< Danieli 2 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wake, Nebukadneza aliota ndoto. Mawazo yake yakasumbuka na hakuweza kulala.
Et la seconde année du règne de Nébucadnézar, Nébucadnézar eut des songes. Et son esprit était agité, et il avait perdu le sommeil.
2 Hivyo mfalme akawaita waganga, wasihiri, wachawi na wanajimu ili wamwambie ndoto yake aliyokuwa ameota. Walipoingia ndani na kusimama mbele ya mfalme,
Et le roi ordonna de convoquer les devins et les enchanteurs, et les mages et les Chaldéens pour qu'ils exposassent au roi ses songes; et ils vinrent et se présentèrent devant le roi.
3 akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”
Et le roi leur dit: J'ai eu un songe, et mon esprit s'agite pour avoir la connaissance de ce songe.
4 Ndipo wanajimu wakamjibu mfalme kwa lugha ya Kiaramu, “Ee mfalme, uishi milele! Waambie watumishi wako hiyo ndoto, nasi tutaifasiri.”
Et les Chaldéens dirent au roi en langue araméenne: O roi, puisses-tu vivre éternellement! dis le songe à tes serviteurs, et nous t'en découvrirons le sens.
5 Mfalme akawajibu wanajimu, “Nimeamua hivi kwa uthabiti: Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu ilikuwa ipi na kuifasiri, mtakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vifusi.
Le roi répondit et dit aux Chaldéens: La parole est émanée de moi! Si vous ne me faites connaître le songe et sa signification, vous serez coupés par morceaux, et vos maisons seront changées en tas de fumier.
6 Lakini mkiniambia ndoto yangu na kuielezea, mtapokea kwangu zawadi, tuzo na heshima kubwa. Basi niambieni ndoto yangu na mnifasirie.”
Mais si vous m'exposez le songe et sa signification, vous recevrez de moi des dons et des largesses, et de grands honneurs; indiquez-moi donc quel est le songe, et quel en est le sens!
7 Wakajibu kwa mara nyingine, “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto yake, nasi tutaifasiri.”
Ils répondirent de nouveau, et dirent: Que le roi dise le songe à ses serviteurs, et nous en découvrirons le sens.
8 Ndipo mfalme akajibu, “Nina hakika kuwa mnajaribu kupata muda zaidi, kwa sababu mnatambua kuwa nimeamua hivi kwa uthabiti:
Le roi répondit et dit: Je comprends, à en être certain, que c'est du temps que vous voulez gagner, par la raison que vous voyez que la parole est émanée de moi.
9 Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu, ipo adhabu moja tu kwenu. Mmefanya shauri kuniambia habari za kunipotosha na mambo maovu, mkitumaini kwamba hali itabadilika. Hivyo basi, niambieni hiyo ndoto, nami nitajua kuwa mwaweza kunifasiria.”
Si donc vous ne me faites pas connaître le songe, c'est là votre unique but, et vous vous êtes entendus pour me débiter des mensonges et des faussetés, jusqu'à ce que le moment ait changé: ainsi, racontez-moi le songe, et je saurai que vous êtes capables de m'en donner l'explication.
10 Wanajimu wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu duniani ambaye anaweza kufanya analotaka mfalme! Vilevile hakuna mfalme hata awe mkuu na mwenye uweza namna gani, aliyeuliza kitu kama hicho kwa mganga au kwa msihiri, wala kwa mnajimu yeyote.
Les Chaldéens répliquèrent devant le roi, et dirent: Sur la terre sèche il n'est personne qui soit en état d'exposer la chose énoncée par le roi: aussi, jamais roi, quelque grand et puissant qu'il fût, n'a exigé chose pareille d'aucun devin, enchanteur et Chaldéen.
11 Anachouliza mfalme ni kigumu mno. Hakuna yeyote awezaye kumfunulia mfalme isipokuwa miungu, nao hawaishi miongoni mwa wanadamu.”
La chose qu'exige le roi est trop difficile, et pour la découvrir au roi il n'y en a pas d'autre que les dieux qui n'habitent pas au milieu des mortels.
12 Jambo hili lilimkasirisha na kumghadhibisha mfalme mno hata kuagiza kuuawa kwa wenye hekima wote wa Babeli.
A cause de cela le roi se mit en colère, et fut fort courroucé, et il ordonna de faire périr tous les sages de Babel.
13 Hivyo amri ikatolewa ya kuwaua wenye hekima, nao watu wakatumwa kuwatafuta Danieli na rafiki zake ili wawaue.
Et l'édit fut promulgué, et les sages devaient être mis à mort; et l'on cherchait Daniel et ses compagnons pour les mettre à mort.
