< Danieli 6 >

1 Ilimpendeza Dario kuteua wakuu 120 kutawala katika ufalme wake wote,
It seemed good before Darius and he appointed over kingdom the satraps the one hundred and twenty who they will be over all kingdom the.
2 pamoja na wasimamizi watatu juu yao, ambao mmoja wao alikuwa Danieli. Wakuu walitoa hesabu kwa hao wasimamizi ili mfalme asipate hasara.
And above more than them overseers three whom Daniel [was] one of them whom they will be satraps the these giving to them report the and king the not he will be suffering injury.
3 Basi Danieli alijidhihirisha, miongoni mwa wasimamizi na wakuu kwa sifa zake za kipekee hata mfalme akapanga kumweka juu ya ufalme wote.
Then Daniel this he was distinguishing himself over overseers the and satraps the as to because that a spirit extraordinary [was] in him and king the [was] planning to appoint him over all kingdom the.
4 Walipofahamu hilo, wakuu na wasimamizi wakajaribu kutafuta sababu za kumshtaki Danieli kuhusu usimamizi wake wa shughuli za serikali, lakini hawakuweza kufanikiwa. Hawakuweza kupata kosa kwake, kwa sababu alikuwa mwaminifu, wala hakupatikana na upotovu au uzembe.
Then overseers the and satraps the they were seeking an occasion to find to Daniel from [the] side of kingdom the and any occasion and corruption not [they were] able to find as to because that [was] trustworthy he and any negligence and corruption not it was found concerning him.
5 Mwishoni watu hawa walisema, “Kamwe hatutapata msingi wa mashtaka dhidi ya huyu Danieli isipokuwa iwe inahusiana na sheria ya Mungu wake.”
Then men the these [were] saying that not we will find to Daniel this any occasion except we have found concerning him in [the] law of God his.
6 Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!
Then overseers the and satraps the these they came as a crowd to king the and as follows [they were] saying to him O Darius king the for ever live!
7 Wasimamizi wa ufalme, wasaidizi, wakuu, washauri na watawala wote wamekubaliana kwamba mfalme atoe sheria na kukazia amri kuwa yeyote atakayetoa dua kwa mungu au mwanadamu yeyote katika muda huu wa siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, ee mfalme, atupwe ndani ya tundu la simba.
They took counsel together all - [the] overseers of kingdom the prefects the and satraps the counselors the and governors the to establish [the] statute of king the and to make stringent a prohibition that every [one] who he will ask a petition from any god and person until days thirty except from you king O he will be thrown to [the] den of lions the.
8 Sasa, ee mfalme, toa amri na uiandike ili isiweze kubadilishwa: kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Now king O you will establish prohibition the so you may sign writing the which not to change according to [the] law of [the] Medes and [the] Persians which not it will pass away.
9 Hivyo Mfalme Dario akaiweka amri hiyo katika maandishi.
As to because this king the Darius he signed writing the and prohibition the.
10 Basi Danieli alipofahamu kuwa amri ile imetangazwa, alikwenda nyumbani kwenye chumba chake cha ghorofani ambako madirisha yalifunguka kuelekea Yerusalemu. Akapiga magoti na kuomba mara tatu kwa siku, akimshukuru Mungu wake kama alivyokuwa akifanya mwanzoni.
And Daniel as that he knew that it was signed writing the he went in to house his and windows [were] opened to it in upper room his facing Jerusalem and times three in day the he - [was] kneeling on knees his and [was] praying and [was] praising before God his as to because that he was doing from [the] former time of this.
11 Ndipo watu hawa wakaenda kama kikundi na kumkuta Danieli akiomba na kumsihi Mungu kwa ajili ya msaada.
Then men the these they came as a crowd and they found Daniel asking and imploring favor before God his.
12 Basi wakaenda kwa mfalme na kusema naye kuhusu amri ya mfalme: “Je, hukutangaza amri kwamba kwa muda huu wa siku thelathini zijazo mtu yeyote ambaye atamwomba mungu au mwanadamu yeyote isipokuwa wewe, ee mfalme, angetupwa ndani ya tundu la simba?” Mfalme akajibu, “Amri ndivyo ilivyo, kulingana na sheria za Wamedi na Waajemi, ambazo haziwezi kubatilishwa.”
Then they approached and [were] saying before king the concerning [the] prohibition of king the ¿ not a prohibition did you sign that every person who he will ask from any god and person until days thirty except from you king O he will be thrown to [the] den of lions the [was] replying king the and saying [is] certain word the according to [the] law of [the] Medes and [the] Persians which not it will pass away.
13 Ndipo wakamwambia mfalme, “Danieli, ambaye ni mmoja wa mahamisho kutoka Yuda, hakuheshimu, ee mfalme, wala hajali amri uliyoiweka kwa maandishi. Bado anaomba mara tatu kwa siku.”
Then they replied and [were] saying before king the that Daniel who [is] one of [the] sons of exile the of Judah not he has set (to you *Q(k)*) king O discretion and to prohibition the which you signed and times three in day the [he is] asking petition his.
14 Wakati mfalme aliposikia hili, akahuzunika mno. Akakusudia kumwokoa Danieli, hivyo akafanya kila jitihada ya kumwokoa hadi jua likatua.
