< Danieli 11 >

1 Nami katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Dario Mmedi, nilisimama kumsaidia na kumlinda.)
and I in/on/with year one to/for Darius [the] Mede to stand: stand my to/for to strengthen: strengthen and to/for security to/for him
2 “Sasa basi, ninakuambia kweli: Wafalme watatu zaidi watatokea Uajemi, kisha atatokea mfalme wa nne, ambaye atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote. Wakati atakapokuwa amekwisha kujipatia nguvu kwa utajiri wake, atamchochea kila mmoja dhidi ya ufalme wa Uyunani.
and now truth: true to tell to/for you behold still three king to stand: rise to/for Persia and [the] fourth to enrich riches great: large from all and like/as strength his in/on/with riches his to rouse [the] all [obj] royalty Greece
3 Ndipo mfalme mwenye nguvu atatokea, ambaye atatawala kwa nguvu nyingi na kufanya anavyopenda.
and to stand: rise king mighty man and to rule dominion many and to make: do like/as acceptance his
4 Baada ya kujitokeza, milki yake itavunjwa na kugawanyika katika pande nne za mbinguni. Hautakwenda kwa wazao wake, wala hautakuwa na nguvu alizotumia, kwa sababu milki yake itangʼolewa na kupewa wengine.
and like/as to stand: rise he to break royalty his and to divide to/for four spirit: breath [the] heaven and not to/for end his and not like/as dominion his which to rule for to uproot royalty his and to/for another from to/for alone: besides these
5 “Mfalme wa Kusini atakuwa na nguvu, lakini mmoja wa majemadari wake atakuwa na nguvu zaidi kuliko mfalme, naye atatawala ufalme wake mwenyewe kwa nguvu nyingi.
and to strengthen: strengthen king [the] south and from ruler his and to strengthen: strengthen upon him and to rule dominion many dominion his
6 Baada ya miaka kadha, wataungana. Binti wa mfalme wa Kusini ataolewa kwa mfalme wa Kaskazini ili kuimarisha mapatano, lakini huyo binti nguvu zake hazitadumu; hata mfalme hatadumu wala nguvu zake. Katika siku hizo atafukuzwa, pamoja na hao wasindikizaji wake wa kifalme, watoto wake, na yeyote aliyemuunga mkono.
and to/for end year to unite and daughter king [the] south to come (in): come to(wards) king [the] north to/for to make uprightness and not to restrain strength [the] arm and not to stand: stand and arm his and to give: give he/she/it and to come (in): come her and [the] to beget her and to strengthen: strengthen her in/on/with time
7 “Mmoja kutoka jamaa ya huyo binti atainuka na kuchukua nafasi yake. Atashambulia majeshi ya mfalme wa Kaskazini na kuingia katika ngome yake; atapigana dhidi yao naye atashinda.
and to stand: rise from branch root her stand his and to come (in): come to(wards) [the] strength: soldiers and to come (in): come in/on/with security king [the] north and to make: do in/on/with them and to strengthen: prevail over
8 Tena ataitwaa miungu yao, vinyago vyao vya chuma, na vitu vyao vya thamani vya fedha na dhahabu, na kuvichukua hadi Misri. Kwa miaka kadha atamwacha mfalme wa Kaskazini bila kumsumbua.
and also God their with libation their with article/utensil desire their silver: money and gold in/on/with captivity to come (in): bring Egypt and he/she/it year to stand: stand from king [the] north
9 Kisha mfalme wa Kaskazini atashambulia nchi ya mfalme wa Kusini, lakini atarudi nyuma hadi kwenye nchi yake.
and to come (in): come in/on/with royalty king [the] south and to return: return to(wards) land: soil his
10 Wana wa mfalme wa Kaskazini watajiandaa kwa vita na kukusanya jeshi kubwa, ambalo litafagia nchi kama mafuriko yasiyozuilika na kuendelea na vita hadi kwenye ngome ya mfalme wa Kusini.
(and son: child his *Q(K)*) to stir up and to gather crowd strength: soldiers many and to come (in): come to come (in): come and to overflow and to pass and to return: again (and to stir up *Q(K)*) till (security his *Q(K)*)
11 “Kisha mfalme wa Kusini atatoka kwa ghadhabu na kupigana dhidi ya mfalme wa Kaskazini, ambaye ataunda jeshi kubwa, lakini litashindwa.
and to provoke king [the] south and to come out: come and to fight with him with king [the] north and to stand: rise crowd many and to give: give [the] crowd in/on/with hand: power his
12 Wakati jeshi litakapokuwa limechukuliwa, mfalme wa Kusini atajawa na kiburi na atachinja maelfu mengi, hata hivyo hatabaki na ushindi.
and to lift: raise [the] crowd (and to exalt *Q(K)*) heart his and to fall: fall ten thousand and not be strong
13 Kwa maana mfalme wa Kaskazini atakusanya jeshi jingine kubwa kuliko lile la kwanza; na baada ya miaka kadha, atasonga mbele na jeshi kubwa mno lililoandaliwa vizuri.
