< Danieli 3 >

1 Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini, na upana wa dhiraa sita, akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli.
La dix-huitième année de son règne, Nabuchodonosor fit faire une statue d'or, haute de soixante coudées, sur six d'épaisseur, et il l'érigea en la plaine de Déira, dans la province de Babylone.
2 Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
Et il convoqua les grands, les généraux et les gouverneurs, les rois, les tyrans et les dignitaires, et tous les chefs des provinces pour venir à l'inauguration de la statue.
3 Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.
Et les gouverneurs, les grands, les généraux, les rois, les principaux tyrans, les dignitaires et les chefs des provinces se rassemblèrent pour l'inauguration de la statue qu'avait érigée le roi Nabuchodonosor, et ils se placèrent debout devant la statue.
4 Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya:
Et le héraut proclama à haute voix: Ceci vous et prescrit, peuples, tribus, hommes de toutes langues:
5 Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha.
À l'instant où vous entendrez le son de la trompette et de la flûte, de la cithare, de la harpe et du psaltérion, et des instruments de toute sorte, tombez la face contre terre, et adorez la statue d'or que le roi Nabuchodonosor a érigée.
6 Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”
Et celui qui n'adorera pas, en tombant à genoux, sera jeté aussitôt dans la fournaise ardente où le feu est allumé.
7 Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
Or ceci advint: dès que les peuples entendirent le son de la trompette et de la flûte, de la cithare, de la harpe et du psaltérion, et des instruments de toute sorte, les peuples tombèrent la face contre terre, et ils adorèrent la statue d'or que le roi Nabuchodonosor avait érigée.
8 Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi.
Alors vinrent des hommes de la Chaldée et ils accusèrent les Juifs
9 Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele!
Devant le roi, disant: Ô roi, vis à jamais!
10 Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu,
Ô toi, tu as fait une ordonnance, disant: Que tout homme qui entendra le son de la trompette et de la flûte, de la cithare, de la harpe et du psaltérion, et des instruments de toute sorte,
11 na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.
Et qui ne tombera pas la face contre terre pour adorer la statue d'or, soit jeté dans la fournaise ardente où le feu est allumé.
12 Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
Or il y a des hommes, des Juifs, que tu as chargés de toutes les affaires de la province de Babylone, Sidrach, Misach et Abdénago, qui n'ont point obéi à ton ordre, ô roi; tes dieux, ils ne les honorent pas; et la statue d'or que tu as érigée, ils ne l'adorent point.
13 Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme,
Alors Nabuchodonosor, plein de colère et de fureur, commanda de lui amener Sidrach, Misach et Abdénago, et on les amena en présence du roi.
14 naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
Et Nabuchodonosor prit la parole, et leur dit: Est-il vrai, Sidrach, Misach et Abdénago, que vous ne servez point mes dieux, et que vous n'adorez pas la statue d'or que j'ai élevée?
15 Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”
Maintenant donc, si vous y êtes disposés, aussitôt que vous entendrez le son de la trompette, de la flûte et de la cithare, de la harpe et du psaltérion, et le concert des instruments de toute sorte, tombez la face contre terre, et adorez la statue d'or que j'ai faite. Que si vous ne l'adorez pas, à l'instant même vous serez jetés dans la fournaise ardente, où le feu est allumé; et quel est le Dieu qui vous tirera de mes mains?
16 Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili.
Sidrach, Misach et Abdénago répondirent au roi Nabuchodonosor, disant: Il n'est pas nécessaire que nous te fassions une réponse à cette question.
17 Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme.
Car notre Dieu qui est au ciel, le Dieu que nous servons, peut nous tirer de la fournaise ardente et nous sauver, ô roi, d'entre tes mains.
18 Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
Et quand même il ne le ferait pas, sache, ô roi, que tes dieux nous ne les servons pas, et que la statue d'or que tu as élevée, nous ne l'adorons point.
19 Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake
Alors Nabuchodonosor, plein de colère, changea de visage envers Sidrach, Misach et Abdénago, et il ordonna de rendre sept fois plus ardent le feu de la fournaise, jusqu'à ce qu'enfin il ne fût plus qu'un brasier.
20 na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto.
Et il ordonna à des hommes robustes de mettre des entraves à Sidrach, Misach et Abdénago, puis de les jeter dans la fournaise ardente.
21 Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine.
Aussitôt ces jeunes gens furent enchaînés sans qu'on leur ôtât ni leurs hauts-de-chausses, ni leurs tiares, ni leurs chaussures, et ils furent jetés au milieu des flammes de la fournaise;
22 Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego.
Car la parole du roi était pressante, et la fournaise était plus ardente que jamais.
23 Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.
Et Sidrach, Misach et Abdénago tombèrent tous trois enchaînés au milieu des flammes de la fournaise embrasée.
24 Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?” Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”
Et Nabuchodonosor les entendit chanter des hymnes, et il fut frappé d'étonnement, et il se leva précipitamment, et il dit aux grands qui l'entouraient: N'avons-nous pas jeté au milieu du feu trois hommes enchaînés? et ils dirent au roi: Oui, seigneur.
25 Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”
Et le roi dit: Et moi, je vois quatre hommes sans liens, se promenant au milieu des flammes, et la destruction n'est pas avec eux, et l'aspect du quatrième ressemble à un fils de Dieu.
26 Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto.
Alors Nabuchodonosor s'approcha de la porte de la fournaise ardente, et il dit: Sidrach, Misach, Abdénago, serviteurs du Dieu tout-puissant, sortez et venez! Et Sidrach, Misach et Abdénago sortirent du milieu des flammes.
27 Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.
Et les satrapes, et les généraux, et les gouverneurs et les lieutenants du roi se rassemblèrent, et ils virent ces hommes sur qui le feu n'avait eu nulle puissance en leur corps; pas un cheveu de leur tête n'était brûlé; leur vêtement n'était point altéré, et nulle odeur de feu n'était en eux.
28 Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao.
Et le roi Nabuchodonosor prit la parole, et il dit: Béni soit le Dieu de Sidrach, de Misach et d'Abdénago, qui a envoyé son ange, et délivré ses serviteurs, parce qu'ils avaient eu confiance eu lui; ils désobéirent à la parole du roi, et ils abandonnèrent leurs corps à la flamme, pour ne point adorer ni servir d'autre dieu que leur Dieu.
29 Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”
Et moi je proclame ce décret: Tout peuple, toute tribu, tout homme, de quelque langue qu'il soit, qui profèrera un blasphème contre le Dieu de Sidrach, de Misach et d'Abdénago, sera exterminé; ses maisons seront livrées au pillage; parce qu'il n'est point d'autre Dieu qui puisse sauver ainsi.
30 Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.
Ensuite le roi rétablit Sidrach, Misach et Abdénago à la tête de la province de Babylone; et il les éleva en honneur, et les jugea dignes de commander à tous les Juifs qui étaient dans son royaume.

< Danieli 3 >