< Danieli 2 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wake, Nebukadneza aliota ndoto. Mawazo yake yakasumbuka na hakuweza kulala.
Druge godine Nabukodonozorova kraljevanja usni Nabukodonozor sanje: njegov se duh zbog toga uznemiri, a san ga ostavi.
2 Hivyo mfalme akawaita waganga, wasihiri, wachawi na wanajimu ili wamwambie ndoto yake aliyokuwa ameota. Walipoingia ndani na kusimama mbele ya mfalme,
Kralj naredi da se pozovu čarobnici i gataoci, zaklinjači i zvjezdari da protumače kralju njegove sanje.
3 akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”
Dođoše dakle te stadoše pred kralja. Kralj im reče: “Usnih jednu sanju i moj se duh uznemiri od želje da razumijem sanju.”
4 Ndipo wanajimu wakamjibu mfalme kwa lugha ya Kiaramu, “Ee mfalme, uishi milele! Waambie watumishi wako hiyo ndoto, nasi tutaifasiri.”
Kaldejci odgovoriše kralju (aramejski): “O kralju, živ bio dovijeka! Pripovjedi svoju sanju slugama svojim, a mi ćemo ti otkriti njezino značenje.”
5 Mfalme akawajibu wanajimu, “Nimeamua hivi kwa uthabiti: Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu ilikuwa ipi na kuifasiri, mtakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vifusi.
Kralj odgovori i reče zvjezdarima: “Moja je odluka neopoziva: ako mi ne kažete što sam snio i što san znači, bit ćete rastrgani u komade, a vaše će kuće postati smetišta.
6 Lakini mkiniambia ndoto yangu na kuielezea, mtapokea kwangu zawadi, tuzo na heshima kubwa. Basi niambieni ndoto yangu na mnifasirie.”
No ako mi otkrijete moju sanju i njezino značenje, dobit ćete od mene darove i poklone i velike časti. Otkrijte mi dakle što sam snio i što san znači.”
7 Wakajibu kwa mara nyingine, “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto yake, nasi tutaifasiri.”
Oni opet odgovoriše: “Neka kralj rekne svoju sanju slugama svojim, a mi ćemo mu otkriti njezino značenje.”
8 Ndipo mfalme akajibu, “Nina hakika kuwa mnajaribu kupata muda zaidi, kwa sababu mnatambua kuwa nimeamua hivi kwa uthabiti:
A kralj: “Dobro ja znam da želite dobiti na vremenu jer znate da je moja odluka neopoziva.
9 Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu, ipo adhabu moja tu kwenu. Mmefanya shauri kuniambia habari za kunipotosha na mambo maovu, mkitumaini kwamba hali itabadilika. Hivyo basi, niambieni hiyo ndoto, nami nitajua kuwa mwaweza kunifasiria.”
Ako mi ne kažete što sam snio, znači da me namjeravate obmanjivati varavim riječima i izmišljotinama dok nekako ne prođe vrijeme. Stoga, recite mi moj san, pa ću znati da li mi možete kazati i njegovo značenje!”
10 Wanajimu wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu duniani ambaye anaweza kufanya analotaka mfalme! Vilevile hakuna mfalme hata awe mkuu na mwenye uweza namna gani, aliyeuliza kitu kama hicho kwa mganga au kwa msihiri, wala kwa mnajimu yeyote.
Zvjezdari odgovoriše pred kraljem: “Nema na svijetu čovjeka koji bi takvo što mogao otkriti kralju. I stoga nijedan kralj, ma kako velik i moćan, takvo što ne traži od čarobnika, gataoca ili zvjezdara.
11 Anachouliza mfalme ni kigumu mno. Hakuna yeyote awezaye kumfunulia mfalme isipokuwa miungu, nao hawaishi miongoni mwa wanadamu.”
Što tražiš, kralju, teško je, i nema ga tko bi to mogao otkriti kralju osim bogova, koji ne borave među smrtnicima.”
12 Jambo hili lilimkasirisha na kumghadhibisha mfalme mno hata kuagiza kuuawa kwa wenye hekima wote wa Babeli.
Tada se kralj silno razgnjevi i razbjesni te naredi da se pogube svi mudraci babilonski.
