< Danieli 2 >

1 Katika mwaka wa pili wa utawala wake, Nebukadneza aliota ndoto. Mawazo yake yakasumbuka na hakuweza kulala.
Nebukhadnezar a bawinae a kum pahni navah, a mang lah a hmu e hno dawkvah roumkalue teh ip thai hoeh.
2 Hivyo mfalme akawaita waganga, wasihiri, wachawi na wanajimu ili wamwambie ndoto yake aliyokuwa ameota. Walipoingia ndani na kusimama mbele ya mfalme,
Hat toteh, siangpahrang ni a ram thung kaawm e mitpalei kathoumnaw, kutkhetkathoumnaw, kahrai ka pâlei thainaw hoi, Khaldeannaw hah pâkhueng awh ati e patetlah ahnimanaw a tho awh teh,
3 akawaambia, “Niliota ndoto inayonisumbua, nami nataka nijue maana yake.”
siangpahrang ni ka mang lah ka hmu e hah bang ngainae ne, ka panue thai hoeh dawkvah, ka lung nawm hoeh, dei awh haw atipouh.
4 Ndipo wanajimu wakamjibu mfalme kwa lugha ya Kiaramu, “Ee mfalme, uishi milele! Waambie watumishi wako hiyo ndoto, nasi tutaifasiri.”
Hatnavah Khaldeannaw ni Aramaih lawk lahoi, siangpahrang na hring saw seh. Kaimouh koe na mang hah rui haw. Kaimouh ni na mang teh ka leh awh vai nei atipouh awh.
5 Mfalme akawajibu wanajimu, “Nimeamua hivi kwa uthabiti: Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu ilikuwa ipi na kuifasiri, mtakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vifusi.
Siangpahrang ni yo ka dei toung hat tayaw. Hote mang hoi a ngainae na dei thai awh hoehpawiteh, tawntarawn lah na tâtueng awh han. Na imlawnaw hai vaipuen songnawng lah ka coung sak han atipouh.
6 Lakini mkiniambia ndoto yangu na kuielezea, mtapokea kwangu zawadi, tuzo na heshima kubwa. Basi niambieni ndoto yangu na mnifasirie.”
Mang hoi deingainae na deicai pawiteh, poehnonaw, tawkphunaw hoi barinae kalen a hmu han. Hatdawkvah, mang hoi deingainae hah kai koe dei awh telah Khaldean a lungkaangnaw koe atipouh.
7 Wakajibu kwa mara nyingine, “Mfalme na awaambie watumishi wake ndoto yake, nasi tutaifasiri.”
Ahnimanaw ni, siangpahrang, na mang hah kaimouh koe dei haw, kaimouh ni ka leh awh vainei bout atipouh awh.
8 Ndipo mfalme akajibu, “Nina hakika kuwa mnajaribu kupata muda zaidi, kwa sababu mnatambua kuwa nimeamua hivi kwa uthabiti:
Hat toteh, siangpahrang ni yo ka dei toung hatayaw. A hnin thapa asaw nahanelah atueng tahruet sak hane doeh na ngai awh tie ka panue.
9 Ikiwa hamtaniambia ndoto yangu, ipo adhabu moja tu kwenu. Mmefanya shauri kuniambia habari za kunipotosha na mambo maovu, mkitumaini kwamba hali itabadilika. Hivyo basi, niambieni hiyo ndoto, nami nitajua kuwa mwaweza kunifasiria.”
Mang hah na dei awh hoehpawiteh, pouknae buet touh duengdoeh kaawm. Atueng kasaw nakunghai, laithoe hrawnghrang doeh dei hanelah na kâcai awh toe. Mang hah bout deih awh. Hottelah na dei thai awh pawiteh, leh hai na leh thai awh han tie ka panue bout atipouh.
10 Wanajimu wakamjibu mfalme, “Hakuna mtu duniani ambaye anaweza kufanya analotaka mfalme! Vilevile hakuna mfalme hata awe mkuu na mwenye uweza namna gani, aliyeuliza kitu kama hicho kwa mganga au kwa msihiri, wala kwa mnajimu yeyote.