14 Wakati Arioko, mkuu wa askari wa walinzi wa mfalme, alikuwa amekwenda kuwaua watu wenye hekima wa Babeli, Danieli akazungumza naye kwa hekima na busara.
Alors Daniel fit une réponse sage et prudente à Arioch, chef des satellites du roi, qui était sorti pour mettre à mort les sages de Babel.
15 Akamuuliza huyo afisa wa mfalme, “Kwa nini mfalme ametoa amri kali hivyo?” Ndipo Arioko akamweleza Danieli jambo hilo.
Prenant la parole il dit à Arioch, général du roi: Pourquoi cet édit sévère de par le roi? Alors Arioch fit connaître à Daniel ce qui en était.
16 Aliposikia jambo hili, Danieli akamwendea mfalme, akamwomba ampe muda ili aweze kumfasiria ile ndoto.
Et Daniel entra, et pria le roi de lui accorder un délai et la permission de donner au roi l'explication.
17 Ndipo Danieli akarudi nyumbani kwake na kuwaeleza rafiki zake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo.
Puis Daniel se rendit dans sa maison, et informa Hananias, Misaël, et Azarias, ses compagnons, de l'état des choses:
18 Aliwasihi waombe rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusu siri hii, ili yeye na rafiki zake wasije wakauawa pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.
qu'il leur fallait implorer la miséricorde du Dieu du ciel au sujet de ce mystère, afin que Daniel et ses compagnons ne périssent pas avec les autres sages de Babel.
19 Wakati wa usiku lile fumbo lilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Ndipo Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni,
Après cela, dans une vision nocturne le mystère fut dévoilé à Daniel; puis Daniel bénit le Dieu du ciel.
20 na akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.
Daniel prit la parole et dit: Béni soit le nom de Dieu de l'éternité à l'éternité! car Il a, oui, Il a sagesse et puissance!
21 Yeye hubadili nyakati na majira; huwaweka wafalme na kuwaondoa. Huwapa hekima wenye hekima, na maarifa wenye ufahamu.
C'est lui qui opère les vicissitudes des temps et des époques, qui dépose des rois, et élève des rois, qui accorde la sagesse aux sages, et l'intelligence à ceux qui savent comprendre.
22 Hufunua siri na mambo yaliyofichika; anajua yale yaliyo gizani, nayo nuru hukaa kwake.
Il met à nu les profondeurs et les secrets, Il pénètre ce qui est ténébreux, et la lumière demeure auprès de lui.
23 Ninakushukuru na kukuhimidi, Ee Mungu wa baba zangu: Umenipa hekima na uwezo, umenijulisha kile tulichokuomba, umetujulisha ndoto ya mfalme.”
A toi, Dieu de mes pères, j'élève mes actions de grâces et mes louanges, parce que tu m'as accordé la sagesse et la force, et que tu m'as révélé ce que je te demandais; car tu nous as révélé la pensée du roi.
24 Ndipo Danieli akamwendea Arioko, ambaye mfalme alikuwa amemteua kuwaua wenye hekima wa Babeli, akamwambia, “Usiwaue wenye hekima wa Babeli. Nipeleke kwa mfalme, nami nitamfasiria ndoto yake.”
Ensuite de cela Daniel entra chez Arioch, à qui le roi avait donné l'office de faire périr les sages de Babel; il alla et lui parla ainsi: Ne fais point périr les sages de Babel! Introduis-moi auprès du roi, et j'exposerai au roi l'explication.
25 Arioko akampeleka Danieli kwa mfalme mara moja na kumwambia, “Nimempata mtu miongoni mwa watu wa uhamisho kutoka Yuda ambaye anaweza kumwambia mfalme maana ya ndoto yake.”
Alors Arioch en hâte introduisit Daniel auprès du roi, auquel il parla en ces termes: J'ai trouvé un homme parmi les captifs de Juda, qui présentera au roi l'explication.
26 Mfalme akamuuliza Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza), “Je, unaweza kuniambia nilichoona katika ndoto yangu na kuifasiri?”
Le roi répondit et dit à Daniel dont le nom était Beltsazar: Es-tu à même de me dire quel songe j'ai eu, et quel en est le sens?
27 Danieli akajibu, “Hakuna mwenye hekima, msihiri, mganga au mwaguzi anayeweza kumweleza mfalme siri aliyouliza,
Daniel répondit en présence du roi et dit: « Le mystère qui est l'objet de la demande du roi, ni sages, ni enchanteurs, ni devins, ni mages ne sont capables de le dévoiler au roi.
