< Danieli 3 >
1 Mfalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya dhahabu, yenye kimo cha dhiraa sitini, na upana wa dhiraa sita, akaisimamisha kwenye tambarare ya Dura katika jimbo la nchi ya Babeli.
Nabugodonosor, the kyng, made a goldun ymage, in the heiythe of sixti cubitis, and in the breede of sixe cubitis; and he settide it in the feeld of Duram, of the prouynce of Babiloyne.
2 Kisha mfalme akaita wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wote wa jimbo kuja kuizindua sanamu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
Therfor Nabugodonosor sente to gadere togidere the wise men, magistratis, and iugis, and duykis, and tirauntis, and prefectis, and alle princes of cuntreis, that thei schulden come togidere to the halewyng of the ymage, which the kyng Nabugodonosor hadde reisid.
3 Basi wakuu, wasimamizi, watawala, washauri, watunza hazina, waamuzi, mahakimu na maafisa wengine wa jimbo walikusanyika ili kuizindua sanamu ile Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha, nao wakasimama mbele ya hiyo sanamu.
Thanne the wise men, magistratis, and iugis, and duykis, and tirauntis, and beste men, that weren set in poweris, and alle the princes of cuntreis, weren gaderid togidere, that thei schulden come togidere to the halewyng of the ymage, which the kyng Nabugodonosor hadde reisid. Forsothe thei stoden in the siyt of the ymage, which Nabugodonosor hadde set; and a bedele criede myytili,
4 Ndipo mpiga mbiu akatangaza kwa sauti kubwa, “Enyi watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha, hili ndilo mnaloamriwa kulifanya:
It is seid to you, puplis, kynredis, and langagis;
5 Mara mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za sauti za ala za uimbaji, lazima mwanguke chini na kuabudu sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza ameisimamisha.
in the our in which ye heren the soun of trumpe, and of pipe, and of harpe, of sambuke, of sawtre, and of symphonye, and of al kynde of musikis, falle ye doun, and worschipe the goldun ymage, which the kyng Nabugodonosor made.
6 Mtu yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu sanamu hiyo, atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.”
Sotheli if ony man fallith not doun, and worschipith not, in the same our he schal be sent in to the furneis of fier brennynge.
7 Kwa hiyo, mara waliposikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda na aina zote za ala za uimbaji, watu wa kabila zote, mataifa na watu wa kila lugha wakaanguka chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza alikuwa ameisimamisha.
Therfor aftir these thingis, anoon as alle puplis herden the sown of trumpe, of pipe, and of harpe, of sambuke, and of sawtre, of symphonye, and of al kynde of musikis, alle puplis, lynagis, and langagis fellen doun, and worschipiden the golden ymage, which the kyng Nabugodonosor hadde maad.
8 Wakati huo baadhi ya Wakaldayo walijitokeza na kuwashtaki Wayahudi.
And anoon in that tyme men of Caldee neiyiden, and accusiden the Jewis,
9 Wakamwambia Mfalme Nebukadneza, “Ee mfalme, uishi milele!
and seiden to the kyng Nabugodonosor, Kyng, lyue thou with outen ende.
10 Ee mfalme, umetoa amri kwamba kila mmoja atakayesikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, kinanda, zumari na aina zote za ala za uimbaji lazima aanguke chini na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu,
Thou, kyng, hast set a decree, that ech man that herith the sown of trumpe, of pipe, and of harpe, of sambuke, and of sawtree, and of symphonye, and of al kynde of musikis, bowe doun hym silf, and worschipe the goldun ymage; forsothe if ony man fallith not doun,
11 na kwamba yeyote ambaye hataanguka chini na kuiabudu atatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto.
and worschipith not, be he sent in to the furneis of fier brennynge.
12 Lakini wako baadhi ya Wayahudi ambao umewaweka juu ya mambo ya jimbo la Babeli: yaani, Shadraki, Meshaki na Abednego, ambao hawakujali wewe, ee mfalme. Hawaitumikii miungu yako wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
Therfor men Jewis ben, Sidrac, Mysaac, and Abdenago, whiche thou hast ordeynede on the werkis of the cuntrei of Babiloyne. Thou kyng, these men han dispisid thi decree; thei onouren not thi goddis, and thei worshipen not the goldun ymage, which thou reisidist.