Khaldeannaw ni, siangpahrang nang ni na dei e patetlah ka dei thai hane tami buet touh boehai awm hoeh. Bangpatet e siangpahrang ni hai a lentoe eiteh, mitpaleikathoumnaw, camkathoumnaw, Khaldean taminaw koe hettelah pacei boihoeh.
11 Anachouliza mfalme ni kigumu mno. Hakuna yeyote awezaye kumfunulia mfalme isipokuwa miungu, nao hawaishi miongoni mwa wanadamu.”
Siangpahrang nang ni na pacei e teh, ka ru poung e hno doeh. Tami lah kaawm hoeh e Cathut hloilah apinihai pâpho thai mahoeh bout atipouh awh.
12 Jambo hili lilimkasirisha na kumghadhibisha mfalme mno hata kuagiza kuuawa kwa wenye hekima wote wa Babeli.
Hote lawk hah a thai navah, puenghoi a lungkhuek teh, Babilon kho dawk kaawm e tami lungkaangnaw pueng koung thei lah awmseh telah kâ a poe.
13 Hivyo amri ikatolewa ya kuwaua wenye hekima, nao watu wakatumwa kuwatafuta Danieli na rafiki zake ili wawaue.
Hat toteh, hote kâ hah a pathang awh teh, a lungkaangnaw thei a kamtawng awh teh, Daniel hoi a huinaw hah thei hanlah a tawng awh.
14 Wakati Arioko, mkuu wa askari wa walinzi wa mfalme, alikuwa amekwenda kuwaua watu wenye hekima wa Babeli, Danieli akazungumza naye kwa hekima na busara.
Daniel ni bangkongmaw siangpahrang e kâ teh, hettelah totouh a rang vaw telah,
15 Akamuuliza huyo afisa wa mfalme, “Kwa nini mfalme ametoa amri kali hivyo?” Ndipo Arioko akamweleza Danieli jambo hilo.
Babilon tami lungkaangnaw thei hanlah ka cet e naw kahrawikung, siangpahrang ka ring e Ariok koe kâhruetcuet laihoi a pacei.
16 Aliposikia jambo hili, Danieli akamwendea mfalme, akamwomba ampe muda ili aweze kumfasiria ile ndoto.
Ariok ni hote konglamnaw hah a dei navah, Daniel ni siangpahrang im a kâen teh, hote mang deicai nahanelah atueng na poe ei telah a kâhei.
17 Ndipo Danieli akarudi nyumbani kwake na kuwaeleza rafiki zake Hanania, Mishaeli na Azaria jambo hilo.
Hahoi ama im a ban teh, hote akongnaw hah a huinaw Hananiah, Mishael, Azariah tinaw koe a dei pouh.
18 Aliwasihi waombe rehema kutoka kwa Mungu wa mbinguni kuhusu siri hii, ili yeye na rafiki zake wasije wakauawa pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.
Hat toteh, maimouh teh alouke Babilon a lungkaangnaw hoi reirei due awh hoeh nahanelah, hete hrolawk dawk lungmanae coe awh nahan, kalvan Cathut koe ratoum awh sei ati awh.
19 Wakati wa usiku lile fumbo lilifunuliwa kwa Danieli katika maono. Ndipo Danieli akamhimidi Mungu wa mbinguni,
Karum toteh Cathut ni vision lahoi, hote hrolawk hah Daniel koe a dei pouh.
20 na akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.
Hat toteh, Daniel ni kalvan Cathut e lungmanae hah a pholen teh, Cathut min teh a yungyoe hoi a yungyoe ditouh pholen lah awmseh. Lungangnae hoi hnotithainae hoi akawi.
21 Yeye hubadili nyakati na majira; huwaweka wafalme na kuwaondoa. Huwapa hekima wenye hekima, na maarifa wenye ufahamu.
A tue hoi khotue naw hah a kâthung sak. Siangpahrangnaw hai a pabo, a tawmtakhang, a lungkaang e naw koe lungangnae na poe. Kho ka pouk thai naw ni hai na lungmanae dawk hoi doeh a panue thai awh.
22 Hufunua siri na mambo yaliyofichika; anajua yale yaliyo gizani, nayo nuru hukaa kwake.
Ka ru e hnonaw hai kamcengcalah, na patue awh. A hmonae koe kaawm e pueng na panue teh, nama koe angnae teh ao.
