< Danieli 12 >

1 “Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
“At that time Michael, the great prince who guards your people, will rise up. There will be a time of trouble such as never was since the beginning of any nation until that time. At that time your people will be saved, everyone whose name is found written in the book.
2 Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
Many of those who sleep in the dust of the earth will rise up, some to everlasting life and some to shame and everlasting contempt.
3 Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
Those who are wise will shine like the brightness of the sky above, and those who turn many to righteousness, are like the stars forever and ever.
4 Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
But you, Daniel, close up these words; keep the book sealed until the time of the end. Many will run here and there, and knowledge will increase.”
5 Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
Then I, Daniel, looked, and there were two others standing. One stood on the bank on this side of the river, and one stood on the bank on the other side of the river.
6 Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
One of them said to the man clothed in linen, the one who was upstream along the river, “How long will it be to the end of these amazing events?”
7 Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
I heard the man clothed in linen, who was upstream along the river—he raised his right hand and his left hand to heaven and swore by the one who lives forever that it would be for a time, times, and half a time. When the power of the holy people has been finally broken, all these things will be completed.
8 Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
I heard, but I did not understand. So I asked, “My master, what will be the outcome of all these things?”
9 Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
He said, “Go your way, Daniel, for the words are shut up and sealed until the time of the end.
10 Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
Many will be purified, cleansed, and refined, but the wicked will act wickedly. None of the wicked will understand, but those who are wise will understand.
11 “Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
From the time that the regular burnt offering is taken away and the abomination that causes complete desolation is set up, there will be 1,290 days.
12 Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
Blessed is the one who waits until the end of the 1,335 days.
13 “Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”
You must go your way until the end, and you will rest. You will rise in the place assigned to you, at the end of days.”

< Danieli 12 >