Then king the as that word the he heard exceedingly it was displeasing to him and concerning Daniel he set mind to deliver him and until [the] goings in of sun the he was striving to rescue him.
15 Ndipo wale watu wakamwendea mfalme kama kikundi na kumwambia, “Ee mfalme, kumbuka kwamba kulingana na sheria ya Wamedi na Waajemi, hakuna amri wala sheria ambayo mfalme ameitoa inayoweza kubadilishwa.”
Then men the these they came as a crowd to king the and [were] saying to king the know king O that [the] law of [the] Medes and [the] Persians that any prohibition and statute which king the he will establish not to change.
16 Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, na wakamtupa ndani ya tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako unayemtumikia daima na akuokoe!”
Then king the he said and they brought Daniel and they threw [him] to den the of lions the [was] replying king the and [was] saying to Daniel God your whom (you *Q(k)*) [are] paying reverence to him in continuance he may he deliver you.
17 Jiwe likaletwa na kuwekwa kwenye mdomo wa tundu, naye mfalme akalitia muhuri kwa pete yake mwenyewe pamoja na kwa pete za wakuu wake, ili hali ya Danieli isiweze kubadilishwa.
And it was brought a stone one and it was set over [the] mouth of den the and he sealed it king the with signet-ring his and with [the] signet-rings of nobles his that not it will change anything with Daniel.
18 Kisha mfalme akarudi kwenye jumba lake la kifalme, naye usiku kucha hakula chakula wala kutumia viburudisho alivyoletewa. Lakini hakuweza kulala.
Then he went king the to palace his and he passed [the] night fasting and thrusting [women] not he brought in before him and sleep his it fled on him.
19 Asubuhi na mapema, mfalme akaondoka na kuharakisha kwenda kwenye tundu la simba.
Then king the at dawn he arose at daylight the and in haste to den the of lions the he went.
20 Wakati alipokaribia lile tundu, akamwita Danieli kwa sauti ya uchungu, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima, ameweza kukuokoa kwa simba?”
And just as approached he to den the to Daniel with a voice pained he cried out [was] replying king the and [was] saying to Daniel O Daniel [the] servant of God the living God your whom (you *Q(k)*) [are] paying reverence to him in continuance ¿ was he able to deliver you from lions the.
21 Danieli akajibu, “Ee mfalme, uishi milele!
Then Daniel with king the he spoke king O for ever live!
22 Mungu wangu alimtuma malaika wake, naye akafunga vinywa vya hawa simba. Hawajanidhuru, kwa sababu nilionekana sina hatia mbele zake. Wala kamwe sijafanya jambo lolote baya mbele yako, ee mfalme.”
God my he sent angel his and he closed [the] mouth of lions the and not they harmed me as to because that before him innocence it was found to me and also (before you *Q(k)*) king O a hurtful act not I have done.
23 Mfalme akafurahi mno, naye akatoa amri Danieli atolewe kutoka kwa lile tundu. Danieli alipotolewa kutoka kwa lile tundu, hakukutwa na jeraha lolote, kwa sababu alikuwa amemtumaini Mungu wake.
Then king the exceedingly it was good to him and Daniel he said to take up from den the and he was taken up Daniel from den the and any hurt not it was found on him that he had trusted in God his.
24 Kwa amri ya mfalme, wale watu waliokuwa wamemshtaki Danieli kwa uongo waliletwa na kutupwa ndani ya lile tundu la simba, pamoja na wake zao na watoto wao. Nao kabla hawajafika chini kwenye sakafu ya lile tundu, simba wakawakamata na kusaga mifupa yao yote.
And he said king the and they brought men the these who they had eaten pieces his of Daniel and to [the] den of lions the they threw they sons their and wives their and not they reached to [the] bottom of den the until that they assaulted them lions the and all bones their they shattered.
25 Kisha Mfalme Dario akawaandikia kabila zote za watu, mataifa, na watu wa kila lugha katika nchi yote: “Ninyi na mstawi sana!
Then Darius king the he wrote to all peoples the nations the and languages the which ([were] dwelling *Q(k)*) in all earth the peace your may it increase.
26 “Natoa amri hii, kwamba katika kila sehemu ya ufalme wangu, lazima watu wamwogope na kumheshimu Mungu wa Danieli. “Kwa maana yeye ni Mungu aliye hai, naye hudumu milele, ufalme wake hautaangamizwa, nao utawala wake hauna mwisho.
From before me it is made a decree that - in all [the] dominion of kingdom my they will be (trembling *Q(k)*) and fearing from before God his of Daniel that he - [is] God the living and enduring for ever and kingdom his which not it will be destroyed and dominion his [is] to end the.
27 Huponya na kuokoa; hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani. Amemwokoa Danieli kutoka nguvu za simba.”
[he is] delivering And [he is] rescuing and [he is] doing signs and wonders in heavens the and on earth the who he has delivered Daniel from [the] hand of lions the.
28 Hivyo Danieli akastawi wakati wa utawala wa Dario, na utawala wa Koreshi Mwajemi.
And Daniel this he prospered in [the] reign of Darius and in [the] reign of Cyrus (Persian the. *Q(k)*)

< Danieli 6 >