13 Mfalme Nebukadneza, akiwa amekasirika na mwenye ghadhabu kali, akawaita Shadraki, Meshaki na Abednego. Hivyo watu hawa wakaletwa mbele ya mfalme,
Thanne Nabugodonosor comaundide, in woodnesse and in wraththe, that Sidrac, Mysaac, and Abdenago schulden be brouyt; whiche weren brouyt anoon in the siyt of the kyng.
14 naye Nebukadneza akawauliza, “Je, ni kweli kwamba ninyi Shadraki, Meshaki na Abednego hamuitumikii miungu yangu wala kuiabudu sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
And the kyng Nabugodonosor pronounside, and seide to hem, Whether verili Sidrac, Mysaac, and Abdenago, ye onouren not my goddis, and worschipen not the golden ymage, which Y made?
15 Basi wakati mtakaposikia sauti ya baragumu, filimbi, marimba, zeze, kinubi, zumari na aina zote za ala za uimbaji, kama mtakuwa tayari kusujudu na kuiabudu hiyo sanamu niliyoitengeneza, vyema sana. Lakini kama hamtaiabudu, mtatupwa saa iyo hiyo ndani ya tanuru iwakayo moto. Naye ni mungu yupi atakayeweza kuwaokoa ninyi, kutoka mkono wangu?”
Now therfor be ye redi, in what euer our ye heren the sown of trumpe, of pipe, of harpe, of sambuke, of sawtree, and of symphonye, and of al kynde of musikis, bowe ye doun you, and worschipe the ymage which Y made; that if ye worschipen not, in the same our ye schulen be sent in to the furneis of fier brennynge; and who is God, that schal delyuere you fro myn hond?
16 Shadraki, Meshaki na Abednego wakamjibu mfalme, “Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea mbele zako kuhusu jambo hili.
Sidrac, Misaac, and Abdenago answeriden, and seiden to the king Nabugodonosor, It nedith not, that we answere of this thing to thee.
17 Ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, ee mfalme.
For whi oure God, whom we worschipen, mai rauysche vs fro the chymenei of fier brennynge, and mai delyuere fro thin hondis, thou kyng.
18 Lakini hata ikiwa hatatuokoa, ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.”
That if he nyle, be it knowun to thee, thou kyng, that we onouren not thi goddis, and we worschipen not the goldun ymage, which thou hast reisid.
19 Ndipo Nebukadneza akawa na ghadhabu kali sana kwa Shadraki, Meshaki na Abednego, nayo nia yake ikabadilika kwao. Akaagiza tanuru ichochewe moto mara saba kuliko kawaida yake
Thanne Nabugodonosor was fillid of woodnesse, and the biholdyng of his face was chaungid on Sidrac, Misaac, and Abdenago. And he comaundide, that the furneis schulde be maad hattere seuenfold, than it was wont to be maad hoot.
20 na kuwaamuru baadhi ya askari wake wenye nguvu zaidi katika jeshi lake kuwafunga Shadraki, Meshaki na Abednego na kuwatupa ndani ya tanuru iwakayo moto.
And he comaundide to the strongeste men of his oost, that thei schulden bynde the feet of Sidrac, Mysaac, and Abdenago, and sende hem in to the furneis of fier brennynge.
21 Hivyo watu hawa, walifungwa na kutupwa ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamevaa majoho yao, suruali, vilemba na nguo zao nyingine.
And anoon tho men weren boundun, with brechis, and cappis, and schoon, and clothis, and weren sent in to the myddis of the furneis of fier brennynge;
22 Amri ya mfalme ilikuwa ya haraka sana na tanuru ilikuwa na moto mkali kiasi kwamba miali ya moto iliwaua wale askari waliowapeleka Shadraki, Meshaki na Abednego.
for whi comaundement of the kyng constreinede. Forsothe the furneis was maad ful hoot; certis the flawme of the fier killid tho men, that hadden sent Sidrac, Misaac, and Abdenago in to the furneis.
