< Danieli 10 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, Danieli (ambaye aliitwa Belteshaza) alipewa ufunuo. Ujumbe wake ulikuwa kweli, nao ulihusu vita vikubwa. Ufahamu wa ujumbe ulimjia katika maono.
In the third year of Cyrus, king of Persia, a matter, was revealed unto Daniel, whose name was called Belteshazzar; and faithful was the matter, but [concerned] a great warfare, and he marked the word, and had understanding in the revelation.
2 Wakati huo, mimi Danieli nikaomboleza kwa majuma matatu.
In those days, I, Daniel, was mourning three sevens of days:
3 Sikula chakula kizuri; nyama wala divai havikugusa midomo yangu; nami sikujipaka mafuta kamwe mpaka majuma matatu yalipotimia.
food to delight in, did I not eat, neither flesh nor wine, came into my mouth, nor did I so much as, anoint, myself, —until were fulfilled three sevens of days.
4 Kwenye siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa nimesimama kwenye ukingo wa mto mkubwa Hidekeli,
And, on the twenty-fourth day of the first month, —when, I, was by the side of the great river, the same, is Tigris,
5 nikatazama juu, na mbele yangu alikuwepo mtu aliyevaa mavazi ya kitani na mshipi wa dhahabu safi kutoka ufazi kiunoni mwake.
then lifted I up mine eyes, and looked, and lo! a man, clothed in linen, —whose loins, were girded with the bright gold of Uphaz;
6 Mwili wake ulikuwa kama kito cha zabarajadi safi, uso wake kama umeme wa radi, macho yake kama mwali wa moto, mikono yake na miguu yake kama mngʼao wa shaba iliyosuguliwa sana, nayo sauti yake kama ya umati mkubwa wa watu.
whose body, was like Tarshish-stone, and, his face, like the appearance of lightning, and, his eyes, were like torches of fire, and, his arms and his feet, like the look of bronze burnished, —and, the sound of his words, was like the sound of a multitude.
7 Mimi Danieli, ni mimi peke yangu niliyeona hayo maono; watu waliokuwa pamoja nami hawakuyaona, lakini waligubikwa na hofu kuu, hata wakakimbia na kujificha.
And, I, Daniel, alone, beheld the revelation, and, the men who were with me, beheld not the revelation, —in truth, a great terror, had fallen upon them, and they had fled while hiding themselves.
8 Kwa hiyo niliachwa peke yangu, nikikodolea macho maono hayo makubwa; sikubakiwa na nguvu, na rangi ya uso wangu ikabadilika kama aliyekufa, nikakosa nguvu.
I, therefore, was left alone, and beheld this great revelation, and there remained in me no strength, —but, my freshness, was turned upon me into disfigurement, and I retained no strength.
9 Kisha nikamsikia akisema, nami nilipokuwa nikimsikiliza, nikalala kifudifudi, nikapatwa na usingizi mzito.
So then I heard the sound of his words, —and, when I heard the sound of his words, then, I myself, came to be in a deep sleep upon my face, with, my face, to the earth.
10 Mkono ulinigusa, ukaninyanyua, na kuniweka nikipiga magoti na mikono yangu ikashika chini, huku nikiwa bado ninatetemeka.
And lo! a hand, touched me; and roused me up on my knees and the palms of my hands.
11 Akasema, “Danieli, wewe mtu upendwaye sana, fikiri kwa makini maneno ninayokwenda kunena nawe sasa; simama wima, kwa maana sasa nimetumwa kwako.” Naye aliponiambia haya, nikasimama nikitetemeka.
Then said he unto me, O Daniel! man greatly delighted in! have understanding in the words which, I, am about to speak unto thee, and stand up where thou art, for, now, have I been sent unto thee. And, when he had spoken with me this word, I stood up trembling.
12 Ndipo akaendelea kusema, “Danieli, usiogope. Tangu siku ya kwanza ulipotia moyo wako ili kupata ufahamu na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wako, maneno yako yalisikiwa, nami nimekuja ili kujibu maneno yako.
Then said he unto me, Do not fear, Daniel, for, from the first day that thou didst set thy heart to understand and to humble thyself before thy God, thy words were heard; and, I, am come, by reason of thy words.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga kwa siku ishirini na moja. Ndipo Mikaeli, mmoja wa malaika wakuu, alikuja kunisaidia, kwa sababu nilikuwa nimezuiliwa huko na mfalme wa Uajemi.
But, the ruler of the kingdom of Persia, withstood me twenty-one days, but lo! Michael, one of the chief rulers, came in to help me, —and, I, left him there, beside the kings of Persia.
14 Sasa nimekuja kukuelezea mambo yatakayowatokea watu wako wakati ujao, kwa maana maono hayo yanahusu wakati ambao haujaja bado.”
So then I am come to let thee understand that which shall befall thy people in the afterpart of the days, —for yet is the vision for [those] days.
15 Alipokuwa akinielezea haya, nilisujudu uso wangu ukiwa umeelekea chini, nikawa bubu.
And, when he had spoken with me such words as these, —I set my face towards the earth, and was dumb.
16 Ndipo mmoja aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa midomo yangu, nami nikafungua kinywa changu, nikaanza kunena. Nikamwambia yule aliyesimama mbele yangu, “Nimepatwa na huzuni kubwa kwa sababu ya maono haya, bwana wangu, nami nimeishiwa nguvu.
Then lo! like the similitude of the sons of men, one was touching my lips, —so I opened my mouth, and spake, and said unto him who was standing before me, O my lord! By the revelation, my pains have seized me, and I retain no strength.
17 Bwana wangu, mimi mtumishi wako nitawezaje kuzungumza na wewe? Nguvu zangu zimeniishia hata ninashindwa kupumua.”
How then can the servant of this my lord speak with this my lord, —seeing that, as for me—henceforth, there remaineth in me no strength, and no, spirit, is left in me?
18 Tena yule aliyeonekana kama mwanadamu akanigusa na kunitia nguvu.
Then again there touched me one like in appearance to a son of earth, and he strengthened me.
19 Akasema, “Ee mtu upendwaye sana, usiogope. Amani iwe kwako! Uwe na nguvu sasa; jipe nguvu.” Alipozungumza nami, nilipata nguvu, nikasema, “Nena, bwana wangu, kwa kuwa umenipa nguvu.”
And he said, Do not fear, O man greatly delighted in! peace to thee, be strong, yea be strong! And, as he spake with me, I gained strength, and said, Let my lord speak, for thou hast strengthened me.
20 Kwa hiyo akasema, “Je, unajua kwa nini nimekujia? Sasa hivi nitarudi kupigana dhidi ya mkuu wa Uajemi, nami nikienda, mkuu wa Uyunani atakuja.
And he said, Knowest thou wherefore I am come unto thee? But, now, must I return to fight with the ruler of Persia; I, therefore am going forth, and lo! the ruler of Greece, is coming.
21 Lakini kwanza nitakuambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Kweli. (Hakuna hata mmoja anayenisaidia dhidi yao isipokuwa Mikaeli, mkuu wenu.
Howbeit I will tell thee that which is inscribed in the writing of truth, —but there is no one who holdeth strongly with me concerning these things, save Michael your ruler.

< Danieli 10 >