< Danieli 5 >
1 Mfalme Belshaza alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakuu wake na akanywa mvinyo pamoja nao.
Belshazzar the king has made a great feast to one thousand of his great men, and before the one thousand he is drinking wine;
2 Wakati Belshaza alipokuwa akinywa mvinyo wake, aliamuru viletwe vile vikombe vya dhahabu na fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekaluni huko Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake waweze kuvinywea.
Belshazzar has said—while tasting the wine—to bring in the vessels of gold and of silver that his father Nebuchadnezzar had taken from the temple that [is] in Jerusalem, that the king may drink with them, and his great men, his wives, and his concubines.
3 Kwa hiyo wakavileta vile vikombe vya dhahabu ambavyo vilikuwa vimechukuliwa kutoka Hekalu la Mungu huko Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake wakavinywea.
Then they have brought in the vessels of gold that had been taken out of the temple of the house of God that [is] in Jerusalem, and the king and his great men, his wives and his concubines, have drunk with them;
4 Walipokuwa wakinywa mvinyo, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, ya shaba, chuma, miti na mawe.
they have drunk wine, and have praised the gods of gold, and of silver, of bronze, of iron, of wood, and of stone.
5 Ghafula vidole vya mkono wa mwanadamu vilitokea na kuandika juu ya ukuta, karibu na kinara cha taa ndani ya jumba la mfalme. Mfalme akatazama kitanga kilivyokuwa kikiandika.
In that hour fingers of a man’s hand have come forth, and they are writing in front of the lampstand, on the plaster of the wall of the king’s palace: and the king is seeing the extremity of the hand that is writing;
6 Uso wa mfalme ukageuka rangi, naye akaogopa sana, kiasi kwamba magoti yake yaligongana na miguu yake ikalegea.
then the king’s countenance has changed, and his thoughts trouble him, and the joints of his loins are loosed, and his knees are striking against one another.
7 Mfalme akawaita wasihiri, wanajimu na waganga waletwe, naye akawaambia hawa wenye hekima wa Babeli, “Yeyote asomaye maandishi haya na kuniambia maana yake atavikwa nguo za zambarau, na kuvikwa mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atafanywa mtawala wa cheo cha tatu katika ufalme.”
The king calls mightily, to bring up the enchanters, the Chaldeans, and the soothsayers. The king has answered and said to the wise men of Babylon, that, “Any man who reads this writing, and shows me its interpretation, he puts on purple, and a bracelet of gold [is] on his neck, and he rules third in the kingdom.”
8 Ndipo watu wote wa mfalme wenye hekima wakaingia, lakini hawakuweza kusoma yale maandishi wala kumwambia mfalme maana yake.
Then all the wise men of the king are coming up, and they are not able to read the writing, and to make known the interpretation to the king;
9 Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.
then King Belshazzar is greatly troubled, and his countenance is changing in him, and his great men are perplexed.
10 Malkia aliposikia sauti za mfalme na wakuu wake, alikuja katika ukumbi wa karamu. Akasema, “Ee mfalme, uishi milele! Usishtuke! Usibadilike rangi kiasi hicho!
The queen, on account of the words of the king and his great men, has come up to the banquet-house. The queen has answered and said, “O king, live for all ages; do not let your thoughts trouble you, nor your countenance be changed:
11 Yuko mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu mitakatifu ndani yake. Wakati wa baba yako, mtu huyo alionekana kuwa na ufahamu, akili na hekima kama ile ya miungu. Mfalme Nebukadneza baba yako, yaani nasema mfalme baba yako, alimweka kuwa mkuu wa waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi.
there is a man in your kingdom in whom [is] the spirit of the holy gods: and in the days of your father, light, and understanding, and wisdom—as the wisdom of the gods—was found in him; and your father King Nebuchadnezzar, chief of the scribes, enchanters, Chaldeans, soothsayers, established him—your father, O king—
12 Mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alionekana kuwa na akili nyepesi, maarifa na ufahamu, pia uwezo wa kufasiri ndoto, kueleza mafumbo na kutatua matatizo magumu. Mwite Danieli, naye atakuambia maana ya haya maandishi.”
because that an excellent spirit, and knowledge, and understanding, interpreting of dreams, and showing of enigmas, and loosing of knots was found in him, in Daniel, whose name the king made Belteshazzar: now let Daniel be called, and the interpretation he shows.”
13 Hivyo Danieli akaletwa mbele ya mfalme, naye mfalme akamuuliza, “Je, wewe ndiwe Danieli, mmoja wa watu wa uhamisho walioletwa na mfalme baba yangu kutoka Yuda?
Then Daniel has been caused to come up before the king; the king has answered and said to Daniel, “You are that Daniel who [is] of the sons of the expulsion of Judah, whom my father the king brought in out of Judah?
14 Nimesikia kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na kwamba una ufahamu, akili na hekima ya pekee.
And I have heard of you, that the spirit of the gods [is] in you, and light, and understanding, and excellent wisdom have been found in you.
15 Watu wenye hekima na wasihiri waliletwa mbele yangu ili kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, lakini hawakuweza kunifafanulia.
