kwa amri ya mfalme, wale watu waliokuwa wamemshtaki Danieli kwa uongo waliletwa na kutupwa ndani ya lile tundu la simba, pamoja na wake zao na watoto wao. Nao kabla hawajafika chini kwenye sakafu ya lile tundu, simba wakawakamata na kusaga mifupa yao yote.
Puis, sur l’ordre du roi, on amena les hommes qui avaient dénoncé Daniel, et on les jeta dans la fosse aux lions, eux, leurs enfants et leurs femmes. Ils n’étaient pas encore arrivés au fond de la fosse, que les lions se jetèrent sur eux et leur broyèrent tous les membres.
25 Kisha Mfalme Dario akawaandikia kabila zote za watu, mataifa, na watu wa kila lugha katika nchi yote: “Ninyi na mstawi sana!
Alors le roi Darius manda à l’ensemble des nations, peuples et langues qui sont répandus sur toute la terre: "Que votre prospérité soit grande!
26 “Natoa amri hii, kwamba katika kila sehemu ya ufalme wangu, lazima watu wamwogope na kumheshimu Mungu wa Danieli. “Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai, naye hudumu milele, ufalme wake hautaangamizwa, nao utawala wake hauna mwisho.
L’Ordre est donné par moi que dans toute l’étendue de mon royaume on manifeste crainte et vénération pour le Dieu de Daniel car il est le Dieu vivant, et il subsiste éternellement; sa royauté est indestructible et sa dénomination sans fin.
27 Huponya na kuokoa; hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani. Amemwokoa Danieli kutoka nguvu za simba.”
Il préserve et il sauve, il accomplit des miracles et des prodiges au ciel et sur la terre, lui qui a sauvé Daniel de la griffe des lions."
28 Hivyo Danieli akastawi wakati wa utawala wa Dario, na utawala wa Koreshi Mwajemi.
Et ce même Daniel prospéra sous le règne de Darius et sous le règne de Cyrus le Perse.