and to return: again king [the] north and to stand: rise crowd many from [the] first and to/for end [the] time year to come (in): come to come (in): come in/on/with strength: soldiers great: large and in/on/with property many
14 “Katika nyakati hizo wengi watainuka dhidi ya mfalme wa Kusini. Watu wenye ghasia miongoni mwa watu wako mwenyewe wataasi ili kutimiza maono, lakini bila mafanikio.
and in/on/with time [the] they(masc.) many to stand: rise upon king [the] south and son: type of violent people your to lift: raise to/for to stand: stand vision and to stumble
15 Ndipo mfalme wa Kaskazini atakuja na kuuzunguka mji kwa majeshi, na kuuteka mji wa ngome. Majeshi ya Kusini yatakosa nguvu za kuyazuia; naam, hata vikosi vyao vya askari vilivyo bora zaidi, havitakuwa na nguvu ya kuwakabili.
and to come (in): come king [the] north and to pour: build siege mound mound and to capture city fortification and arm [the] south not to stand: stand and people: soldiers best his and nothing strength to/for to stand: stand
16 Huyo mvamia nchi atafanya apendavyo; hakuna yeyote atakayeweza kumpinga. Atajiimarisha katika Nchi ya Kupendeza, na atakuwa na uwezo wa kuiangamiza.
and to make: do [the] to come (in): come to(wards) him like/as acceptance his and nothing to stand: stand to/for face: before his and to stand: stand in/on/with land: country/planet [the] beauty and consumption in/on/with hand: power his
17 Ataamua kuja na nguvu za ufalme wake wote na kufanya mapatano ya amani na mfalme wa Kusini. Naye atamtoa binti yake aolewe naye ili kuuangusha ufalme, lakini mipango yake haitafanikiwa wala kumsaidia.
and to set: make face his to/for to come (in): come in/on/with power all royalty his and upright with him and to make: do and daughter [the] woman to give: give(marriage) to/for him to/for to ruin her and not to stand: stand and not to/for him to be
18 Ndipo atabadili nia yake kupigana na nchi za pwani na ataziteka nyingi, lakini jemadari mmoja atakomesha ufidhuli wake na kurudisha ufidhuli wake juu yake.
(and to set: put *Q(K)*) face his to/for coastland and to capture many and to cease chief reproach his to/for him lest reproach his to return: return to/for him
19 Baada ya hili atazigeukia ngome za nchi yake mwenyewe, lakini atajikwaa na kuanguka, wala hataonekana tena.
and to return: return face his to/for security land: country/planet his and to stumble and to fall: kill and not to find
20 “Atakayetawala baada yake atamtuma mtoza ushuru ili kudumisha fahari ya kifalme. Hata hivyo, baada ya miaka michache ataangamizwa, lakini si katika hasira wala katika vita.
and to stand: rise upon stand his to pass to oppress glory royalty and in/on/with day one to break and not in/on/with face: anger and not in/on/with battle
21 “Atakayetawala baada yake atakuwa mtu wa kudharauliwa ambaye hajapewa heshima ya kifalme. Atauvamia ufalme wakati watu wake wanapojiona wako salama, naye atautwaa kwa hila.
and to stand: rise upon stand his to despise and not to give: give upon him splendor royalty and to come (in): come in/on/with ease and to strengthen: prevail over royalty in/on/with smoothness
22 Ndipo jeshi kubwa litafagiliwa mbele yake; jeshi pamoja na mkuu mmoja wa agano wataangamizwa.
and arm [the] flood to overflow from to/for face: before his and to break and also leader covenant
23 Baada ya kufanya mapatano naye, atatenda kwa udanganyifu, na akitumia watu wachache tu ataingia madarakani.
and from to unite to(wards) him to make: do deceit and to ascend: rise and be vast in/on/with little nation
24 Wakati majimbo yaliyo tajiri sana yanajiona salama, atayavamia, naye atafanikisha kile ambacho baba zake wala babu zake hawakuweza. Atagawa nyara, mateka na utajiri miongoni mwa wafuasi wake. Atafanya hila ya kupindua miji yenye maboma, lakini kwa muda mfupi tu.
in/on/with ease and in/on/with fatness province to come (in): come and to make: do which not to make: do father his and father father his plunder and spoil and property to/for them to scatter and upon fortification to devise: devise plot his and till time
25 “Pamoja na jeshi kubwa atachochea nguvu zake na ushujaa wake dhidi ya mfalme wa Kusini. Mfalme wa Kusini atafanya vita na jeshi lenye nguvu sana, lakini hataweza kusimama kwa sababu ya kwa hila zilizofanywa dhidi yake.
and to rouse strength his and heart his upon king [the] south in/on/with strength: soldiers great: large and king [the] south to stir up to/for battle in/on/with strength: soldiers great: large and mighty till much and not to stand: stand for to devise: devise upon him plot
26 Wale wanaokula kutoka kwenye ruzuku za mfalme watajaribu kumwangamiza; jeshi lake litafagiliwa mbali, nao wengi watakufa vitani.