And now, caused to come up before me have been the wise men, the enchanters, that they may read this writing, and its interpretation to cause me to know: and they are not able to show the interpretation of the thing:
16 Basi nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo magumu. Ikiwa unaweza kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utafanywa mtawala wa tatu katika ufalme.”
and I have heard of you, that you are able to give interpretations, and to loose knots: now, behold—you are able to read the writing, and its interpretation to cause me to know—purple you put on, and a bracelet of gold [is] on your neck, and you rule third in the kingdom.”
17 Ndipo Danieli akamjibu mfalme, “Waweza kubaki na zawadi zako mwenyewe na kumpa mtu mwingine zawadi zako. Hata hivyo, nitasoma maandishi kwa mfalme na kumwambia maana yake.
Then Daniel has answered and said before the king, “Your gifts be to yourself, and give your fee to another; nevertheless, the writing I read to the king, and the interpretation I cause him to know;
18 “Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Sana alimpa baba yako Nebukadneza utawala, ukuu, utukufu na fahari.
you, O king, God Most High, a kingdom, and greatness, and glory, and honor, gave to your father Nebuchadnezzar:
19 Kwa sababu ya nafasi ya juu aliyompa baba yako, kabila zote za watu, mataifa na watu wa kila lugha walimhofu na kumwogopa. Wale ambao mfalme alitaka kuwaua, aliwaua; wale aliotaka kuwaacha hai, aliwaacha hai; wale aliotaka kuwapandisha cheo, aliwapandisha; aliotaka kuwashusha, aliwashusha.
and because of the greatness that He gave to him, all peoples, nations, and languages were trembling and fearing before him: whom he willed he was slaying, and whom he willed he was keeping alive, and whom he willed he was raising up, and whom he willed he was making low;
20 Lakini moyo wake ulipokuwa na majivuno na kuwa mgumu kwa kiburi, aliondolewa kutoka kwa kiti chake cha ufalme na kuvuliwa utukufu wake.
and when his heart was high, and his spirit was strong to act proudly, he has been caused to come down from the throne of his kingdom, and his glory they have caused to pass away from him,
21 Akafukuzwa mbali na wanadamu na kupewa akili ya mnyama, akaishi pamoja na punda-mwitu, akala majani kama ngʼombe, nao mwili wake ukaloweshwa kwa umande wa mbingu, mpaka alipotambua kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye mtawala juu ya falme za wanadamu na kwamba humtawaza juu yao yeyote amtakaye.
and he is driven from the sons of men, and his heart has been like with the beasts, and with the wild donkeys [is] his dwelling; they cause him to eat the herb like oxen, and by the dew of the heavens is his body wet, until he has known that God Most High is ruler in the kingdom of men, and whom He wills He raises up over it.
22 “Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote.
And you, his son, Belshazzar, have not humbled your heart, though all this you have known;
23 Badala yake, umejiinua dhidi ya Bwana wa mbingu. Uliletewa vikombe vya Hekalu lake, nawe na wakuu wako, wake zako na masuria wako mlivitumia kwa kunywea mvinyo. Ukaisifu miungu ya fedha na dhahabu, ya shaba, chuma, miti na mawe, miungu ambayo haiwezi kuona, au kusikia wala kufahamu. Lakini hukumheshimu Mungu ambaye anaushikilia uhai wako na njia zako zote mkononi mwake.
and against the Lord of the heavens you have lifted up yourself; and the vessels of His house they have brought in before you, and you, and your great men, your wives, and your concubines, are drinking wine with them, and gods of silver, and of gold, of bronze, of iron, of wood, and of stone, that are not seeing, nor hearing, nor knowing, you have praised: and the God in whose hand [is] your breath, and all your ways, Him you have not honored.
24 Kwa hiyo ameutuma mkono ule ulioandika maneno.
Then from before Him is the extremity of the hand sent, and the writing is noted down;
25 “Haya ndiyo maneno yaliyoandikwa: mene, mene, tekeli na peresi
and this [is] the writing that is noted down: Numbered, Numbered, Weighed, and Divided.
26 “Hii ndiyo maana ya maneno haya: “Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.
This [is] the interpretation of the thing: Numbered—God has numbered your kingdom, and has finished it.
27 Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.
Weighed—You are weighed in the balances, and have been found lacking.
28 Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”
Divided—Your kingdom is divided, and it has been given to the Medes and Persians.”
29 Ndipo kwa amri ya Belshaza, Danieli akavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni, tena akatangazwa kuwa mtawala wa tatu katika ufalme.
Then Belshazzar has spoken, and they have clothed Daniel with purple, and a bracelet of gold [is] on his neck, and they have proclaimed concerning him that he is the third ruler in the kingdom.
30 Usiku ule ule, Belshaza mfalme wa Wakaldayo akauawa,
In that night Belshazzar king of the Chaldeans is slain,
31 naye Dario Mmedi akashika ufalme akiwa na miaka sitini na miwili.
and Darius the Mede has received the kingdom when a son of sixty-two years.