< Danieli 10 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, Danieli (ambaye aliitwa Belteshaza) alipewa ufunuo. Ujumbe wake ulikuwa kweli, nao ulihusu vita vikubwa. Ufahamu wa ujumbe ulimjia katika maono.
In year three of Cyrus [the] king of Persia a word it was revealed to Daniel whom it had been called name his Belteshazzar and [was] truth the word and a war great and he understood the word and understanding [belonged] to him by the vision.
2 Wakati huo, mimi Danieli nikaomboleza kwa majuma matatu.
In the days those I Daniel I was mourning three sevens days.
3 Sikula chakula kizuri; nyama wala divai havikugusa midomo yangu; nami sikujipaka mafuta kamwe mpaka majuma matatu yalipotimia.
Food of desirableness not I ate and meat and wine not it came into mouth my and indeed not I anointed myself until were completed three sevens days.
4 Kwenye siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa nimesimama kwenye ukingo wa mto mkubwa Hidekeli,
And on day twenty and four of the month first and I I was on [the] side of the river great that [is] [the] Tigris.
5 nikatazama juu, na mbele yangu alikuwepo mtu aliyevaa mavazi ya kitani na mshipi wa dhahabu safi kutoka ufazi kiunoni mwake.
And I lifted up eyes my and I saw and there! a man one clothed linen and loins his [were] girded with [the] gold of Uphaz.
6 Mwili wake ulikuwa kama kito cha zabarajadi safi, uso wake kama umeme wa radi, macho yake kama mwali wa moto, mikono yake na miguu yake kama mngʼao wa shaba iliyosuguliwa sana, nayo sauti yake kama ya umati mkubwa wa watu.
And body his [was] like topaz and face his [was] like [the] appearance of lightning and eyes his [were] like torches of fire and arms his and feet his [were] like [the] appearance of bronze burnished and [the] sound of words his [was] like [the] sound of a multitude.
7 Mimi Danieli, ni mimi peke yangu niliyeona hayo maono; watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini waligubikwa na hofu kuu, hata wakakimbia na kujificha.
And I saw I Daniel to alone me the vision and the men who they were with me not they saw the vision but terror great it fell on them and they fled in hiding themselves.
8 Kwa hiyo niliachwa peke yangu, nikikodolea macho maono hayo makubwa; sikubakiwa na nguvu, na rangi ya uso wangu ikabadilika kama aliyekufa, nikakosa nguvu.
And I I was left behind to alone me and I saw the vision great this and not it remained in me strength and vigor my it was changed on me into destruction and not I retained strength.
9 Kisha nikamsikia akisema, nami nilipokuwa nikimsikiliza, nikalala kifudifudi, nikapatwa na usingizi mzito.
And I heard [the] sound of words his and just as heard I [the] sound of words his and I I was dazed on face my and face my [was] ground towards.
10 Mkono ulinigusa, ukaninyanyua, na kuniweka nikipiga magoti na mikono yangu ikashika chini, huku nikiwa bado ninatetemeka.
And there! a hand it touched me and it shook me on knees my and [the] palms of hands my.
11 Akasema, “Danieli, wewe mtu upendwaye sana, fikiri kwa makini maneno ninayokwenda kunena nawe sasa; simama wima, kwa maana sasa nimetumwa kwako.” Naye aliponiambia haya, nikasimama nikitetemeka.
And he said to me O Daniel man of preciousness understand the words which I [am] about to speak to you and stand on standing place your for now I have been sent to you and when spoke he with me the word this I stood up trembling.
12 Ndipo akaendelea kusema, “Danieli, usiogope. Tangu siku ya kwanza ulipotia moyo wako ili kupata ufahamu na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wako, maneno yako yalisikiwa, nami nimekuja ili kujibu maneno yako.
And he said to me may not you fear O Daniel for - from the day first which you gave heart your to understand and to humble yourself before God your they were heard words your and I I have come on words your.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga kwa siku ishirini na moja. Ndipo Mikaeli, mmoja wa malaika wakuu, alikuja kunisaidia, kwa sababu nilikuwa nimezuiliwa huko na mfalme wa Uajemi.
And [the] prince of - [the] kingdom of Persia [was] standing to before me twenty and one day[s] and there! Michael one of the princes chief he came to help me and I I remained behind there beside [the] kings of Persia.
14 Sasa nimekuja kukuelezea mambo yatakayowatokea watu wako wakati ujao, kwa maana maono hayo yanahusu wakati ambao haujaja bado.”
And I have come to make understand you [that] which it will happen to people your at [the] end of the days for still [the] vision [is] for the days.
15 Alipokuwa akinielezea haya, nilisujudu uso wangu ukiwa umeelekea chini, nikawa bubu.
And when spoke he with me according to the words these I put face my [the] ground towards and I was dumb.
16 Ndipo mmoja aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa midomo yangu, nami nikafungua kinywa changu, nikaanza kunena. Nikamwambia yule aliyesimama mbele yangu, “Nimepatwa na huzuni kubwa kwa sababu ya maono haya, bwana wangu, nami nimeishiwa nguvu.
And there! like [the] likeness of [the] sons of humankind [was] touching lips my and I opened mouth my and I spoke! and I said! to the [one] standing to before me O lord my on the vision they have turned pangs my on me and not I have retained strength.
17 Bwana wangu, mimi mtumishi wako nitawezaje kuzungumza na wewe? Nguvu zangu zimeniishia hata ninashindwa kupumua.”
And how? is he able [the] servant of lord my this to speak with lord my this and I from now not it remains in me strength and breath not it is left in me.
18 Tena yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa na kunitia nguvu.
And he repeated and he touched me like [the] appearance of humankind and he strengthened me.
19 Akasema, “Ee mtu upendwaye sana, usiogope. Amani iwe kwako! Uwe na nguvu sasa; jipe nguvu.” Alipozungumza nami, nilipata nguvu, nikasema, “Nena, bwana wangu, kwa kuwa umenipa nguvu.”
And he said may not you fear O man of preciousness peace [be] to you be strong and be strong (and when spoke he *L(abh)*) with me I strengthened myself and I said let him speak lord my for you have strengthened me.
20 Kwa hiyo akasema, “Je, unajua kwa nini nimekujia? Sasa hivi nitarudi kupigana dhidi ya mkuu wa Uajemi, nami nikienda, mkuu wa Uyunani atakuja.
And he said ¿ do you know why? have I come to you and now I will return to engage in battle with [the] prince of Persia and I [am] about to go forth and there! [the] prince of Greece he will come.
21 Lakini kwanza nitakuambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Kweli. (Hakuna hata mmoja anayenisaidia dhidi yao isipokuwa Mikaeli, mkuu wenu.
But I will tell to you the [thing] inscribed in writing of truth and there not [is] one [who] shows himself strong with me on these that except Michael prince your.