13 Hivyo amri ikatolewa ya kuwaua wenye hekima, nao watu wakatumwa kuwatafuta Danieli na rafiki zake ili wawaue.
Pošto je objavljena naredba da se ubiju mudraci, potražiše i Daniela i njegove drugove da ih pogube.
14 Wakati Arioko, mkuu wa askari wa walinzi wa mfalme, alikuwa amekwenda kuwaua watu wenye hekima wa Babeli, Danieli akazungumza naye kwa hekima na busara.
No Daniel se mudrim i umnim riječima obrati na Arjoka, zapovjednika kraljevskih straža, koji bijaše izišao da pogubi mudrace babilonske.
15 Akamuuliza huyo afisa wa mfalme, “Kwa nini mfalme ametoa amri kali hivyo?” Ndipo Arioko akamweleza Danieli jambo hilo.
On reče Arjoku, zapovjedniku kraljevu: “Zašto je kralj izdao tako strogu naredbu?” Arjok pripovjedi Danielu,
16 Aliposikia jambo hili, Danieli akamwendea mfalme, akamwomba ampe muda ili aweze kumfasiria ile ndoto.
a Daniel otiđe kralju i zamoli da mu dade vremena te će kralju otkriti što san znači.
17 Ndipo Danieli akarudi nyumbani kwake na kuwaeleza rafiki zake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo.
Daniel uđe u svoju kuću te sve kaza Hananiji, Mišaelu i Azarji, svojim drugovima,
18 Aliwasihi waombe rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusu siri hii, ili yeye na rafiki zake wasije wakauawa pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.
da mole milosrđe u Boga Nebeskoga radi te tajne, da Daniel i njegovi drugovi ne poginu s drugim mudracima babilonskim.
19 Wakati wa usiku lile fumbo lilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Ndipo Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni,
I objavi se tajna Danielu u noćnom viđenju. A Daniel blagoslovi Boga Nebeskoga.
20 na akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.
Daniel prihvati riječ i reče: “Bilo ime Božje blagoslovljeno odvijeka dovijeka, njegova je mudrost i sila.
21 Yeye hubadili nyakati na majira; huwaweka wafalme na kuwaondoa. Huwapa hekima wenye hekima, na maarifa wenye ufahamu.
On mijenja doba i vremena, ruši i postavlja kraljeve, daje mudrost mudrima a znanje pronicavima.
22 Hufunua siri na mambo yaliyofichika; anajua yale yaliyo gizani, nayo nuru hukaa kwake.
On otkriva dubine i tajne, zna što je u tminama i svjetlost prebiva u njega.
23 Ninakushukuru na kukuhimidi, Ee Mungu wa baba zangu: Umenipa hekima na uwezo, umenijulisha kile tulichokuomba, umetujulisha ndoto ya mfalme.”
Tebe, o Bože otaca mojih, slavim i hvalim što si mi dao mudrost i jakost! Evo, objavio si mi ono što smo te molili, objavio si nam što kralj traži.”
24 Ndipo Danieli akamwendea Arioko, ambaye mfalme alikuwa amemteua kuwaua wenye hekima wa Babeli, akamwambia, “Usiwaue wenye hekima wa Babeli. Nipeleke kwa mfalme, nami nitamfasiria ndoto yake.”
Daniel ode k Arjoku, kome bijaše kralj naredio da smakne mudrace babilonske. Uđe i reče mu: “Ne ubijaj mudraca babilonskih! Odvedi me kralju, pa ću mu otkriti što san znači.”
25 Arioko akampeleka Danieli kwa mfalme mara moja na kumwambia, “Nimempata mtu miongoni mwa watu wa uhamisho kutoka Yuda ambaye anaweza kumwambia mfalme maana ya ndoto yake.”
Arjok žurno odvede Daniela kralju i reče: “Našao sam među izgnanicima judejskim čovjeka koji će kralju kazati što san znači.”
26 Mfalme akamuuliza Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza), “Je, unaweza kuniambia nilichoona katika ndoto yangu na kuifasiri?”
Kralj reče Danielu (koji se zvaše Baltazar): “Jesi li kadar kazati mi san koji sam usnio i što znači?”
