< Danieli 12 >
1 “Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
Tanī laikā celsies Miķelis, tas lielais valdnieks, kas tavu ļaužu bērnus aizstāv, un tad būs tāds bēdu laiks, kāds vēl nav bijis, kamēr ļaudis bijuši, līdz tam laikam. Un tanī laikā tavi ļaudis taps izpestīti, visi, kas atrodas grāmatā rakstīti.
2 Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
Un daudz no tiem, kas guļ zemes pīšļos, uzmodīsies, citi uz mūžīgu dzīvošanu, bet citi uz mūžīgu kaunu un negantību.
3 Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
Bet mācītāji spīdēs kā debess spožums, un kas daudzus veduši uz taisnību, kā zvaigznes mūžīgi mūžam.
4 Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
Un tu, Daniēl, apslēp šos vārdus un aizzieģelē šo grāmatu līdz pēdējam laikam, tad daudzi meklēs tikuši(visapkārt), un atzīšana vairosies.
5 Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
Un es, Daniēls, skatījos, un redzi, divi citi stāvēja, viens šai upes malā un otrs otrā upes malā.
6 Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
Un viens sacīja uz to vīru, kas bija ģērbts nātnu drēbēs, kas upes virsū stāvēja: cik ilgi tas būs, kad tiem brīnumiem būs gals?
7 Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
Un es dzirdēju to vīru, kas bija ģērbts nātnu drēbēs un stāvēja upes virsū, tas pacēla savu labo un kreiso roku pret debesīm un zvērēja pie Tā, kas dzīvo mūžīgi, ka viss tas notiks pēc viena laika, diviem laikiem un pus laika, un kad tās svētās tautas klīšana būs beigta.
8 Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
To es dzirdēju, bet nesapratu, un sacīju: mans kungs, kas būs tam visam gals?
9 Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
Un viņš sacīja: ej, Daniēl, jo šie vārdi ir apslēpti un aizzieģelēti līdz gala laikam.
10 Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
Daudzi taps šķīstīti un tīrīti un kausēti, un tie bezdievīgie būs bezdievīgi, un tie bezdievīgie visi to neliks vērā, bet tie prātīgie to liks vērā.
11 “Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
Un no tā laika, kad tas ikdienas upuris kļūs atņemts un tā negantība un postīšana notiks, būs tūkstoš divi simti un deviņdesmit dienas.
12 Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
Svētīgs ir, kas sagaida un aizsniedz tūkstoš trīs simti trīsdesmit un piecas dienas.
13 “Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”
Bet tu noej līdz galam, un tu dusēsi un atkal celsies, savu daļu dabūt pastarā laikā.