< Danieli 4 >

1 Mfalme Nebukadneza, Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote: Mafanikio yawe kwenu sana!
Цар Навуходоносор към всичките племена, народи и езици, които живеят по цял свят - Мир да ви се умножи!
2 Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.
Видя ми се за добре да оповестя знаменията и чудесата, които ми направи всевишният Бог.
3 Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.
Колко са велики Неговите знамения! И колко могъщи са чудесата му! Неговото царство е вечно царство, и Неговото владичество из род в род.
4 Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa.
Аз Навуходоносор, като бях спокоен у дома си и благополучен в палата си,
5 Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha.
видях сън, който ме уплаши; и размишленията ми на леглото ми и виденията на главата ми ме смутиха.
6 Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu.
За това, издадох указ да се въведат пред мене всичките вавилонски мъдреци, за да ми явят значението на съня.
7 Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria.
Тогава влязоха врачовете, вражарите, халдейците, и астролозите, и аз разказах съня си пред тях; но не можаха да ми явят значението му.
8 Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)
А най- после дойде пред мене Даниил, чието име бе Валтасасар по името на моя бог, и в когото е духът на светите богове; и аз разказах съня пред него, като рекох:
9 Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie.
Валтасасаре, началниче на врачовете, понеже узнах, че духът на светите богове е в тебе, и че никаква тайна не е мъчна за тебе, обясни ми виденията на съня, който видях, и кажи ми значението му.
10 Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana.
Ето какви бяха виденията на главата ми и на леглото ми: Гледах, и ето дърво всред света, на което височината бе голяма.
11 Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia.
Това дърво стана голямо и яко, височината му стигаше до небето, и то се виждаше до краищата на целия свят.
12 Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.
Листата му бяха хубави, плодът му изобилен, и в него имаше храна за всички; под сянката му почиваха полските животни, и на клоновете му обитаваха небесните птици, и от него се хранеше всяка твар.
13 “Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.
Видях във виденията на главата си на леглото си, и ето, един свет страж слезе от небето,
14 Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake.
и извика със силен глас, казвайки така: Отсечете дървото и изсечете клоновете му; отърсете листата му и разпръснете плода му; нека бягат животните изпод него, и птиците от клоновете му;
15 Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni. “‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia.
обаче оставете в земята пъна с корените му всред полската трева, и то с железен и меден обръч наоколо, и нека се мокри с небесна роса, и участта му нека бъде с животните в тревата на земята;
16 Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.
нека се измени човешкото му сърце, и нека му се даде животинско сърце; и така нека минат над него седем времена.
17 “‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’
Тая присъда е по заповед от стражите, и делото на думата на светите, за да знаят живите, че Всевишният владее над царството на човеците, дава го комуто ще, и поставя над него най-нищожният измежду човеците.
18 “Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”
Тоя сън видях аз цар Навуходоносор, и ти, Валтасасаре, кажи значението му; защото ни един от мъдреците на царството ми не може да ми яви значението; а ти можеш, защото духът на светите богове е в тебе.
19 Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.” Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako!
Тогава Даниил, чието име бе Валтасасар, остана смаян за малко, и размишленията му го смущаваха. Царят продумайки, рече: Валтасасаре, да те не смущава сънят или значението му. Валтасасар рече в отговор: Господарю мой, сънят нека бъде върху ония, които те мразят, и това, което означава, върху неприятелите ти!
20 Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote,
Дървото, което си видял, че станало голямо и яко, чиято височина стигала до небето, и което се виждало от целия свят,
21 ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani.
чиито листа били хубави и плодът му изобилен, дори достатъчна храна за всички, под което живеели полските животни, и по клоновете на което се подсланяли небесните птици,
22 Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.
това дърво си ти, царю, който си станал голям и як; защото величието ти нарасна и стигна до небето, и владичеството ти до края на света.
23 “Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’
А дето царят е видял един свет страж да слиза от небето и да казва: Отсечете дървото и го съборете, но оставете в земята, в полската трева, пъна с корените му, и то със железен и меден обръч наоколо, и нека се мокри от небесната роса, и нека бъде участта му с полските животни, докато така минат над него седем времена,
24 “Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme:
ето значението му, царю: Решението на Всевишния, което постигна господаря ми царя, е
25 Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.
да бъдеш изгонен измежду човеците, жилището ти да бъде с полските животни, да ядеш трева като говедата, и да те мокри небесната роса, и да минат над тебе седем времена, догдето познаеш, че Всевишният владее в царството на човеците, и го дава комуто ще.
26 Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo.
А дето се заповядало да оставят пъна с корените на дървото, значи, че царството ти ще бъде обезпечено щом признаеш, че небесата владеят.
27 Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”
Затова, царю, нека ти бъде угоден моят съвет да напуснеш греховете си чрез вършене на правда, и беззаконията си чрез правене благодеяния на бедните, негли се продължи благоденствието ти.(Или: се прости престъплението ти)
28 Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.
Всичко това постигна цар Навуходоносора.
29 Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli,
В края на дванадесет месеца, като ходеше по царския палат у Вавилон,
30 alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
царят проговори, казвайки: Не е ли велик тоя Вавилон, който аз съградих с мощната си сила за царското жилище и за славата на величието си!
31 Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako.
Думата бе още в устата на царя, и глас дойде от небесата, който рече: На тебе се известява, царю Навуходоносоре, че царството премина от тебе;
32 Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”
и ще бъдеш изгонен измежду човеците, между полските животни ще бъде жилището ти, и ще те хранят с трева като говедата; и седем времена ще минат над тебе, додето признаеш, че Всевишният владее над царството на човеците, и го дава комуто ще.
33 Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.
В същия час това нещо се изпълни над Навуходоносора; той бе изгонен измежду човеците, ядеше трева като говедата, и тялото му се мокреше от небесната роса, додето космите му пораснаха като пера на орли, и ноктите му като на птици.
34 Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele. Utawala wake ni utawala wa milele; ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.
А в края на тия дни аз Навуходоносор повдигнах очите си към небесата; и разумът ми се възвърна като благослових Всевишния и похвалих и прославих Оногова, който живее до века, понеже владичеството Му е вечно владичество, и царството Му из род в род;
35 Mataifa yote ya dunia yanahesabiwa kuwa si kitu. Hufanya kama atakavyo kwa majeshi ya mbinguni, na kwa mataifa ya dunia. Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”
пред Него всичките земни жители се считат като нищо; по волята Си Той действа между небесната войска и между земните жители; и никой не може да спре ръката Му, или да Му каже - Що правиш Ти?
36 Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni.
И в същото време, когато разумът ми се възвърна, възвърнаха ми се, за славата на царството ми, и величието и светлостта ми; защото съветниците ми и големците ми ме търсеха, закрепих се на царството си, и ми се притури превъзходно величие.
37 Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.
Сега аз Навуходоносор хваля, превъзнасям, и славя небесния Цар; защото всичко, що върши е с вярност, и пътищата му са справедливи; а Той може да смири ония, които ходят горделиво.

< Danieli 4 >