27 Danieli akajibu, “Hakuna mwenye hekima, msihiri, mganga au mwaguzi anayeweza kumweleza mfalme siri aliyouliza,
Daniel odgovori pred kraljem: “Tajnu koju istražuje kralj ne mogahu kralju otkriti mudraci, čarobnici, gataoci i zaklinjači;
28 lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri. Amemwonyesha Mfalme Nebukadneza kitakachotokea siku zijazo. Ndoto yako na maono yaliyopita mawazoni mwako ulipokuwa umelala kitandani mwako ni haya:
ali ima na nebu Bog koji objavljuje tajne i on je saopćio kralju Nabukodonozoru ono što će biti na svršetku dana. Evo tvoje sanje i onoga što ti se prividjelo na postelji:
29 “Ee mfalme, ulipokuwa umelala kitandani, yalikujia mawazo kuhusu mambo yatakayotokea baadaye, naye mfunuaji wa siri akakuonyesha ni kitu gani kitakachotokea.
O kralju, na tvojoj ti postelji dođoše misli o tome što će se dogoditi kasnije, a Otkrivatelj tajna saopćio ti je ono što će biti.
30 Kwangu mimi, nimefunuliwa siri hii, si kwa sababu nina hekima kubwa kuliko watu wengine wanaoishi, bali ni ili wewe, ee mfalme, upate kujua tafsiri, na ili uweze kuelewa kile kilichopita mawazoni mwako.
Iako nemam mudrosti više nego ostali smrtnici, ta mi je tajna objavljena samo zato da njezino značenje saopćim kralju i da upoznaš misli svoga srca.
31 “Ee mfalme, ulitazama, na mbele yako ilisimama sanamu kubwa, kubwa mno kupita kiasi, sanamu iliyongʼaa na kutisha kwa kuonekana kwake.
Ti si, o kralju, imao viđenje: gle, kip, golem kip, vrlo blistav, stajaše pred tobom, strašan za oči.
32 Kichwa cha ile sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya fedha, tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba,
Tome kipu glava bijaše od čistog zlata, prsa i ruke od srebra, trbuh i bedra od mjedi,
33 miguu yake ilikuwa ya chuma, na nyayo zake zilikuwa chuma nazo sehemu nyingine zilikuwa udongo wa mfinyanzi uliochomwa.
gnjati od željeza, a stopala dijelom od željeza, dijelom od gline.
34 Ulipokuwa unaangalia, jiwe lilikatwa, lakini si kwa mikono ya mwanadamu. Lile jiwe liliipiga ile sanamu kwenye nyayo zake za chuma na udongo wa mfinyanzi, na kuivunja.
Ti si promatrao: iznenada se odvali kamen a da ga ne dodirnu ruka, pa udari u kip, u stopala od željeza i gline te ih razbi.
35 Ndipo ile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu vikavunjika vipande vipande kwa wakati mmoja, na vikawa kama makapi katika sakafu ya kupuria nafaka wakati wa kiangazi. Upepo ukavipeperusha bila kuacha hata alama. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa mno na kuijaza dunia yote.
Tada se smrvi najednom željezo i glina, mjed, srebro i zlato, i sve postade kao pljeva na gumnu ljeti i vjetar sve odnese bez traga. A kamen koji bijaše u kip udario postade veliko brdo te napuni svu zemlju.
36 “Hii ndiyo iliyokuwa ndoto, nasi sasa tutamfasiria mfalme.
To bijaše sanja; a njezino ćemo značenje reći pred kraljem.”
37 Ee mfalme, wewe ni mfalme wa wafalme. Mungu wa mbinguni amekupa wewe utawala, uweza, nguvu na utukufu.
“Ti, o kralju, kralju kraljeva, komu Bog Nebeski dade kraljevstvo, silu moć i slavu -
38 Mikononi mwako amewaweka wanadamu, wanyama wa kondeni, na ndege wa angani. Popote waishipo amekufanya wewe kuwa mtawala juu yao wote. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.
i u čije je ruke stavio, gdje god se našli, sinove ljudske, životinje poljske, ptice nebeske i postavio te gospodarom nad svim time - ti si glava od zlata.
39 “Baada yako, ufalme mwingine utainuka, ulio dhaifu kuliko wako. Baadaye utafuata ufalme wa tatu, ule wa shaba, nao utatawala juu ya dunia yote.
Poslije tebe ustat će drugo kraljevstvo, slabije od tvoga, pa treće, od mjedi, koje će gospodariti svom zemljom.