28 lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri. Amemwonyesha Mfalme Nebukadneza kitakachotokea siku zijazo. Ndoto yako na maono yaliyopita mawazoni mwako ulipokuwa umelala kitandani mwako ni haya:
Mais il est dans le ciel un Dieu qui dévoile les mystères, et Il révèle au roi Nébucadnézar ce qui aura lieu dans la suite des temps. Voici le songe et la vision qui se sont présentés à ton esprit, pendant que tu étais couché.
29 “Ee mfalme, ulipokuwa umelala kitandani, yalikujia mawazo kuhusu mambo yatakayotokea baadaye, naye mfunuaji wa siri akakuonyesha ni kitu gani kitakachotokea.
O roi, tes pensées se sont élevées en toi pendant que tu étais couché, et se sont portées sur ce qui arrivera après ce temps-ci; et Celui qui dévoile les mystères, t'a révélé l'avenir.
30 Kwangu mimi, nimefunuliwa siri hii, si kwa sababu nina hekima kubwa kuliko watu wengine wanaoishi, bali ni ili wewe, ee mfalme, upate kujua tafsiri, na ili uweze kuelewa kile kilichopita mawazoni mwako.
Quant à moi, ce n'est point par une sagesse que j'aurais de plus que tous les vivants, que ce mystère m'a été dévoilé, mais c'est afin que le sens en soit découvert au roi, et que tu comprennes les pensées de ton cœur.
31 “Ee mfalme, ulitazama, na mbele yako ilisimama sanamu kubwa, kubwa mno kupita kiasi, sanamu iliyongʼaa na kutisha kwa kuonekana kwake.
O roi, tu avais une vision, et voici, [tu voyais] une grande figure; cette figure était immense, et elle avait un éclat extraordinaire; elle était debout devant toi, et son aspect était formidable.
32 Kichwa cha ile sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya fedha, tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba,
La figure était ainsi composée: elle avait la tête d'or fin, la poitrine et les bras d'argent, le ventre et les hanches d'airain,
33 miguu yake ilikuwa ya chuma, na nyayo zake zilikuwa chuma nazo sehemu nyingine zilikuwa udongo wa mfinyanzi uliochomwa.
les jambes de fer, les pieds en partie de fer, et en partie d'argile.
34 Ulipokuwa unaangalia, jiwe lilikatwa, lakini si kwa mikono ya mwanadamu. Lile jiwe liliipiga ile sanamu kwenye nyayo zake za chuma na udongo wa mfinyanzi, na kuivunja.
Tu regardais, regardais, quand sans l'aide de mains se détacha une pierre qui frappa la figure à ses pieds qui étaient de fer et d'argile, et les mit en pièces.
35 Ndipo ile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu vikavunjika vipande vipande kwa wakati mmoja, na vikawa kama makapi katika sakafu ya kupuria nafaka wakati wa kiangazi. Upepo ukavipeperusha bila kuacha hata alama. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa mno na kuijaza dunia yote.
Alors, à ce seul coup, fer, argile, airain, argent et or furent pulvérisés, et devinrent comme la balle qui s'élève de l'aire au blé, et le vent les emporta, et on n'en retrouva point de traces; et la pierre qui avait frappé la figure, devint une grande montagne, et remplit toute la terre.
36 “Hii ndiyo iliyokuwa ndoto, nasi sasa tutamfasiria mfalme.
Tel est le songe, et nous allons en exposer le sens devant le roi.
37 Ee mfalme, wewe ni mfalme wa wafalme. Mungu wa mbinguni amekupa wewe utawala, uweza, nguvu na utukufu.
Tu es, ô roi, le roi des rois, à qui le Dieu du ciel a donné l'empire, la puissance et la force et la gloire;
38 Mikononi mwako amewaweka wanadamu, wanyama wa kondeni, na ndege wa angani. Popote waishipo amekufanya wewe kuwa mtawala juu yao wote. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.
et partout où habitent des enfants des hommes, des bêtes des champs et des oiseaux du ciel, Il les a remis entre tes mains, et t'a fait le souverain d'eux tous; c'est toi qui es la tête d'or.
39 “Baada yako, ufalme mwingine utainuka, ulio dhaifu kuliko wako. Baadaye utafuata ufalme wa tatu, ule wa shaba, nao utatawala juu ya dunia yote.
Et après toi s'élèvera un autre empire, moindre que toi, puis un troisième et autre empire d'airain qui dominera sur toute la terre.
