< Danieli 10 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, Danieli (ambaye aliitwa Belteshaza) alipewa ufunuo. Ujumbe wake ulikuwa kweli, nao ulihusu vita vikubwa. Ufahamu wa ujumbe ulimjia katika maono.
En la troisième année du règne de Cyrus, roi des Perses, une parole fut révélée à Daniel, que l'on nommait Baltasar. Et cette parole était véritable, et une grande force et une grande intelligence lui furent données en cette vision.
2 Wakati huo, mimi Danieli nikaomboleza kwa majuma matatu.
En ces jours-là, moi, Daniel, je fus pleurant durant trois semaines.
3 Sikula chakula kizuri; nyama wala divai havikugusa midomo yangu; nami sikujipaka mafuta kamwe mpaka majuma matatu yalipotimia.
Je ne mangeai point de pain agréable au goût; ni chair ni vin n'entrèrent dans ma bouche, et je n'usai d'aucun parfum, jusqu'à ce que les trois semaines fussent accomplies.
4 Kwenye siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa nimesimama kwenye ukingo wa mto mkubwa Hidekeli,
Le vingt-quatrième jour du premier mois, j'étais sur les bords du grand fleuve que l'on appelle le Tigre.
5 nikatazama juu, na mbele yangu alikuwepo mtu aliyevaa mavazi ya kitani na mshipi wa dhahabu safi kutoka ufazi kiunoni mwake.
Et je levai les yeux, et je regardai; et voilà qu'il y avait un homme vêtu de lin, et ses reins étaient ceints d'or d'Ophaz;
6 Mwili wake ulikuwa kama kito cha zabarajadi safi, uso wake kama umeme wa radi, macho yake kama mwali wa moto, mikono yake na miguu yake kama mngʼao wa shaba iliyosuguliwa sana, nayo sauti yake kama ya umati mkubwa wa watu.
Et son corps était comme Tharsis, et son front avait l'aspect d'un éclair; et ses yeux étaient comme des lampes de feu; ses bras et ses jambes avaient l'aspect de l'airain resplendissant; et sa voix, quand il parlait, était comme la voix d'une multitude.
7 Mimi Danieli, ni mimi peke yangu niliyeona hayo maono; watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini waligubikwa na hofu kuu, hata wakakimbia na kujificha.
Et moi, Daniel, j'eus seul cette vision, et les hommes qui étaient avec moi ne la virent point; mais un grand trouble les saisit, et ils s'enfuirent de terreur.
8 Kwa hiyo niliachwa peke yangu, nikikodolea macho maono hayo makubwa; sikubakiwa na nguvu, na rangi ya uso wangu ikabadilika kama aliyekufa, nikakosa nguvu.
Et moi je restai seul, et j'eus cette grande vision; et mes forces m'abandonnèrent, et la gloire de mon visage en fut altérée, et je ne pus recouvrer ma force.
9 Kisha nikamsikia akisema, nami nilipokuwa nikimsikiliza, nikalala kifudifudi, nikapatwa na usingizi mzito.
Et j'entendis retentir ces paroles; et, en les entendant, j'étais plein d'épouvante, et j'avais la face contre terre.
10 Mkono ulinigusa, ukaninyanyua, na kuniweka nikipiga magoti na mikono yangu ikashika chini, huku nikiwa bado ninatetemeka.
Et voilà qu'une main me toucha, et me releva sur mes genoux.
11 Akasema, “Danieli, wewe mtu upendwaye sana, fikiri kwa makini maneno ninayokwenda kunena nawe sasa; simama wima, kwa maana sasa nimetumwa kwako.” Naye aliponiambia haya, nikasimama nikitetemeka.
Et il me dit: Daniel, homme des désirs, comprends les paroles que je te dis, et tiens-toi debout; car je suis envoyé vers toi; et pendant qu'Il me dit ces mots je me relevai tremblant.
12 Ndipo akaendelea kusema, “Danieli, usiogope. Tangu siku ya kwanza ulipotia moyo wako ili kupata ufahamu na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wako, maneno yako yalisikiwa, nami nimekuja ili kujibu maneno yako.
Et il me dit: N'aie point peur, Daniel; car du premier jour où tu as appliqué ton cœur à converser avec le Seigneur ton Dieu, et à t'affliger devant lui, tes prières ont été entendues, et je suis venu à tes prières.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga kwa siku ishirini na moja. Ndipo Mikaeli, mmoja wa malaika wakuu, alikuja kunisaidia, kwa sababu nilikuwa nimezuiliwa huko na mfalme wa Uajemi.
Or le prince du royaume des Perses m'a résisté vingt et un jours, et Michel, l'un des archanges, est venu à mon aide, et je l'ai laissé au lieu où j'étais, avec le prince du royaume des Perses.
14 Sasa nimekuja kukuelezea mambo yatakayowatokea watu wako wakati ujao, kwa maana maono hayo yanahusu wakati ambao haujaja bado.”
Et je suis venu t'enseigner les choses qui adviendront à ton peuple dans les derniers jours; car cette vision est pour bien des jours encore.
15 Alipokuwa akinielezea haya, nilisujudu uso wangu ukiwa umeelekea chini, nikawa bubu.
Et pendant qu'il me dit ces paroles, je retombai la face contre terre, et je fus rempli d'épouvante.
16 Ndipo mmoja aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa midomo yangu, nami nikafungua kinywa changu, nikaanza kunena. Nikamwambia yule aliyesimama mbele yangu, “Nimepatwa na huzuni kubwa kwa sababu ya maono haya, bwana wangu, nami nimeishiwa nguvu.
Et voilà qu'une image du fils de l'homme me toucha les lèvres, et j'ouvris la bouche, et je parlai; et je dis à celui qui se tenait devant moi: Seigneur, à votre vue mes entrailles ont été émues, et j'ai perdu ma force.
17 Bwana wangu, mimi mtumishi wako nitawezaje kuzungumza na wewe? Nguvu zangu zimeniishia hata ninashindwa kupumua.”
Et comment, ô Seigneur, votre serviteur pourra-t-il s'entretenir avec vous, mon seigneur? Je ne puis plus recouvrer aucune force, et il n'est plus de souffle en moi.
18 Tena yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa na kunitia nguvu.
Et celui qui avait l'apparence d'un homme s'approcha, me toucha de nouveau et me raffermit.
19 Akasema, “Ee mtu upendwaye sana, usiogope. Amani iwe kwako! Uwe na nguvu sasa; jipe nguvu.” Alipozungumza nami, nilipata nguvu, nikasema, “Nena, bwana wangu, kwa kuwa umenipa nguvu.”
Et il me dit: N'aie point peur, homme des désirs; la paix soit avec toi; sois homme et sois fort. Et pendant qu'il me dit ces mots je me fortifiai, et je dis: Parlez-moi, seigneur, car vous m'avez fortifié.
20 Kwa hiyo akasema, “Je, unajua kwa nini nimekujia? Sasa hivi nitarudi kupigana dhidi ya mkuu wa Uajemi, nami nikienda, mkuu wa Uyunani atakuja.
Et il me dit: Sais-tu pourquoi je suis venu te trouver? Maintenant je vais retourner combattre le roi des Perses; car comme j'entrais ici, le roi des Hellènes est venu.
21 Lakini kwanza nitakuambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Kweli. (Hakuna hata mmoja anayenisaidia dhidi yao isipokuwa Mikaeli, mkuu wenu.
Or je te dirai ce qui est prescrit en l'Écriture au livre de vérité: Nul ne m'assiste en toutes ces choses, sinon Michel, votre prince.

< Danieli 10 >