< Danieli 1 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja akazingira Yerusalemu kwa jeshi.
Yahuda Kralı Yehoyakim'in krallığının üçüncü yılında Babil Kralı Nebukadnessar Yeruşalim'in üzerine yürüyüp kenti kuşattı.
2 Bwana akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadneza, pamoja na baadhi ya vyombo kutoka Hekalu la Mungu. Hivi akavichukua hadi kwenye hekalu la mungu wake huko Shinari, naye akaviweka nyumbani ya hazina ya mungu wake.
Rab, Yahuda Kralı Yehoyakim'i ve Tanrı'nın Tapınağı'ndaki bazı eşyaları Nebukadnessar'ın eline teslim etti. Nebukadnessar bunları Şinar ülkesine götürüp kendi ilahının tapınağının hazinesine yerleştirdi.
3 Kisha mfalme akamwagiza Ashpenazi, mkuu wa maafisa wa mfalme, kumletea baadhi ya Waisraeli kutoka jamaa ya mfalme na kutoka jamaa kuu,
Kral İsrailliler arasından kral soyundan gelme ya da soylu bazı gençlerin seçilip saraya getirilmesi için saray görevlilerinin yöneticisi Aşpenaz'a buyruk verdi. Bu gençler kusursuz, yakışıklı, her konuda bilge, bilgili, öğrenmeye yetenekli, sarayda görev almaya uygun nitelikte kişiler olmalıydı. Aşpenaz onlara Kildaniler'in dilini ve yazısını öğretecekti.
4 vijana wanaume wasio na dosari mwilini, wenye sura nzuri, wanaoonyesha kipaji katika kila aina ya elimu, wenye ufahamu mzuri, wepesi kuelewa, na waliofuzu kuhudumu katika jumba la kifalme. Alikuwa awafundishe lugha na maandiko ya Wakaldayo.
5 Mfalme akawaagizia kiasi cha chakula na divai ya kila siku kutoka meza ya mfalme. Walikuwa wafundishwe kwa miaka mitatu, na hatimaye waingie kwenye utumishi wa mfalme.
Kral bu gençler için kendi sofrasından gündelik yiyecek ve şarap ayırdı. Üç yıl eğitildikten sonra gençler kralın önüne çıkarılacaklardı.
6 Baadhi ya hawa vijana walitoka Yuda: nao ni Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.
Seçilen gençler arasında Yahudalılar'dan Daniel, Hananya, Mişael ve Azarya da vardı.
7 Mkuu wa maafisa akawapa majina mapya: Danieli akamwita Belteshaza, Hanania akamwita Shadraki, Mishaeli akamwita Meshaki, na Azaria akamwita Abednego.
Saray görevlilerinin yöneticisi onlara yeni adlar koydu. Daniel'e Belteşassar, Hananya'ya Şadrak, Mişael'e Meşak, Azarya'ya Abed-Nego adını verdi.
8 Lakini Danieli alikusudia kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme na divai, naye akamwomba mkuu wa maafisa ruhusa ili asijinajisi kwa njia hii.
Daniel dinsel açıdan kendini kirletmemek için kralın onlara ayırdığı yemeklerden yemeyi de şaraptan içmeyi de istemedi. Bu yoldan kendini kirletmemek için saray görevlilerinin yöneticisine ricada bulundu.
9 Basi Mungu alikuwa amemfanya huyo mkuu wa maafisa kuonyesha upendeleo na huruma kwa Danieli,
Tanrı saray görevlileri yöneticisinin Daniel'e sevgiyle, sevecenlikle davranmasını sağladı.
10 lakini huyo mkuu wa maafisa akamwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme, aliyeagizia chakula na kinywaji chenu. Kwa nini aone nyuso zenu zikiwa mbaya kuliko za vijana wengine wa rika lenu? Mfalme atakata kichwa changu kwa sababu yenu.”
Adam Daniel'e, “Yiyecek içecek payınızı ayıran efendimiz kraldan korkarım” dedi, “Eğer yüzünüzü yaşıtınız olan öbür gençlerin yüzünden daha solgun görürse, başımı tehlikeye sokmuş olursunuz.”
11 Ndipo Danieli akamwambia mlinzi aliyeteuliwa na huyo mkuu wa maafisa kuwasimamia Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria,
Daniel, saray görevlileri yöneticisinin Hananya, Mişael, Azarya ve kendisinin başına koyduğu gözeticiye gidip, “Lütfen kullarınıza on gün olanak tanıyın” dedi, “Bu on gün içinde bize yemek için sebze, içmek için de su verilsin.
12 “Tafadhali wajaribu watumishi wako kwa siku kumi. Usitupe chochote ila nafaka na mboga za majani tule, na maji ya kunywa.
13 Baadaye ulinganishe sura zetu na vijana wanaokula chakula cha mfalme, ukawatendee watumishi wako kulingana na unachoona.”
Sonra yüzlerimizi kralın yemeklerini yiyen öbür gençlerin yüzleriyle kıyaslayın ve kullarınıza gördüğünüze göre davranın.”
14 Basi akakubali jambo hili, akawajaribu kwa siku kumi.
Gözetici bu isteği kabul etti ve onlara on gün deneme fırsatı verdi.
15 Mwisho wa zile siku kumi, walionekana kuwa na afya na kunawiri zaidi kuliko yeyote kati ya wale vijana waliokula chakula cha mfalme.
On gün sonra dört genç kralın yemeklerini yiyen öbür gençlerin hepsinden daha sağlıklı, daha iyi beslenmiş görünüyordu.
16 Hivyo mlinzi wao akaondoa chakula chao na divai yao waliopangiwa kula na kunywa, akawapa nafaka na mboga za majani badala yake.
Böylece gözetici o günden sonra kralın gençler için ayırdığı yemekle şarabı kaldırdı ve onlara sebze vermeyi sürdürdü.
17 Mungu akawapa hawa vijana wanne maarifa na ufahamu wa kila aina ya maandiko na elimu. Naye Danieli aliweza kufahamu maono na aina zote za ndoto.
Tanrı bu dört gence her konuda bilgi, beceri, bilgelik verdi. Daniel her çeşit görümü ve düşü yorumlayabiliyordu.
18 Mwisho wa muda uliowekwa na mfalme kuwaingiza kwake, mkuu wa maafisa akawaleta mbele ya Mfalme Nebukadneza.
Kralın belirlediği süre tamamlanınca, saray görevlileri yöneticisi gençleri Nebukadnessar'a götürdü.
19 Mfalme akazungumza nao, akaona hakuna aliyelingana na Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria. Hivyo wakaingia katika utumishi wa mfalme.
Kral onlarla görüştü; içlerinde Daniel, Hananya, Mişael, Azarya gibisi yoktu. Bu yüzden kralın hizmetine onlar atandı.
20 Katika kila jambo la hekima na ufahamu kuhusu kile mfalme alichowauliza, aliwaona bora mara kumi zaidi kuliko waganga na wasihiri wote katika ufalme wake wote.
Kral bilgelik ve anlayışla ilgili konularda onları sınadı ve dört genci ülkesindeki bütün sihirbazlardan, falcılardan on kat üstün buldu.
21 Naye Danieli akabaki huko mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi.
Kral Koreş'in krallığının birinci yılına dek Daniel sarayda kaldı.