and to eat choice choice his to break him and strength: soldiers his to overflow and to fall: kill slain: killed many
27 Wafalme hawa wawili, mioyo yao ikiwa imekusudia mabaya, wataketi kwenye meza moja na kudanganyana wao kwa wao, lakini pasipo faida, kwa sababu bado mwisho utakuja katika wakati ulioamriwa.
and two their [the] king heart their to/for mischief and upon table one lie to speak: speak and not to prosper for still end to/for meeting: time appointed
28 Mfalme wa Kaskazini atarudi katika nchi yake na utajiri mwingi, lakini atakuwa ameukaza moyo wake kinyume na agano takatifu. Atachukua hatua dhidi ya hilo agano, kisha atarudi nchi yake.
and to return: return land: country/planet his in/on/with property great: large and heart his upon covenant holiness and to make: do and to return: return to/for land: country/planet his
29 “Wakati ulioamriwa, atavamia tena Kusini, lakini wakati huu matokeo yake yatakuwa tofauti na yale ya wakati wa kwanza.
to/for meeting: time appointed to return: return and to come (in): come in/on/with south and not to be like/as first: previous and like/as last
30 Meli za nchi ya Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atarudi nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha fadhili kwa wale waliachao agano takatifu.
and to come (in): come in/on/with him ship Cyprus and be disheartened and to return: return and be indignant upon covenant holiness and to make: [do] and to return: return and to understand upon to leave: forsake covenant holiness
31 “Majeshi yake yenye silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya Hekalu, na kuondolea mbali sadaka ya kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu lisababishalo ukiwa.
and arm from him to stand: rise and to profane/begin: profane [the] sanctuary [the] security and to turn aside: remove [the] continually and to give: put [the] abomination be desolate: destroyed
32 Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano, lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti.
and be wicked covenant to pollute in/on/with flattery and people to know God his to strengthen: persevere and to make: do
33 “Wenye hekima watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto, au kukamatwa au kufanywa mateka.
and be prudent people to understand to/for many and to stumble in/on/with sword and in/on/with flame in/on/with captivity and in/on/with plunder day
34 Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi ambao si waaminifu wataungana nao.
and in/on/with to stumble they to help helper little and to join upon them many in/on/with smoothness
35 Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho, kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamriwa.
and from [the] be prudent to stumble to/for to refine in/on/with them and to/for to purify and to/for to whiten till time end for still to/for meeting: time appointed
36 “Mfalme atafanya apendavyo. Atajikweza na kujitukuza juu ya kila mungu, naye atasema mambo ambayo hayajasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu. Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa lazima kitokee.
and to make: do like/as acceptance his [the] king and to exalt and to magnify upon all god and upon God god to speak: speak to wonder and to prosper till to end: expend indignation for to decide to make: do
37 Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu yeyote, bali atajikweza mwenyewe juu yao wote.
and upon God father his not to understand and upon desire woman and upon all god not to understand for upon all to magnify
38 Badala ya kuwajali miungu, ataheshimu mungu wa ngome; mungu ambaye hakujulikana na baba zake ndiye atamheshimu kwa dhahabu na fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa.
and to/for god security upon stand his to honor: honour and to/for god which not to know him father his to honor: honour in/on/with gold and in/on/with silver: money and in/on/with stone precious and in/on/with precious thing
39 Atashambulia ngome zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi, na atagawa nchi kwa gharama.
and to make: do to/for fortification security with god foreign which (to recognize *Q(K)*) to multiply glory and to rule them in/on/with many and land: soil to divide in/on/with price
40 “Katika wakati wa mwisho, mfalme wa Kusini atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita, askari wapanda farasi, na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na kuzikumba nchi hizo kama mafuriko.
and in/on/with time end to gore with him king [the] south and to storm upon him king [the] north in/on/with chariot and in/on/with horseman and in/on/with fleet many and to come (in): come in/on/with land: country/planet and to overflow and to pass
41 Pia ataivamia Nchi ya Kupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka mkono wake.
and to come (in): come in/on/with land: country/planet [the] beauty and many to stumble and these to escape from hand: power his Edom and Moab and first: best son: descendant/people Ammon
42 Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi; hata Misri haitaepuka.
and to send: reach hand: power his in/on/with land: country/planet and land: country/planet Egypt not to be to/for survivor
43 Atamiliki hazina za dhahabu, fedha na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha.
and to rule in/on/with hidden [the] gold and [the] silver: money and in/on/with all precious thing Egypt and Libyan and Ethiopian in/on/with step his
44 Lakini taarifa kutoka mashariki na kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na kuharibu kabisa wengi.
and tidings to dismay him from east and from north and to come out: come in/on/with rage great: large to/for to destroy and to/for to devote/destroy many
45 Atasimika hema zake za ufalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna yeyote atakayemsaidia.
and to plant tent palace his between sea to/for mountain: mount beauty holiness and to come (in): come till end his and nothing to help to/for him

< Danieli 11 >