< Danieli 12 >

1 “Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
Toho času postaví se Michal, kníže veliké, kterýž zastává synů lidu tvého, a bude čas ssoužení, jakéhož nebylo, jakž jest národ, až do toho času; toho, pravím, času vysvobozen bude lid tvůj, kdožkoli nalezen bude zapsaný v knize.
2 Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
Tuť mnozí z těch, kteříž spí v prachu země, procítí, jedni k životu věčnému, druzí pak ku pohanění a ku potupě věčné.
3 Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
Ale ti, kteříž jiné vyučují, stkvíti se budou jako blesk oblohy, a kteříž k spravedlnosti přivozují mnohé, jako hvězdy na věčné věky.
4 Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
Ty pak Danieli, zavři slova tato, a zapečeť knihu tuto až do času jistého. Mnozíť budou pilně zpytovati, a rozmnoženo bude umění.
5 Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
Zatím viděl jsem já Daniel, a aj, jiní dva stáli, jeden z této strany břehu řeky, a druhý z druhé strany břehu též řeky.
6 Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
A řekl muži tomu oblečenému v roucho lněné, kterýž stál nad vodou té řeky: Když bude konec těm divným věcem?
7 Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
I slyšel jsem muže toho oblečeného v roucho lněné, kterýž stál nad vodou té řeky, an zdvihl pravici svou i levici svou k nebi, a přisáhl skrze Živého na věky, že po uloženém času, a uložených časích, i půl času, a když do cela rozptýlí násilí lidu svatého, dokonají se všecky tyto věci.
8 Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
A když jsem já slyše, nerozuměl, řekl jsem: Pane můj, jaký konec bude těch věcí?
9 Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
Tedy řekl: Odejdi, Danieli, nebo zavřína jsou a zapečetěna slova ta až do času jistého.
10 Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
Přečišťováni a bíleni a prubováni budou mnozí; bezbožní zajisté bezbožnost páchati budou, aniž co porozumějí kteří z nich, ale moudří porozumějí.
11 “Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
Od toho pak času, v němž odjata bude obět ustavičná, a postavena ohavnost hubící, bude dnů tisíc, dvě stě a devadesát.
12 Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
Blahoslavený, kdož dočeká a přijde ke dnům tisíci, třem stům, třidcíti a pěti.
13 “Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”
Ty pak odejdi k místu svému, a odpočívati budeš, a zůstaneš v losu svém na skonání dnů.

< Danieli 12 >