< Danieli 10 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, Danieli (ambaye aliitwa Belteshaza) alipewa ufunuo. Ujumbe wake ulikuwa kweli, nao ulihusu vita vikubwa. Ufahamu wa ujumbe ulimjia katika maono.
No terceiro ano de Ciro, rei da Pérsia, uma mensagem foi revelada a Daniel, cujo nome era Belteshazzar; e a mensagem era verdadeira, até mesmo uma grande guerra. Ele compreendeu a mensagem, e teve compreensão da visão.
2 Wakati huo, mimi Danieli nikaomboleza kwa majuma matatu.
Naqueles dias eu, Daniel, estava de luto por três semanas inteiras.
3 Sikula chakula kizuri; nyama wala divai havikugusa midomo yangu; nami sikujipaka mafuta kamwe mpaka majuma matatu yalipotimia.
Eu não comi nenhuma comida agradável. Nenhuma carne ou vinho entrava em minha boca. Eu não me ungi, até que três semanas inteiras foram cumpridas.
4 Kwenye siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa nimesimama kwenye ukingo wa mto mkubwa Hidekeli,
No vigésimo quarto dia do primeiro mês, quando estava à beira do grande rio, que é Hiddekel,
5 nikatazama juu, na mbele yangu alikuwepo mtu aliyevaa mavazi ya kitani na mshipi wa dhahabu safi kutoka ufazi kiunoni mwake.
levantei os olhos e olhei, e eis que estava um homem vestido de linho, cuja cintura estava enfeitada com ouro puro de Uphaz.
6 Mwili wake ulikuwa kama kito cha zabarajadi safi, uso wake kama umeme wa radi, macho yake kama mwali wa moto, mikono yake na miguu yake kama mngʼao wa shaba iliyosuguliwa sana, nayo sauti yake kama ya umati mkubwa wa watu.
Seu corpo também era como o berilo, e seu rosto como a aparência de um raio, e seus olhos como tochas flamejantes. Seus braços e seus pés eram como bronze polido. A voz de suas palavras era como a voz de uma multidão.
7 Mimi Danieli, ni mimi peke yangu niliyeona hayo maono; watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini waligubikwa na hofu kuu, hata wakakimbia na kujificha.
Eu, Daniel, sozinho vi a visão, pois os homens que estavam comigo não viram a visão, mas um grande tremor caiu sobre eles, e eles fugiram para se esconder.
8 Kwa hiyo niliachwa peke yangu, nikikodolea macho maono hayo makubwa; sikubakiwa na nguvu, na rangi ya uso wangu ikabadilika kama aliyekufa, nikakosa nguvu.
Então eu fiquei sozinho e vi esta grande visão. Nenhuma força ficou em mim; pois meu rosto ficou pálido e eu não retive nenhuma força.
9 Kisha nikamsikia akisema, nami nilipokuwa nikimsikiliza, nikalala kifudifudi, nikapatwa na usingizi mzito.
Ainda assim, ouvi a voz de suas palavras. Quando ouvi a voz de suas palavras, então caí num sono profundo em meu rosto, com meu rosto voltado para o chão.
10 Mkono ulinigusa, ukaninyanyua, na kuniweka nikipiga magoti na mikono yangu ikashika chini, huku nikiwa bado ninatetemeka.
Eis que uma mão me tocou, que me pôs de joelhos e nas palmas das minhas mãos.
11 Akasema, “Danieli, wewe mtu upendwaye sana, fikiri kwa makini maneno ninayokwenda kunena nawe sasa; simama wima, kwa maana sasa nimetumwa kwako.” Naye aliponiambia haya, nikasimama nikitetemeka.
Ele me disse: “Daniel, tu, homem muito amado, entende as palavras que te falo, e fica de pé, pois fui enviado a ti, agora”. Quando ele me disse esta palavra, eu fiquei tremendo.
12 Ndipo akaendelea kusema, “Danieli, usiogope. Tangu siku ya kwanza ulipotia moyo wako ili kupata ufahamu na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wako, maneno yako yalisikiwa, nami nimekuja ili kujibu maneno yako.
Então ele me disse: “Não tenha medo, Daniel; pois desde o primeiro dia em que você colocou seu coração para entender, e para se humilhar diante de seu Deus, suas palavras foram ouvidas. Eu vim pelo bem de suas palavras.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga kwa siku ishirini na moja. Ndipo Mikaeli, mmoja wa malaika wakuu, alikuja kunisaidia, kwa sababu nilikuwa nimezuiliwa huko na mfalme wa Uajemi.
Mas o príncipe do reino da Pérsia me resistiu vinte e um dias; mas, eis que Miguel, um dos príncipes principais, veio para me ajudar porque eu permaneci lá com os reis da Pérsia.
14 Sasa nimekuja kukuelezea mambo yatakayowatokea watu wako wakati ujao, kwa maana maono hayo yanahusu wakati ambao haujaja bado.”
Agora vim para fazer-vos compreender o que acontecerá ao vosso povo nos últimos dias, pois a visão ainda é por muitos dias”.
15 Alipokuwa akinielezea haya, nilisujudu uso wangu ukiwa umeelekea chini, nikawa bubu.
Quando ele me disse estas palavras, eu coloquei meu rosto no chão e fiquei mudo.
16 Ndipo mmoja aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa midomo yangu, nami nikafungua kinywa changu, nikaanza kunena. Nikamwambia yule aliyesimama mbele yangu, “Nimepatwa na huzuni kubwa kwa sababu ya maono haya, bwana wangu, nami nimeishiwa nguvu.
Eis que um, à semelhança dos filhos dos homens, tocou meus lábios. Então abri minha boca, e falei e disse àquele que estava diante de mim: “Meu senhor, por causa da visão, minhas tristezas me ultrapassaram, e eu não retenho forças.
17 Bwana wangu, mimi mtumishi wako nitawezaje kuzungumza na wewe? Nguvu zangu zimeniishia hata ninashindwa kupumua.”
Pois como pode o servo deste meu senhor falar com este meu senhor? Pois quanto a mim, imediatamente não restou força em mim. Não restava fôlego em mim”.
18 Tena yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa na kunitia nguvu.
Então uma pessoa como um homem me tocou novamente, e ele me fortaleceu.
19 Akasema, “Ee mtu upendwaye sana, usiogope. Amani iwe kwako! Uwe na nguvu sasa; jipe nguvu.” Alipozungumza nami, nilipata nguvu, nikasema, “Nena, bwana wangu, kwa kuwa umenipa nguvu.”
Ele disse: “Grande homem amado, não tenha medo”. Que a paz esteja com você”. Seja forte. Sim, sê forte”. Quando ele falou comigo, eu me fortaleci e disse: “Deixe o meu senhor falar, pois o senhor me fortaleceu”.
20 Kwa hiyo akasema, “Je, unajua kwa nini nimekujia? Sasa hivi nitarudi kupigana dhidi ya mkuu wa Uajemi, nami nikienda, mkuu wa Uyunani atakuja.
Então ele disse: “Você sabe por que eu vim até você? Agora vou voltar para lutar com o príncipe da Pérsia. Quando eu sair, eis que o príncipe da Grécia virá.
21 Lakini kwanza nitakuambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Kweli. (Hakuna hata mmoja anayenisaidia dhidi yao isipokuwa Mikaeli, mkuu wenu.
Mas eu lhe direi o que está inscrito na escrita da verdade. Não há ninguém que me oponha a estes, a não ser Miguel, seu príncipe.

< Danieli 10 >