< Danieli 12 >

1 “Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
and in/on/with time [the] he/she/it to stand: rise Michael [the] ruler [the] great: large [the] to stand: appoint upon son: descendant/people people your and to be time distress which not to be from to be nation till [the] time [the] he/she/it and in/on/with time [the] he/she/it to escape people your all [the] to find to write in/on/with scroll: book
2 Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
and many from sleeping land: soil dust to awake these to/for life forever: enduring and these to/for reproach to/for abhorrence forever: enduring
3 Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
and [the] be prudent to shine like/as brightness [the] expanse and to justify [the] many like/as star to/for forever: enduring and perpetuity
4 Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
and you(m. s.) Daniel to close [the] word and to seal [the] scroll: book till time end to rove many and to multiply [the] knowledge
5 Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
and to see: see I Daniel and behold two another to stand: stand one here/thus to/for lip: shore [the] stream and one here/thus to/for lip: shore [the] stream
6 Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
and to say to/for man to clothe [the] linen which from above to/for water [the] stream till how end [the] wonder
7 Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
and to hear: hear [obj] [the] man to clothe [the] linen which from above to/for water [the] stream and to exalt right his and left his to(wards) [the] heaven and to swear in/on/with alive [the] forever: enduring for to/for meeting: time appointed meeting: time appointed and half and like/as to end: finish to shatter hand: power people holiness to end: finish all these
8 Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
and I to hear: hear and not to understand and to say [emph?] lord my what? end these
9 Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
and to say to go: journey Daniel for to close and to seal [the] word till time end
10 Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
to purify and to whiten and to refine many and be wicked wicked and not to understand all wicked and [the] be prudent to understand
11 “Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
and from time to turn aside: remove [the] continually and to/for to give: put abomination be desolate: destroyed day thousand hundred and ninety
12 Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
blessed [the] to wait and to touch to/for day thousand three hundred thirty and five
13 “Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”
and you(m. s.) to go: journey to/for end and to rest and to stand: stand to/for allotted your to/for end [the] day

< Danieli 12 >