40 Hatimaye, kutakuwako na ufalme wa nne, wenye nguvu kama chuma, kwa maana chuma huvunja na kupondaponda kila kitu; kama vile chuma ivunjavyo vitu vipande vipande, ndivyo ufalme huo utakavyopondaponda na kuvunjavunja nyingine zote.
Et un quatrième empire aura la force du fer; de même que le fer brise et fracasse tout, oui, comme un fer qui met en pièces, il fracassera et pulvérisera le tout.
41 Kama vile ulivyoona kuwa kwa sehemu nyayo na vidole vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi uliochomwa na kwa sehemu nyingine chuma, hivyo huu utakuwa ufalme uliogawanyika; hata hivyo utakuwa na sehemu zenye nguvu za chuma ndani yake, kama vile ulivyoona chuma imechanganywa na udongo wa mfinyanzi.
Quant à ce que tu as vu les pieds et les orteils être en partie d'argile de potier, en partie de fer, c'est que ce sera un empire divisé; mais il y aura en lui quelque chose de la force du fer; car tu as vu le fer allié avec l'argile.
42 Kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu udongo wa mfinyanzi, hivyo ufalme huo kwa sehemu utakuwa na nguvu na kwa sehemu udhaifu.
Quant aux orteils qui étaient en partie de fer et en partie d'argile, c'est que cet empire en partie sera fort, et en partie fragile.
43 Kama vile ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyikana na udongo wa mfinyanzi uliochomwa, ndivyo watu watakavyokuwa mchanganyiko, wala hawatabaki wameungana tena, kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mfinyanzi.
Quant à ce que tu as vu le fer mêlé à l'argile, c'est qu'ils s'allieront entre eux par le mélange de races d'hommes, mais ils ne seront pas adhérents entre eux, voici, ce sera comme le fer qui ne s'allie pas avec l'argile.
44 “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atauweka ufalme ambao kamwe hautaangamizwa, wala hautaachiwa taifa jingine. Utaziponda zile falme zote na kuzikomesha, bali wenyewe utadumu milele.
Mais dans les temps de ces mêmes rois, le Dieu du ciel élèvera un empire éternellement indestructible, et dont la souveraineté ne sera dévolue à aucun autre peuple; il pulvérisera et anéantira tous ces empires; mais lui-même il subsistera éternellement,
45 Hii ndiyo maana ya maono ya jiwe lililochongwa kutoka mlimani, lakini si kwa mikono ya mwanadamu, lile jiwe ambalo lilivunja chuma, shaba, udongo wa mfinyanzi, fedha na dhahabu vipande vipande. “Mungu Mkuu amemwonyesha mfalme kile kitakachotokea wakati ujao. Ndoto hii ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.”
comme tu as vu une pierre sans l'aide de mains se détacher de la montagne, et mettre en pièces le fer, l'airain, l'argile, l'argent et l'or. Le grand Dieu a fait connaître au roi ce qui arrivera après ce temps-ci; et le songe est véridique, et l'explication en est fidèle. »
46 Ndipo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi mbele ya Danieli kumpa heshima, akaagiza wamtolee Danieli sadaka na uvumba.
Alors le roi Nébucadnézar tomba sur sa face, et se prosterna devant Daniel, et commanda de répandre devant lui des offrandes et des parfums.
47 Mfalme akamwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, na Bwana wa wafalme, na mfunuaji wa siri zote, kwa maana umeweza kufunua siri hii.”
Le roi répondit à Daniel, et dit: Il est vrai! votre Dieu est le Dieu des dieux, et le Souverain des rois, et c'est lui qui dévoile les mystères, puisque tu as été capable de me dévoiler ce mystère.
48 Ndipo mfalme akamweka Danieli nafasi ya juu, na kumpa zawadi nyingi tele. Akamfanya kuwa mtawala wa jimbo lote la Babeli, na kumweka kuwa mkuu wa wenye hekima wote.
Alors le roi éleva Daniel, et lui fit des dons nombreux et considérables, et il l'établit gouverneur de toute la province de Babel, et chef de tous les sages de Babel.
49 Zaidi ya hayo, kwa ombi la Danieli, mfalme akawateua Shadraki, Meshaki na Abednego kuwa wasimamizi wa jimbo la Babeli, huku Danieli akibaki katika ukumbi wa mfalme.
Mais sur la prière de Daniel le roi préposa à l'administration de la province de Babel, Sadrach, Mésach et Abednégo; et Daniel fut dans la Porte du roi.

< Danieli 2 >