23 Watu hawa watatu walianguka ndani ya tanuru iwakayo moto wakiwa wamefungwa kwa uthabiti sana.
Sotheli these thre men, Sidrac, Misaac, and Abdenago, fellen doun boundun in the mydis of the chymenei of fier brennynge.
24 Ndipo Mfalme Nebukadneza akashangaa, akainuka kwa haraka na kuwauliza washauri wake, “Je, hawakuwa watu watatu ambao tuliwafunga na kuwatupa ndani ya moto?” Washauri wakajibu, “Hakika, ee mfalme.”
Thanne kyng Nabugodonosor was astonyed, and roos hastily, and seide to hise beste men, Whether we senten not thre men feterid in to the myddis of the fier? Whiche answeriden the kyng, and seiden, Verili, kyng.
25 Mfalme akasema, “Tazama! Naona watu wanne wakitembeatembea ndani ya moto, hawajafungwa wala kudhurika, naye mtu yule wa nne anaonekana kama mwana wa miungu.”
The kyng answeride, and seide, Lo! Y se foure men vnboundun, and goynge in the myddis of the fier, and no thing of corrupcioun is in hem; and the licnesse of the fourthe is lijk the sone of God.
26 Ndipo Nebukadneza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iwakayo moto na kupaza sauti, “Shadraki, Meshaki na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye Juu Sana, tokeni! Njooni hapa!” Ndipo Shadraki, Meshaki na Abednego wakatoka ndani ya moto.
Thanne the kyng Nabugodonosor neiyide to the dore of the furneis of fier brennynge, and seide, Sidrac, Mysaac, and Abdenago, the seruauntis of hiy God lyuynge, go ye out, and come ye. And anoon Sidrac, Mysaac, and Abdenago, yeden out of the myddis of the fier.
27 Nao maliwali, wasimamizi, watawala na washauri wa mfalme wakakusanyika kuwazunguka. Waliona kwamba moto haukudhuru miili yao, wala unywele wa vichwa vyao haukuungua, majoho yao hayakuungua, wala hapakuwepo na harufu ya moto kwenye miili yao.
And the wise men, and magistratis, and iugis, and miyti men of the kyng, weren gaderid togidere, and bihelden tho men, for the fier hadde had no thing of power in the bodies of hem, and an heer of her heed was not brent; also the breechis of hem weren not chaungid, and the odour of fier hadde not passid bi hem.
28 Ndipo Nebukadneza akasema, “Ahimidiwe Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, ambaye amemtuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake. Walimtumaini na kukaidi amri ya mfalme, nao wakawa tayari kufa kuliko kutumikia au kuabudu mungu mwingine yeyote isipokuwa Mungu wao.
And Nabugodonosor brac out, and seide, Blessid be the God of hem, that is, of Sidrac, Mysaac, and Abdenago, that sente his aungel, and delyueride hise seruauntis, that bileuyden in to hym, and chaungiden the word of the kyng, and yauen her bodies, that thei schulden not serue, and that thei schulden not worschipe ony god, outakun her God aloone.
29 Kwa hiyo ninaamuru kwamba watu wa taifa lolote au lugha yoyote watakaosema kitu chochote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego wakatwe vipande vipande na nyumba zao zifanywe kuwa malundo ya kokoto, kwa maana hakuna mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.”
Therfor this decree is set of me, that ech puple, and langagis, and lynagis, who euer spekith blasfemye ayen God of Sidrac, and of Mysaac, and of Abdenago, perische, and his hous be distried; for noon other is God, that mai saue so.
30 Kisha mfalme akawapandisha vyeo Shadraki, Meshaki na Abednego katika jimbo la Babeli.
Thanne the kyng auaunside Sidrac, Mysaac, and Abdenago, in the prouynce of Babiloyne; and sente in to al the lond a pistle, conteynynge these wordis.