< Danieli 5 >

1 Mfalme Belshaza alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakuu wake na akanywa mvinyo pamoja nao.
Belshazzar, the king gave a great feast to his thousands lords, and drank wine before the thousand.
2 Wakati Belshaza alipokuwa akinywa mvinyo wake, aliamuru viletwe vile vikombe vya dhahabu na fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekaluni huko Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake waweze kuvinywea.
Belshazzar, while he tasted the wine, commanded to bring the golden and silver vessels which his father Nebuchadnezzar had taken out of the temple at Jerusalem; that the king and his princes, his wives and his concubines, might drink therein.
3 Kwa hiyo wakavileta vile vikombe vya dhahabu ambavyo vilikuwa vimechukuliwa kutoka Hekalu la Mungu huko Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake wakavinywea.
Then they brought the golden vessels that were taken out of the temple of the house of God at Jerusalem; and the king and his princes, his wives and his concubines, drank in them.
4 Walipokuwa wakinywa mvinyo, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, ya shaba, chuma, miti na mawe.
They drank wine, and praised the gods of gold and of silver, of brass, of iron, of wood, and of stone.
5 Ghafula vidole vya mkono wa mwanadamu vilitokea na kuandika juu ya ukuta, karibu na kinara cha taa ndani ya jumba la mfalme. Mfalme akatazama kitanga kilivyokuwa kikiandika.
In the same hour came forth fingers of a man's hand, and wrote over against the chandelier upon the plaster of the wall of the king's palace; and the king saw the hand that wrote.
6 Uso wa mfalme ukageuka rangi, naye akaogopa sana, kiasi kwamba magoti yake yaligongana na miguu yake ikalegea.
Then the king's countenance was changed, and his thoughts troubled him, so that the joints of his loins were loosened, and his knees smote one against the other.
7 Mfalme akawaita wasihiri, wanajimu na waganga waletwe, naye akawaambia hawa wenye hekima wa Babeli, “Yeyote asomaye maandishi haya na kuniambia maana yake atavikwa nguo za zambarau, na kuvikwa mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atafanywa mtawala wa cheo cha tatu katika ufalme.”
The king cried aloud to bring in the magicians, the Chaldaeans, and the astrologers. And the king spake and said to the wise men of Babylon, Whoever shall read this writing, and show me the interpretation thereof, shall be clothed with purple, and have a chain of gold about his neck, and shall rule as the third in the kingdom.
8 Ndipo watu wote wa mfalme wenye hekima wakaingia, lakini hawakuweza kusoma yale maandishi wala kumwambia mfalme maana yake.
Then all the king's wise men came in; but they could not read the writing, nor make known to the king its signification.
9 Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.
Then was King Belshazzar in great consternation, and his countenance was changed, and his lords were amazed.
10 Malkia aliposikia sauti za mfalme na wakuu wake, alikuja katika ukumbi wa karamu. Akasema, “Ee mfalme, uishi milele! Usishtuke! Usibadilike rangi kiasi hicho!
Then the queen, on account of this affair of the king and his lords, came into the banquet-house; and the queen spake and said, O king, live forever! Let not thy thoughts terrify thee, nor let thy countenance be changed.
11 Yuko mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu mitakatifu ndani yake. Wakati wa baba yako, mtu huyo alionekana kuwa na ufahamu, akili na hekima kama ile ya miungu. Mfalme Nebukadneza baba yako, yaani nasema mfalme baba yako, alimweka kuwa mkuu wa waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi.
There is a man in thy kingdom in whom is the spirit of the holy gods; and in the days of thy father, light and understanding and wisdom, like the wisdom of the gods, were found in him; and the king Nebuchadnezzar, thy father, made him chief of the scribes, the magicians, the Chaldeans, and the astrologers, thy father, O king!
12 Mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alionekana kuwa na akili nyepesi, maarifa na ufahamu, pia uwezo wa kufasiri ndoto, kueleza mafumbo na kutatua matatizo magumu. Mwite Danieli, naye atakuambia maana ya haya maandishi.”
forasmuch as an excellent spirit and knowledge and understanding to interpret dreams, and to explain hard sentences, and solve difficult questions were found in him, in Daniel, whom the king named Belteshazzar; now let Daniel be called, and he will show the interpretation.
13 Hivyo Danieli akaletwa mbele ya mfalme, naye mfalme akamuuliza, “Je, wewe ndiwe Danieli, mmoja wa watu wa uhamisho walioletwa na mfalme baba yangu kutoka Yuda?
Then was Daniel brought in before the king. And the king spake and said to Daniel, Art thou that Daniel, of the captives of Judah, whom the king, my father, brought out of Judaea?
14 Nimesikia kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na kwamba una ufahamu, akili na hekima ya pekee.
I have heard concerning thee, that the spirit of the gods is in thee, and that light and understanding and excellent wisdom are found in thee.
15 Watu wenye hekima na wasihiri waliletwa mbele yangu ili kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, lakini hawakuweza kunifafanulia.
