< Danieli 5 >
1 Mfalme Belshaza alifanya karamu kubwa kwa ajili ya maelfu ya wakuu wake na akanywa mvinyo pamoja nao.
King Belshazzar made a great feast to a thousand of his princes, and dranke wine before the thousand.
2 Wakati Belshaza alipokuwa akinywa mvinyo wake, aliamuru viletwe vile vikombe vya dhahabu na fedha ambavyo Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua kutoka hekaluni huko Yerusalemu, ili mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake waweze kuvinywea.
And Belshazzar whiles he tasted the wine, commanded to bring him the golden and siluer vessels, which his father Nebuchad-nezzar had brought from the Temple in Ierusalem, that the King and his princes, his wiues, and his concubines might drinke therein.
3 Kwa hiyo wakavileta vile vikombe vya dhahabu ambavyo vilikuwa vimechukuliwa kutoka Hekalu la Mungu huko Yerusalemu, naye mfalme na wakuu wake, wake zake na masuria wake wakavinywea.
Then were brought the golden vessels, that were taken out of the Temple of the Lords house at Ierusalem, and the King and his princes, his wiues and his concubines dranke in them.
4 Walipokuwa wakinywa mvinyo, wakaisifu miungu ya dhahabu na fedha, ya shaba, chuma, miti na mawe.
They drunke wine and praysed the gods of golde, and of siluer, of brasse, of yron, of wood and of stone.
5 Ghafula vidole vya mkono wa mwanadamu vilitokea na kuandika juu ya ukuta, karibu na kinara cha taa ndani ya jumba la mfalme. Mfalme akatazama kitanga kilivyokuwa kikiandika.
At the same houre appeared fingers of a mans hand, which wrote ouer against the candlesticke vpon the plaister of the wall of ye Kings palace, and the King sawe the palme of the hand that wrote.
6 Uso wa mfalme ukageuka rangi, naye akaogopa sana, kiasi kwamba magoti yake yaligongana na miguu yake ikalegea.
Then the Kings countenance was changed, and his thoughtes troubled him, so that the ioynts of his loynes were loosed, and his knees smote one against the other.
7 Mfalme akawaita wasihiri, wanajimu na waganga waletwe, naye akawaambia hawa wenye hekima wa Babeli, “Yeyote asomaye maandishi haya na kuniambia maana yake atavikwa nguo za zambarau, na kuvikwa mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atafanywa mtawala wa cheo cha tatu katika ufalme.”
Wherefore the King cryed loude, that they should bring the astrologians, the Caldeans and the soothsayers. And the King spake, and sayd to the wise men of Babel, Whosoeuer can reade this writing, and declare me the interpretation thereof, shalbe clothed with purple, and shall haue a chaine of golde about his necke, and shall be the third ruler in the kingdome.
8 Ndipo watu wote wa mfalme wenye hekima wakaingia, lakini hawakuweza kusoma yale maandishi wala kumwambia mfalme maana yake.
Then came all the Kings wise men, but they could neither reade the writing, nor shewe the King the interpretation.
9 Basi Mfalme Belshaza akazidi kujawa na hofu, na uso wake ukageuka rangi zaidi. Wakuu wake wakapigwa na bumbuazi.
Then was King Belshazzar greatly troubled, and his countenance was changed in him, and his princes were astonied.
10 Malkia aliposikia sauti za mfalme na wakuu wake, alikuja katika ukumbi wa karamu. Akasema, “Ee mfalme, uishi milele! Usishtuke! Usibadilike rangi kiasi hicho!
Now the Queene by reason of the talke of the King, and his princes came into the banket house, and the Queene spake, and sayd, O King, liue for euer: let not thy thoughtes trouble thee, nor let thy countenance be changed.
11 Yuko mtu katika ufalme wako ambaye ana roho ya miungu mitakatifu ndani yake. Wakati wa baba yako, mtu huyo alionekana kuwa na ufahamu, akili na hekima kama ile ya miungu. Mfalme Nebukadneza baba yako, yaani nasema mfalme baba yako, alimweka kuwa mkuu wa waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi.
There is a man in thy kingdome, in whom is the spirit of the holy gods, and in the dayes of thy father light and vnderstanding and wisdome like the wisdome of the gods, was found in him: whom the King Nebuchad-nezzar thy father, the King, I say, thy father, made chiefe of the enchanters, astrologians, Caldeans, and soothsayers,
12 Mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alionekana kuwa na akili nyepesi, maarifa na ufahamu, pia uwezo wa kufasiri ndoto, kueleza mafumbo na kutatua matatizo magumu. Mwite Danieli, naye atakuambia maana ya haya maandishi.”
Because a more excellent spirit, and knowledge, and vnderstanding (for hee did expound dreames, and declare hard sentences, and dissolued doubtes) were founde in him, euen in Daniel, whome the King named Belteshazzar: nowe let Daniel be called, and hee will declare the interpretation.
13 Hivyo Danieli akaletwa mbele ya mfalme, naye mfalme akamuuliza, “Je, wewe ndiwe Danieli, mmoja wa watu wa uhamisho walioletwa na mfalme baba yangu kutoka Yuda?
Then was Daniel brought before the King, and the King spake and sayd vnto Daniel, Art thou that Daniel, which art of the children of the captiuitie of Iudah, whom my father the King brought out of Iewrie?
14 Nimesikia kwamba roho ya miungu iko ndani yako, na kwamba una ufahamu, akili na hekima ya pekee.
Now I haue heard of thee, that the spirit of the holy gods is in thee, and that light and vnderstanding and excellent wisdome is found in thee.
15 Watu wenye hekima na wasihiri waliletwa mbele yangu ili kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, lakini hawakuweza kunifafanulia.