40 Hatimaye, kutakuwako na ufalme wa nne, wenye nguvu kama chuma, kwa maana chuma huvunja na kupondaponda kila kitu; kama vile chuma ivunjavyo vitu vipande vipande, ndivyo ufalme huo utakavyopondaponda na kuvunjavunja nyingine zote.
A četvrto kraljevstvo bit će tvrdo poput željeza, poput željeza koje sve satire i mrvi; kao željezo koje razbija, skršit će i razbit sva ona kraljevstva.
41 Kama vile ulivyoona kuwa kwa sehemu nyayo na vidole vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi uliochomwa na kwa sehemu nyingine chuma, hivyo huu utakuwa ufalme uliogawanyika; hata hivyo utakuwa na sehemu zenye nguvu za chuma ndani yake, kama vile ulivyoona chuma imechanganywa na udongo wa mfinyanzi.
Stopala koja si vidio, dijelom glina a dijelom željezo, jesu podijeljeno kraljevstvo; imat će nešto od čvrstoće željeza prema onome što si vidio željezo izmiješano s glinom.
42 Kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu udongo wa mfinyanzi, hivyo ufalme huo kwa sehemu utakuwa na nguvu na kwa sehemu udhaifu.
Prsti stopala, dijelom željezo a dijelom glina: kraljevstvo će biti dijelom čvrsto a dijelom krhko.
43 Kama vile ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyikana na udongo wa mfinyanzi uliochomwa, ndivyo watu watakavyokuwa mchanganyiko, wala hawatabaki wameungana tena, kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mfinyanzi.
A što si vidio željezo izmiješano s glinom: oni će se miješati ljudskim sjemenom, ali se neće držati zajedno, kao što se ni željezo ne da pomiješati s glinom.
44 “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atauweka ufalme ambao kamwe hautaangamizwa, wala hautaachiwa taifa jingine. Utaziponda zile falme zote na kuzikomesha, bali wenyewe utadumu milele.
U vrijeme ovih kraljeva Bog Nebeski podići će kraljevstvo koje neće nikada propasti i neće prijeći na neki drugi narod. Ono će razbiti i uništiti sva ona kraljevstva, a samo će stajati dovijeka -
45 Hii ndiyo maana ya maono ya jiwe lililochongwa kutoka mlimani, lakini si kwa mikono ya mwanadamu, lile jiwe ambalo lilivunja chuma, shaba, udongo wa mfinyanzi, fedha na dhahabu vipande vipande. “Mungu Mkuu amemwonyesha mfalme kile kitakachotokea wakati ujao. Ndoto hii ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.”
kao što si vidio da se kamen s brijega odvalio a da ga ne dodirnu ruka te smrvio željezo, mjed, glinu, srebro i zlato. Veliki je Bog saopćio kralju što se ima dogoditi. Sanja je istinita, a tumačenje joj pouzdano.”
46 Ndipo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi mbele ya Danieli kumpa heshima, akaagiza wamtolee Danieli sadaka na uvumba.
Nato kralj Nabukodonozor pade ničice i pokloni se pred Danielom. Naredi da mu prinesu dar i kad.
47 Mfalme akamwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, na Bwana wa wafalme, na mfunuaji wa siri zote, kwa maana umeweza kufunua siri hii.”
I reče kralj Danielu: “Zaista, vaš je bog Bog nad bogovima i gospodar nad kraljevima, Otkrivatelj tajna, kad si mogao otkriti ovu tajnu.”
48 Ndipo mfalme akamweka Danieli nafasi ya juu, na kumpa zawadi nyingi tele. Akamfanya kuwa mtawala wa jimbo lote la Babeli, na kumweka kuwa mkuu wa wenye hekima wote.
Kralj uzvisi Daniela i dariva ga mnogim blistavim darovima. Postavi ga upraviteljem sve pokrajine babilonske i starješinom svih mudraca babilonskih.
49 Zaidi ya hayo, kwa ombi la Danieli, mfalme akawateua Shadraki, Meshaki na Abednego kuwa wasimamizi wa jimbo la Babeli, huku Danieli akibaki katika ukumbi wa mfalme.
Daniel zamoli kralja da odredi za upravitelje pokrajine babilonske Šadraka, Mešaka i Abed Nega, a Daniel ostade na kraljevu dvoru.

< Danieli 2 >