< Danieli 10 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, Danieli (ambaye aliitwa Belteshaza) alipewa ufunuo. Ujumbe wake ulikuwa kweli, nao ulihusu vita vikubwa. Ufahamu wa ujumbe ulimjia katika maono.
In the third year of Cyrus king of Persia, a message was revealed to Daniel, who was also called Belteshazzar. This message was true. It was about a great war. Daniel understood the message when he had insight from the vision.
2 Wakati huo, mimi Danieli nikaomboleza kwa majuma matatu.
In those days I, Daniel, was in mourning for three weeks.
3 Sikula chakula kizuri; nyama wala divai havikugusa midomo yangu; nami sikujipaka mafuta kamwe mpaka majuma matatu yalipotimia.
I ate no delicacies, I ate no meat, I drank no wine, and I did not anoint myself with oil until the completion of three entire weeks.
4 Kwenye siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa nimesimama kwenye ukingo wa mto mkubwa Hidekeli,
On the twenty-fourth day of the first month, as I was beside the great river (that is, the Tigris),
5 nikatazama juu, na mbele yangu alikuwepo mtu aliyevaa mavazi ya kitani na mshipi wa dhahabu safi kutoka ufazi kiunoni mwake.
I looked up and saw a man dressed in linen, with a belt around his waist made of pure gold from Uphaz.
6 Mwili wake ulikuwa kama kito cha zabarajadi safi, uso wake kama umeme wa radi, macho yake kama mwali wa moto, mikono yake na miguu yake kama mngʼao wa shaba iliyosuguliwa sana, nayo sauti yake kama ya umati mkubwa wa watu.
His body was like topaz, and his face was like lightning. His eyes were like flaming torches, and his arms and his feet were like polished bronze. The sound of his words was like the sound of a great crowd.
7 Mimi Danieli, ni mimi peke yangu niliyeona hayo maono; watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini waligubikwa na hofu kuu, hata wakakimbia na kujificha.
I, Daniel, alone saw the vision, for the men who were with me did not see the vision. However, a great terror came on them, and they ran away to hide themselves.
8 Kwa hiyo niliachwa peke yangu, nikikodolea macho maono hayo makubwa; sikubakiwa na nguvu, na rangi ya uso wangu ikabadilika kama aliyekufa, nikakosa nguvu.
So I was left alone and saw this great vision. No strength remained in me; my bright appearance was turned into a ruined look, and no strength remained in me.
9 Kisha nikamsikia akisema, nami nilipokuwa nikimsikiliza, nikalala kifudifudi, nikapatwa na usingizi mzito.
Then I heard his words—and as I heard them, I fell on my face in deep sleep with my face to the ground.
10 Mkono ulinigusa, ukaninyanyua, na kuniweka nikipiga magoti na mikono yangu ikashika chini, huku nikiwa bado ninatetemeka.
A hand touched me, and it made me tremble in my knees and the palms of my hands.
11 Akasema, “Danieli, wewe mtu upendwaye sana, fikiri kwa makini maneno ninayokwenda kunena nawe sasa; simama wima, kwa maana sasa nimetumwa kwako.” Naye aliponiambia haya, nikasimama nikitetemeka.
The angel said to me, “Daniel, man greatly treasured, understand the words that I am speaking to you. Stand upright, for I have been sent to you.” When he had spoken this message to me, I stood up trembling.
12 Ndipo akaendelea kusema, “Danieli, usiogope. Tangu siku ya kwanza ulipotia moyo wako ili kupata ufahamu na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wako, maneno yako yalisikiwa, nami nimekuja ili kujibu maneno yako.
Then he said to me, “Do not be afraid, Daniel. Since the first day you set your mind to understand and to humble yourself before your God, your words were heard, and I have come because of your words.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga kwa siku ishirini na moja. Ndipo Mikaeli, mmoja wa malaika wakuu, alikuja kunisaidia, kwa sababu nilikuwa nimezuiliwa huko na mfalme wa Uajemi.
The prince of the kingdom of Persia resisted me, and I was kept there with the kings of Persia for twenty-one days. But Michael, one of the chief princes, came to help me.
14 Sasa nimekuja kukuelezea mambo yatakayowatokea watu wako wakati ujao, kwa maana maono hayo yanahusu wakati ambao haujaja bado.”
Now I have come to help you understand what will happen to your people in the last days. For the vision is for days yet to come.”
15 Alipokuwa akinielezea haya, nilisujudu uso wangu ukiwa umeelekea chini, nikawa bubu.
While he was speaking to me using these words, I turned my face toward the ground and was unable to speak.
16 Ndipo mmoja aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa midomo yangu, nami nikafungua kinywa changu, nikaanza kunena. Nikamwambia yule aliyesimama mbele yangu, “Nimepatwa na huzuni kubwa kwa sababu ya maono haya, bwana wangu, nami nimeishiwa nguvu.
One who was like the sons of man touched my lips, and I opened my mouth and spoke to him who stood before me: “My master, I am in agony because of the vision; I have no strength left.
17 Bwana wangu, mimi mtumishi wako nitawezaje kuzungumza na wewe? Nguvu zangu zimeniishia hata ninashindwa kupumua.”
I am your servant. How can I talk with my master? For I now have no strength, and there is no breath left in me.”
18 Tena yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa na kunitia nguvu.
Again the one with an appearance of a man touched me and strengthened me.
19 Akasema, “Ee mtu upendwaye sana, usiogope. Amani iwe kwako! Uwe na nguvu sasa; jipe nguvu.” Alipozungumza nami, nilipata nguvu, nikasema, “Nena, bwana wangu, kwa kuwa umenipa nguvu.”
He said, “Do not be afraid, man greatly treasured. May peace be to you! Be strong now, be strong!” While he was speaking to me, I was strengthened. I said, “Let my master speak, for you have strengthened me.”
20 Kwa hiyo akasema, “Je, unajua kwa nini nimekujia? Sasa hivi nitarudi kupigana dhidi ya mkuu wa Uajemi, nami nikienda, mkuu wa Uyunani atakuja.
He said, “Do you know why I have come to you? I will soon return to fight against the prince of Persia. When I go, the prince of Greece will come.
21 Lakini kwanza nitakuambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Kweli. (Hakuna hata mmoja anayenisaidia dhidi yao isipokuwa Mikaeli, mkuu wenu.
But I will tell you what is written in the Book of Truth. There is no one who shows himself to be strong with me against them, except Michael your prince.”