23 Ninakushukuru na kukuhimidi, Ee Mungu wa baba zangu: Umenipa hekima na uwezo, umenijulisha kile tulichokuomba, umetujulisha ndoto ya mfalme.”
Mintoenaw e Cathut, hnotithainae hoi lungangnae na poe teh, kaimouh ni ka ratoum awh e patetlah siangpahrang e a mang pâpho thainae lungangnae teh ka pholen telah Daniel ni a ratoum.
24 Ndipo Danieli akamwendea Arioko, ambaye mfalme alikuwa amemteua kuwaua wenye hekima wa Babeli, akamwambia, “Usiwaue wenye hekima wa Babeli. Nipeleke kwa mfalme, nami nitamfasiria ndoto yake.”
Hathnukkhu Babilon lungkaangnaw thei hanlah a patoun e Ariok koe a cei teh, Babilon tami lungkaangnaw hah thet hanh. Kai hah siangpahrang koe na thak haw. Kai ni mang hoi deingainae hah ka pâpho pouh vainei atipouh.
25 Arioko akampeleka Danieli kwa mfalme mara moja na kumwambia, “Nimempata mtu miongoni mwa watu wa uhamisho kutoka Yuda ambaye anaweza kumwambia mfalme maana ya ndoto yake.”
Hat toteh, Ariok ni Daniel hah karanglah siangpahrang koe a hrawi teh, siangpahrang, nange mang hoi deingainae ka pâpho thai e tami Judahnaw man e thung dawk e buet touh ka hmu toe atipouh.
26 Mfalme akamuuliza Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza), “Je, unaweza kuniambia nilichoona katika ndoto yangu na kuifasiri?”
Siangpahrang ni kai ni ka mang e mang hah dei vaiteh deingainae hah na pâpho thai han maw telah Belteshazzar tie Daniel hah a pacei navah,
27 Danieli akajibu, “Hakuna mwenye hekima, msihiri, mganga au mwaguzi anayeweza kumweleza mfalme siri aliyouliza,
Daniel ni siangpahrang, nang ni na pacei e hah a lungkaangnaw, camkathoumnaw, mitpaleikathoumnaw, hoi khueyuenaw ni pâpho thai mahoeh.
28 lakini yuko Mungu mbinguni afunuaye siri. Amemwonyesha Mfalme Nebukadneza kitakachotokea siku zijazo. Ndoto yako na maono yaliyopita mawazoni mwako ulipokuwa umelala kitandani mwako ni haya:
Hro e naw ka pâpho niteh, ato hmalah ka tho hane naw siangpahrang nang koe ka dei pouh e Cathut buet touh duengdoeh kalvan vah kaawm.
29 “Ee mfalme, ulipokuwa umelala kitandani, yalikujia mawazo kuhusu mambo yatakayotokea baadaye, naye mfunuaji wa siri akakuonyesha ni kitu gani kitakachotokea.
Oe siangpahrang, na i navah ato hmalah ka tho hane naw hah na pouk. Hro e naw kapâphokung Cathut ni ato hmalah ka tho hane naw hah nang koe na patue.
30 Kwangu mimi, nimefunuliwa siri hii, si kwa sababu nina hekima kubwa kuliko watu wengine wanaoishi, bali ni ili wewe, ee mfalme, upate kujua tafsiri, na ili uweze kuelewa kile kilichopita mawazoni mwako.
Hete hro e hno hah, kai teh alouke moithangnaw hlak hoe ka lungang dawkvah kai koe a pâpho e nahoeh. Nang ni na lungthung na pouk e naw hah na panue thai nahanlah doeh deingainae naw hah Cathut ni na pâpho pouh.
31 “Ee mfalme, ulitazama, na mbele yako ilisimama sanamu kubwa, kubwa mno kupita kiasi, sanamu iliyongʼaa na kutisha kwa kuonekana kwake.
Siangpahrang, na i lahun nah na mang e vision teh, na khet navah meikaphawk hah na hmu. Athakaawme lah ao. Hote meikaphawk teh, taki ka tho e meilam hoi na hmalah a kâpâhung.
32 Kichwa cha ile sanamu kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi, kifua chake na mikono yake vilikuwa vya fedha, tumbo lake na mapaja yake vilikuwa vya shaba,
A lû teh sui, a lungtabue hoi a kut roi teh ngun lah ao.
