< Danieli 4 >

1 Mfalme Nebukadneza, Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote: Mafanikio yawe kwenu sana!
Nebuchadnezzar the king to all people, nations, and languages that dwell upon the whole earth. Peace be multiplied to you!
2 Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.
I have thought it good to show the signs and wonders which the Most High God hath wrought toward me.
3 Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.
How great are his signs, and how mighty are his wonders! His kingdom is an everlasting kingdom, and his dominion endureth from generation to generation.
4 Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa.
I, Nebuchadnezzar, was at ease in my house, and flourishing in my palace.
5 Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha.
There I saw a dream which made me afraid, and the thoughts upon my bed and the visions of my head troubled me.
6 Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu.
Therefore made I a decree to bring in all the wise men of Babylon before me; that they might make known to me the interpretation of the dream.
7 Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria.
Then came in the scribes, the magicians, the Chaldaeans, and the astrologers; and I told the dream before them; but they did not make known to me its interpretation.
8 Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)
But at the last Daniel came in before me, whose name is Belteshazzar, according to the name of my god, and in whom is the spirit of the holy gods, and I told him the dream.
9 Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie.
O Belteshazzar, chief of the scribes, since I know that the spirit of the holy gods is in thee, and no secret is too hard for thee, tell me the visions of my dream which I have seen, and the interpretation thereof.
10 Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana.
The visions of my head were these. I saw, and behold a tree in the midst, whose height was very great.
11 Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia.
The tree was large and strong, and its height reached to heaven, and it might be seen to the end of the whole earth.
12 Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.
The leaves thereof were fair, and the fruit abundant, and in it was food for all. The beasts of the field had shadow under it, and the birds of heaven dwelt in the boughs thereof, and all flesh was fed of it.
13 “Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.
I saw, in the visions of my head upon my bed, and behold, a watcher, even a holy one, came down from heaven;
14 Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake.
he cried aloud, and spake thus: Hew down the tree, and cut off its branches; shake off its leaves, and scatter its fruit; let the beasts go away from under it, and the birds from its branches.
15 Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni. “‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia.
Yet leave the stump of its roots in the earth, in bands of iron and brass, in the tender grass of the field; and he shall be wet with the dew of heaven, and his portion shall be with the beasts in the grass of the field.
16 Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.
His heart shall be changed, and be no more that of a man, and a beast's heart shall be given him, and seven times shall pass over him.
17 “‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’
By a decision of the watchers is the decree, and by a command of the holy ones is the sentence; to the intent that the living may know that the Most High ruleth in the kingdoms of men, and giveth them to whomsoever he will, and setteth up over them the lowest of men.
18 “Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”
This dream I, King Nebuchadnezzar, saw, and do thou, O Belteshazzar, declare the interpretation thereof, forasmuch as all the wise men of my kingdom are not able to make known to me the interpretation; but thou art able, for the spirit of the holy gods is in thee.
19 Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.” Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako!
Then Daniel, who was called Belteshazzar, was amazed for one hour, and his thoughts troubled him. The king spake and said, Belteshazzar, let not the dream or the interpretation thereof trouble thee. Belteshazzar answered and said, My lord, the dream be to them that hate thee, and the signification of it to thine enemies!
20 Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote,
The tree which thou sawest, which was large and strong, whose height reached to heaven, and which might be seen by all the earth,
21 ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani.
whose leaves were fair, and whose fruit abundant, and in which was food for all, under which all the beasts of the field dwelt, and upon whoso branches the birds of heaven had their lodging, —
22 Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.
it is thou, O king, who art become great and strong; for thy greatness is immense, and reacheth to heaven, and thy dominion to the end of the earth.
23 “Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’
And whereas the king saw a watcher, even a holy one, coming down from heaven, and saying, Hew the tree down and destroy it, yet leave the stump of its roots in the earth, in bands of iron and brass, in the tender grass of the field, and he shall be wet with the dew of heaven, and his portion shall be with the beasts of the field, till seven times pass over him;
24 “Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme:
this is the interpretation, O king, and this is the decree of the Most High, which is come upon my lord, the king;
25 Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.
they shall drive thee from men, and thy dwelling shall be with the beasts of the field, and they shall let thee eat grass as oxen, and be wet with the dew of heaven, and seven times shall pass over thee, till thou know that the Most High ruleth in the kingdoms of men, and giveth them to whomsoever he will.
26 Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo.
And whereas it was commanded to leave the stump of the roots of the tree, thy kingdom shall be sure to thee after thou shalt have acknowledged that Heaven ruleth.
27 Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”
Wherefore, O king, let my counsel be acceptable to thee, and break off thy sins by righteousness, and thy iniquities by showing mercy to the poor; if it may be a lengthening out of thy tranquility.
28 Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.
All this came upon King Nebuchadnezzar.
29 Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli,
At the end of twelve months, he was walking in the palace of the kingdom of Babylon;
30 alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
and the king spake and said, Is not this the great Babylon which I have built for the seat of the kingdom by the might of my power and for the honor of my majesty?
31 Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako.
While the word was in the king's mouth, there fell a voice from heaven: “To thee it is said, O Nebuchadnezzar! the kingdom is departed from thee.
32 Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”
And they shall drive thee from men, and thy dwelling shall be with the beasts of the field; they shall make thee eat grass as oxen, and seven times shall pass over thee, until thou know that the Most High ruleth in the kingdoms of men, and giveth them to whomsoever he will.”
33 Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.
The same hour was the word fulfilled against Nebuchadnezzar, and he was driven from men, and did eat grass as oxen, and his body was wet with the dew of heaven, till his hairs were grown like eagles' feathers, and his nails like birds' claws.
34 Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele. Utawala wake ni utawala wa milele; ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.
But at the end of the days, I Nebuchadnezzar lifted up my eyes to heaven, and my understanding returned to me, and I blessed the Most High, and I praised and honored Him that liveth forever, whose dominion is an everlasting dominion, and whose kingdom endureth from generation to generation.
35 Mataifa yote ya dunia yanahesabiwa kuwa si kitu. Hufanya kama atakavyo kwa majeshi ya mbinguni, na kwa mataifa ya dunia. Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”
And all the inhabitants of the earth are counted as nothing; and he doeth according to his will in the army of heaven, and among the inhabitants of the earth; and none can stay his hand, or say to him, What doest thou?
36 Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni.
At the same time my reason returned to me, and also the glory of my kingdom, my honor, and my splendor returned to me; and my counsellors and my lords sought me; and I was established in my kingdom, and I received yet greater majesty.
37 Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.
Now I Nebuchadnezzar praise and extol and honor the King of heaven; all whose works are truth and his ways justice; and those that walk in pride he is able to abase.

< Danieli 4 >