< Danieli 12 >
1 “Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
And at that time Michael shall stand up, the great prince who stands for the sons of thy people. And there shall be a time of trouble, such as never was since there was a nation even to that same time. And at that time thy people shall be delivered, everyone who shall be found written in the book.
2 Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
And many of those who sleep in the dust of the earth shall awake, some to everlasting life, and some to shame and everlasting contempt.
3 Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
And those who are wise shall shine as the brightness of the firmament, and those who turn many to righteousness as the stars forever and ever.
4 Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
But thou, O Daniel, shut up the words, and seal the book, even to the time of the end. Many shall run to and fro, and knowledge shall be increased.
5 Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
Then I, Daniel, looked, and, behold, another two stood, the one on the brink of the river on this side, and the other on the brink of the river on that side.
6 Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
And one said to the man clothed in linen, who was above the waters of the river, How long shall it be to the end of these wonders?
7 Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
And I heard the man clothed in linen, who was above the waters of the river, when he held up his right hand and his left hand to heaven, and swore by him who lives forever that it shall be for a time, times, and a half. And when they have made an end of breaking in pieces the power of the holy people, all these things shall be finished.
8 Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
And I heard, but I did not understand. Then I said, O my lord, what shall be the outcome of these things?
9 Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
And he said, Go thy way, Daniel, for the words are shut up and sealed till the time of the end.
10 Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
Many shall purify themselves, and make themselves white, and be refined, but the wicked shall do wickedly. And none of the wicked shall understand, but those who are wise shall understand.
11 “Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
And from the time that the continual burnt offering shall be taken away, and the abomination that makes desolate is set up, there shall be a thousand and two hundred and ninety days.
12 Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
Blessed is he who waits, and comes to the thousand three hundred and thirty-five days.
13 “Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”
But go thou thy way till the end is. For thou shall rest, and shall stand in thy lot at the end of the days.