And now the wise men and the magicians have been brought in before me, that they might read this writing, and make known to me its signification; but they could not show the signification of the thing.
16 Basi nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo magumu. Ikiwa unaweza kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utafanywa mtawala wa tatu katika ufalme.”
But I have heard of thee that thou canst give interpretations, and solve difficult questions. Now if thou canst read the writing and make known to me its signification, thou shalt be clothed with purple, and have a chain of gold about thy neck, and shalt rule as the third in the kingdom.
17 Ndipo Danieli akamjibu mfalme, “Waweza kubaki na zawadi zako mwenyewe na kumpa mtu mwingine zawadi zako. Hata hivyo, nitasoma maandishi kwa mfalme na kumwambia maana yake.
Then answered Daniel and said before the king, Let thy gifts be to thyself, and give thy rewards to another: yet I will read the writing to the king, and make known to him the signification.
18 “Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Sana alimpa baba yako Nebukadneza utawala, ukuu, utukufu na fahari.
O king, the Most High God gave to Nebuchadnezzar, thy father, a kingdom, and majesty, and glory, and honor.
19 Kwa sababu ya nafasi ya juu aliyompa baba yako, kabila zote za watu, mataifa na watu wa kila lugha walimhofu na kumwogopa. Wale ambao mfalme alitaka kuwaua, aliwaua; wale aliotaka kuwaacha hai, aliwaacha hai; wale aliotaka kuwapandisha cheo, aliwapandisha; aliotaka kuwashusha, aliwashusha.
And by reason of the majesty which he gave him, all people, nations, and languages trembled and feared before him; whom he would he slew, and whom he would he kept alive; whom he would he set up, and whom he would he put down.
20 Lakini moyo wake ulipokuwa na majivuno na kuwa mgumu kwa kiburi, aliondolewa kutoka kwa kiti chake cha ufalme na kuvuliwa utukufu wake.
But when his heart was lifted up, and his spirit hardened in pride, he was thrust down from his kingly throne, and his glory was taken from him.
21 Akafukuzwa mbali na wanadamu na kupewa akili ya mnyama, akaishi pamoja na punda-mwitu, akala majani kama ngʼombe, nao mwili wake ukaloweshwa kwa umande wa mbingu, mpaka alipotambua kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye mtawala juu ya falme za wanadamu na kwamba humtawaza juu yao yeyote amtakaye.
And he was driven from the sons of men; and his heart became like the beasts, and his dwelling was with wild asses; he was fed with grass like oxen, and his body was wet with the dew of heaven; till he knew that the Most High God ruled in the kingdoms of men, and set up over them whomsoever he would.
22 “Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote.
And thou, his son, O Belshazzar, hast not humbled thy heart, though thou knewest all this;
23 Badala yake, umejiinua dhidi ya Bwana wa mbingu. Uliletewa vikombe vya Hekalu lake, nawe na wakuu wako, wake zako na masuria wako mlivitumia kwa kunywea mvinyo. Ukaisifu miungu ya fedha na dhahabu, ya shaba, chuma, miti na mawe, miungu ambayo haiwezi kuona, au kusikia wala kufahamu. Lakini hukumheshimu Mungu ambaye anaushikilia uhai wako na njia zako zote mkononi mwake.
but hast lifted thyself up against the Lord of heaven; and the vessels of his house have been brought before thee, and thou, and thy lords, thy wives, and thy concubines have drunk wine in them; and thou hast praised the gods of silver and gold, of brass, iron, wood, and stone, which see not, nor hear, nor know; and the God in whose hand is thy breath, and whose are all thy ways, thou hast not honored.
24 Kwa hiyo ameutuma mkono ule ulioandika maneno.
Then was sent from him the hand, and this writing was written.
25 “Haya ndiyo maneno yaliyoandikwa: mene, mene, tekeli na peresi
And this is the writing which was written: Numbered, Numbered, Weighed, and To be Divided.
26 “Hii ndiyo maana ya maneno haya: “Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.
And this is the interpretation of it. Numbered: God hath numbered thy kingdom, and made an end of it.
27 Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.
Weighed: Thou art weighed in the balances, and found wanting.
28 Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”
Divided: Thy kingdom is divided, and given to the Medes and Persians.
29 Ndipo kwa amri ya Belshaza, Danieli akavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni, tena akatangazwa kuwa mtawala wa tatu katika ufalme.
Then Belshazzar commanded, and they clothed Daniel with purple, and put a chain of gold about his neck, and made a proclamation concerning him that he should be third ruler in the kingdom.
30 Usiku ule ule, Belshaza mfalme wa Wakaldayo akauawa,
In the same night was Belshazzar, the king of the Chaldaeans, slain;
31 naye Dario Mmedi akashika ufalme akiwa na miaka sitini na miwili.
and Darius the Mede took the kingdom, being about sixty-two years old.

< Danieli 5 >