Now therefore, wisemen and astrologians haue bene brought before me, that they should reade this writing, and shewe me the interpretation thereof: but they could not declare the interpretation of the thing.
16 Basi nimesikia kwamba unaweza kutoa tafsiri na kutatua matatizo magumu. Ikiwa unaweza kusoma maandishi haya na kuniambia maana yake, utavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni mwako, nawe utafanywa mtawala wa tatu katika ufalme.”
Then heard I of thee, that thou couldest shewe interpretations, and dissolue doutes: nowe if thou canst reade the writing, and shew me the interpretation thereof, thou shalt be clothed with purple, and shalt haue a chaine of golde about thy necke, and shalt be the third ruler in the kingdome.
17 Ndipo Danieli akamjibu mfalme, “Waweza kubaki na zawadi zako mwenyewe na kumpa mtu mwingine zawadi zako. Hata hivyo, nitasoma maandishi kwa mfalme na kumwambia maana yake.
Then Daniel answered, and sayd before the King, Keepe thy rewards to thy selfe, and giue thy giftes to another: yet I will reade the writing vnto the King, and shew him the interpretation.
18 “Ee mfalme, Mungu Aliye Juu Sana alimpa baba yako Nebukadneza utawala, ukuu, utukufu na fahari.
O King, heare thou, The most high God gaue vnto Nebuchad-nezzar thy father a kingdome, and maiestie, and honour and glory.
19 Kwa sababu ya nafasi ya juu aliyompa baba yako, kabila zote za watu, mataifa na watu wa kila lugha walimhofu na kumwogopa. Wale ambao mfalme alitaka kuwaua, aliwaua; wale aliotaka kuwaacha hai, aliwaacha hai; wale aliotaka kuwapandisha cheo, aliwapandisha; aliotaka kuwashusha, aliwashusha.
And for the maiestie that he gaue him, all people, nations, and languages trembled, and feared before him: he put to death whom he would: he smote whome he would: whome he would he set vp, and whome he would he put downe.
20 Lakini moyo wake ulipokuwa na majivuno na kuwa mgumu kwa kiburi, aliondolewa kutoka kwa kiti chake cha ufalme na kuvuliwa utukufu wake.
But when his heart was puft vp, and his minde hardened in pride, hee was deposed from his kingly throne, and they tooke his honour from him.
21 Akafukuzwa mbali na wanadamu na kupewa akili ya mnyama, akaishi pamoja na punda-mwitu, akala majani kama ngʼombe, nao mwili wake ukaloweshwa kwa umande wa mbingu, mpaka alipotambua kwamba Mungu Aliye Juu Sana ndiye mtawala juu ya falme za wanadamu na kwamba humtawaza juu yao yeyote amtakaye.
And hee was driuen from the sonnes of men, and his heart was made like the beastes, and his dwelling was with the wilde asses: they fed him with grasse like oxen, and his body was wet with the dewe of the heauen, till he knewe, that the most high God bare rule ouer the kingdome of men, and that he appointeth ouer it, whomsoeuer he pleaseth.
22 “Lakini wewe mwanawe, ee Belshaza, hukujinyenyekeza, ingawa ulifahamu haya yote.
And thou his sonne, O Belshazzar, hast not humbled thine heart, though thou knewest all these things,
23 Badala yake, umejiinua dhidi ya Bwana wa mbingu. Uliletewa vikombe vya Hekalu lake, nawe na wakuu wako, wake zako na masuria wako mlivitumia kwa kunywea mvinyo. Ukaisifu miungu ya fedha na dhahabu, ya shaba, chuma, miti na mawe, miungu ambayo haiwezi kuona, au kusikia wala kufahamu. Lakini hukumheshimu Mungu ambaye anaushikilia uhai wako na njia zako zote mkononi mwake.
But hast lift thy selfe vp against the Lord of heauen, and they haue brought the vessels of his House before thee, and thou and thy princes, thy wiues and thy concubines haue drunke wine in them, and thou hast praysed the gods of siluer and golde, of brasse, yron, wood and stone, which neither see, neither heare, nor vnderstand: and the God in whose hand thy breath is and all thy wayes, him hast thou not glorified.
24 Kwa hiyo ameutuma mkono ule ulioandika maneno.
Then was the palme of the hand sent from him, and hath written this writing.
25 “Haya ndiyo maneno yaliyoandikwa: mene, mene, tekeli na peresi
And this is the writing that he hath written, MENE, MENE, TEKEL UPHARSIN.
26 “Hii ndiyo maana ya maneno haya: “Mene: Mungu amezihesabu siku za utawala wako na kuukomesha.
This is the interpretation of the thing, MENE, God hath nombred thy kingdome, and hath finished it.
27 Tekeli: Wewe umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua.
TEKEL, thou art wayed in the balance, and art found too light.
28 Peresi: Ufalme wako umegawanywa na kupewa Wamedi na Waajemi.”
PERES, thy kingdome is deuided, and giuen to the Medes and Persians.
29 Ndipo kwa amri ya Belshaza, Danieli akavikwa nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni, tena akatangazwa kuwa mtawala wa tatu katika ufalme.
Then at the commandement of Belshazzar they clothed Daniel with purple, and put a chaine of golde about his necke, and made a proclamation concerning him that he should be the third ruler in the kingdome.
30 Usiku ule ule, Belshaza mfalme wa Wakaldayo akauawa,
The same night was Belshazzar the King of the Caldeans slaine.
31 naye Dario Mmedi akashika ufalme akiwa na miaka sitini na miwili.
And Darius of the Medes tooke the kingdome, being threescore and two yeere olde.