33 miguu yake ilikuwa ya chuma, na nyayo zake zilikuwa chuma nazo sehemu nyingine zilikuwa udongo wa mfinyanzi uliochomwa.
A von hoi a phai roi teh, rahum lah ao. A khok buembue roi teh sum lah ao. Khoktabei hoi khoksampha teh sum atangawn amhru atangawn lah ao.
34 Ulipokuwa unaangalia, jiwe lilikatwa, lakini si kwa mikono ya mwanadamu. Lile jiwe liliipiga ile sanamu kwenye nyayo zake za chuma na udongo wa mfinyanzi, na kuivunja.
Nang ni na khet lahun nah, kut hoi sak hoeh e amahmawk kaawm e talung buet touh ni, meikaphawk e khok sum tangawn amhru tangawn e koe a ten torei teh,
35 Ndipo ile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha na ile dhahabu vikavunjika vipande vipande kwa wakati mmoja, na vikawa kama makapi katika sakafu ya kupuria nafaka wakati wa kiangazi. Upepo ukavipeperusha bila kuacha hata alama. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa mno na kuijaza dunia yote.
sum, amhru, rahum, ngun, sui naw teh, reppasei lah ao. Kawmpoi vah, cangkatinnae koe e vaiphu patetlah ao nahan awm laipalah, kahlî ni a palek teh a kahma. Meikaphawk ka ten e talung a roung teh, kalenpounge mon lah a coung. Talaivan pueng koung a ramuk telah mang na sak.
36 “Hii ndiyo iliyokuwa ndoto, nasi sasa tutamfasiria mfalme.
Atuvah, mang ni deingainae na dei pouh vai.
37 Ee mfalme, wewe ni mfalme wa wafalme. Mungu wa mbinguni amekupa wewe utawala, uweza, nguvu na utukufu.
Siangpahrang, nang teh siangpahrangnaw e siangpahrang lah na o. Kalvan Cathut ni uknaeram, thasainae, hoi bawilennae na poe toe.
38 Mikononi mwako amewaweka wanadamu, wanyama wa kondeni, na ndege wa angani. Popote waishipo amekufanya wewe kuwa mtawala juu yao wote. Wewe ndiye kile kichwa cha dhahabu.
Tami khosaknae hmuen pueng koe, saringnaw hoi kahlun e tavanaw pueng na kut dawk poe lah ao teh, abuemlahoi uknae kâ na tawn. Nang teh, meikaphawk e suilû lah na o.
39 “Baada yako, ufalme mwingine utainuka, ulio dhaifu kuliko wako. Baadaye utafuata ufalme wa tatu, ule wa shaba, nao utatawala juu ya dunia yote.
Nang hnukkhu lah, nang patetlah kalen hoeh e alouke uknaeram a tâco han. Hathnukkhu talai van pueng ka uk hane apâthum e rahum ram a tâco han.
40 Hatimaye, kutakuwako na ufalme wa nne, wenye nguvu kama chuma, kwa maana chuma huvunja na kupondaponda kila kitu; kama vile chuma ivunjavyo vitu vipande vipande, ndivyo ufalme huo utakavyopondaponda na kuvunjavunja nyingine zote.
Apalinae uknaeram teh, sum patetlah kate e lah ao han. Sum teh alouke hno pueng a raphoe thai e patetlah apalinae ram ni raphoe vaiteh, a rektap han.
41 Kama vile ulivyoona kuwa kwa sehemu nyayo na vidole vilikuwa vya udongo wa mfinyanzi uliochomwa na kwa sehemu nyingine chuma, hivyo huu utakuwa ufalme uliogawanyika; hata hivyo utakuwa na sehemu zenye nguvu za chuma ndani yake, kama vile ulivyoona chuma imechanganywa na udongo wa mfinyanzi.
Kutsak e khoktabei hoi khoksamphanaw teh, sum tangawn amhru tangawn lah ao e hah na hmu e patetlah, buet touh hoi buet touh kâtaran e uknaeram lah ao han. Hatei, amhru pâeng e hoi sum kalawt e na hmu e patetlah sum teh a tê han.
