< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
« Quant à moi, la première année de Darius le Mède, je me suis levé pour le confirmer et le renforcer.
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
« Maintenant, je vais te montrer la vérité. Voici que trois autres rois vont se lever en Perse. Le quatrième sera beaucoup plus riche que tous les autres. Quand il sera devenu fort par ses richesses, il soulèvera tout contre le royaume de Grèce.
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
Un roi puissant se lèvera, qui dominera avec une grande autorité, et fera ce qu'il voudra.
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
Quand il se lèvera, son royaume sera brisé et partagé aux quatre vents du ciel, mais non pas pour sa postérité, ni selon la domination avec laquelle il a régné; car son royaume sera arraché, même pour d'autres que ceux-là.
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
« Le roi du midi sera puissant. L'un de ses princes deviendra plus fort que lui et dominera. Sa domination sera une grande domination.
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
A la fin des années, ils s'uniront; et la fille du roi du midi ira vers le roi du nord pour conclure une alliance, mais elle ne conservera pas la force de son bras. Lui aussi ne tiendra pas, et son bras non plus; mais elle sera livrée, avec ceux qui l'ont amenée, et celui qui l'a engendrée, et celui qui l'a fortifiée en ces temps-là.
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
« Mais d'un rejeton sorti de ses racines se lèvera un homme à sa place, qui ira à l'armée et entrera dans la forteresse du roi du nord; il traitera avec eux et sera vainqueur.
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
Il emmènera aussi en captivité en Égypte leurs dieux, avec leurs images en fonte, et leurs vases d'argent et d'or. Il s'abstiendra quelques années du roi du nord.
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
Il entrera dans le royaume du roi du midi, mais il retournera dans son pays.
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
Ses fils feront la guerre et rassembleront une multitude de grandes forces qui arriveront, déborderont et passeront. Ils reviendront et feront la guerre, jusqu'à sa forteresse.
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
« Le roi du Midi sera irrité et sortira pour le combattre, même le roi du Nord. Il enverra une grande multitude, et la multitude sera livrée entre ses mains.
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
La multitude sera emportée, et son cœur s'élèvera. Il renversera des dizaines de milliers, mais il ne vaincra pas.
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
Le roi du nord reviendra, et il enverra une multitude plus nombreuse que la précédente. Il arrivera à la fin des temps, des années, avec une grande armée et des provisions abondantes.
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
« En ces temps-là, beaucoup se dresseront contre le roi du Midi. Les enfants des violents parmi ton peuple se lèveront aussi pour établir la vision, mais ils tomberont.
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
Alors le roi du nord viendra, il élèvera un monticule et prendra une ville bien fortifiée. Les forces du sud ne tiendront pas, ni ses troupes choisies, et il n'y aura pas de force pour tenir.
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
Mais celui qui viendra contre lui agira selon sa propre volonté, et personne ne tiendra devant lui. Il se tiendra dans le pays de la gloire, et la destruction sera dans sa main.
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
Il se préparera à venir avec la force de tout son royaume, et avec lui des conditions équitables. Il les exécutera. Il lui donnera la fille des femmes, pour détruire le royaume, mais elle ne tiendra pas, et ne sera pas pour lui.
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
Après cela, il tournera sa face vers les îles, et il en prendra beaucoup, mais un prince fera cesser l'opprobre qui lui est fait. Oui, bien plus, il fera en sorte que l'opprobre se retourne contre lui.
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
Puis il tournera sa face vers les forteresses de son pays; mais il trébuchera et tombera, et on ne le retrouvera pas.
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
« Alors se dressera à sa place celui qui fera passer un collecteur d'impôts dans le royaume pour en maintenir la gloire; mais en peu de jours il sera détruit, non par la colère, ni par la bataille.
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
« A sa place se lèvera un homme méprisable, à qui on n'avait pas donné l'honneur du royaume; mais il viendra au temps de la sécurité, et il obtiendra le royaume par des flatteries.
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
Les forces écrasantes seront submergées devant lui, et seront brisées. Oui, aussi le prince de l'alliance.
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
Après le traité conclu avec lui, il agira avec ruse; car il s'élèvera et deviendra fort avec peu de gens.