42 Kama vile vidole vyake vya miguu vilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu udongo wa mfinyanzi, hivyo ufalme huo kwa sehemu utakuwa na nguvu na kwa sehemu udhaifu.
Khokcareinaw teh sum tangawn amhru tangawn lah ao e na hmu e patetlah, uknaeram atangawn teh a tê han, atangawn teh a rawk a yawi han.
43 Kama vile ulivyoona chuma kikiwa kimechanganyikana na udongo wa mfinyanzi uliochomwa, ndivyo watu watakavyokuwa mchanganyiko, wala hawatabaki wameungana tena, kama vile chuma kisivyoweza kuchanganyikana na udongo wa mfinyanzi.
Amhru pâeng e hoi sum kalawt e hah na hmu e patetlah khocanaw teh ram alouknaw hoi a kâkalawt awh han. Hatei, amhru hoi sum a kâkalawt thai hoeh e patetlah buet touh hoi buet touh kâpo thai mahoeh.
44 “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atauweka ufalme ambao kamwe hautaangamizwa, wala hautaachiwa taifa jingine. Utaziponda zile falme zote na kuzikomesha, bali wenyewe utadumu milele.
Kut hoi sak hoeh e talung buet touh ni mon hoi amahmawk a kamlei teh, sum, rahum, ngun, sui, amhrunaw hah reppasei lah a ten e na hmu e hateh, rawknae koe ka phat thai hoeh e, hote bawinae tueng nah kalvan Cathut ni uknaeram a kangdue sak han. Hote teh Jentelnaw e kut dawk phat toung laipalah, ahmaloe dei tangcoung e ram pueng hah raphoe vaiteh, a yungyoe a cak han.
45 Hii ndiyo maana ya maono ya jiwe lililochongwa kutoka mlimani, lakini si kwa mikono ya mwanadamu, lile jiwe ambalo lilivunja chuma, shaba, udongo wa mfinyanzi, fedha na dhahabu vipande vipande. “Mungu Mkuu amemwonyesha mfalme kile kitakachotokea wakati ujao. Ndoto hii ni ya kweli na tafsiri yake ni ya kuaminika.”
Hottelah, ato hmalah ka tho hane hnonaw hah ka lentoe poung e Cathut ni siangpahrang nang koe a dei e doeh. Nange mang teh, katang e doeh. Deicainae hai kahman e doeh telah Daniel ni a dei pouh.
46 Ndipo Mfalme Nebukadneza akaanguka kifudifudi mbele ya Danieli kumpa heshima, akaagiza wamtolee Danieli sadaka na uvumba.
Hattoteh siangpahrang ni Daniel hmalah a tabo teh barinae a poe. Hmuitui hmaisawi hane hoi pasoumhno pasoung hanelah kâ a poe hnukkhu,
47 Mfalme akamwambia Danieli, “Hakika Mungu wako ni Mungu wa miungu, na Bwana wa wafalme, na mfunuaji wa siri zote, kwa maana umeweza kufunua siri hii.”
nang ni hete hrolawk hah na pâpho thai dawkvah, atangcalah nange Cathut teh, cathutnaw e Cathut, siangpahrangnaw e Bawi, hrolawk ka pâpho thai e Bawipa doeh telah a ti.
48 Ndipo mfalme akamweka Danieli nafasi ya juu, na kumpa zawadi nyingi tele. Akamfanya kuwa mtawala wa jimbo lote la Babeli, na kumweka kuwa mkuu wa wenye hekima wote.
Hat toteh, Daniel hah thaw a luen sak teh, hnopai moikapap a poe hnukkhu, Babilon ram dawk bawi lah thoseh, Babilon lungkaangnaw kaukkung bawi lah a ta.
49 Zaidi ya hayo, kwa ombi la Danieli, mfalme akawateua Shadraki, Meshaki na Abednego kuwa wasimamizi wa jimbo la Babeli, huku Danieli akibaki katika ukumbi wa mfalme.
Hat toteh, Daniel ni a kâhei e patetlah siangpahrang ni, Shadrak, Meshak, hoi Abednego tinaw hah Babilon ram thung thaw katawkkung lah a ta. Hatei, Daniel teh siangpahrang im vah a tahung.

< Danieli 2 >