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
Au temps de la sécurité, il s'attaquera même aux lieux les plus gras de la province. Il fera ce que ses pères n'ont pas fait, ni les pères de ses pères. Il répandra parmi eux la proie, le pillage et la richesse. Oui, il élaborera ses plans contre les forteresses, mais seulement pour un temps.
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
« Il excitera sa puissance et son courage contre le roi du Midi avec une grande armée; et le roi du Midi livrera bataille avec une armée extrêmement grande et puissante, mais il ne tiendra pas, car on ourdira des plans contre lui.
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
Oui, ceux qui mangeront de ses mets le détruiront, et son armée sera balayée. Beaucoup tomberont tués.
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
Quant à ces deux rois, leur cœur sera porté à faire le mal, et ils diront des mensonges à une table; mais cela ne réussira pas, car la fin sera toujours au temps fixé.
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
Puis il retournera dans son pays avec de grandes richesses. Son cœur sera contre l'alliance sainte. Il agira, et retournera dans son pays.
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
« Il reviendra au temps fixé et entrera dans le Midi; mais ce ne sera pas au dernier temps comme au premier.
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
Car des navires de Kittim viendront contre lui. C'est pourquoi il sera affligé, et il reviendra, et il s'indignera contre l'alliance sainte, et il agira. Il reviendra même, et aura égard à ceux qui abandonnent l'alliance sainte.
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
« Des forces de sa part profaneront le sanctuaire, la forteresse, et feront disparaître l'holocauste perpétuel. Puis ils dresseront l'abomination qui désole.
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
Il corrompra par des flatteries les méchants de l'alliance, mais le peuple qui connaît son Dieu sera fort et agira.
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
« Les sages parmi le peuple en instruiront beaucoup; mais ils tomberont par l'épée et par la flamme, par la captivité et par le pillage, pendant plusieurs jours.
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
Lorsqu'ils tomberont, on leur portera un petit secours; mais beaucoup se joindront à eux par des flatteries.
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
Quelques-uns des sages tomberont pour les affiner, pour les purifier, pour les blanchir, jusqu'au temps de la fin, car c'est encore pour le temps fixé.
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
« Le roi fera ce qu'il voudra. Il s'élèvera et se glorifiera au-dessus de tout dieu, et il dira des choses merveilleuses contre le Dieu des dieux. Il prospérera jusqu'à l'accomplissement de l'indignation, car ce qui est déterminé s'accomplira.
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
Il ne tiendra pas compte des dieux de ses pères, ni du désir des femmes, ni d'aucun dieu, car il s'élèvera au-dessus de tous.
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
Mais à leur place, il honorera le dieu des forteresses. Il honorera un dieu que ses pères n'ont pas connu, avec de l'or, de l'argent, des pierres précieuses et des choses agréables.
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
Il vaincra les forteresses les plus puissantes avec l'aide d'un dieu étranger. Il accroîtra la gloire de ceux qui le reconnaîtront. Il les fera dominer sur beaucoup de gens, et il partagera le pays à prix d'argent.
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
« Au temps de la fin, le roi du midi lui fera la guerre, et le roi du nord viendra contre lui comme un tourbillon, avec des chars, des cavaliers et de nombreux navires. Il entrera dans les pays, il les débordera et les traversera.
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
Il entrera aussi dans le pays de la gloire, et beaucoup de pays seront renversés; mais ceux-ci seront délivrés de sa main: Édom, Moab, et le chef des enfants d'Ammon.
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
Il étendra aussi sa main sur les pays. Le pays d'Égypte n'échappera pas.
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
Mais il aura le pouvoir sur les trésors d'or et d'argent, et sur tous les objets précieux de l'Égypte. Les Libyens et les Éthiopiens suivront ses traces.
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
Mais des nouvelles de l'Orient et du Nord le troubleront, et il sortira avec une grande fureur pour détruire et exterminer beaucoup de gens.
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
Il plantera les tentes de son palais entre la mer et la glorieuse montagne sainte; mais il arrivera à sa perte, et personne ne lui viendra en aide.

< Danieli 11 >