< Danieli 1 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja akazingira Yerusalemu kwa jeshi.
In the third year of the reign of Jehoiakim, the king of Judah, came Nebuchadnezzar, the king of Babylon, against Jerusalem, and besieged it.
2 Bwana akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadneza, pamoja na baadhi ya vyombo kutoka Hekalu la Mungu. Hivi akavichukua hadi kwenye hekalu la mungu wake huko Shinari, naye akaviweka nyumbani ya hazina ya mungu wake.
And the Lord gave Jehoiakim, the king of Judah, into his hand, with part of the vessels of the house of God; and he carried them into the land of Shinar, to the house of his god; and he brought the vessels into the treasure-house of his god.
3 Kisha mfalme akamwagiza Ashpenazi, mkuu wa maafisa wa mfalme, kumletea baadhi ya Waisraeli kutoka jamaa ya mfalme na kutoka jamaa kuu,
And the king commanded Ashpenaz, the master of his eunuchs, that he should bring certain of the sons of Israel of the king's race, and of the princes,
4 vijana wanaume wasio na dosari mwilini, wenye sura nzuri, wanaoonyesha kipaji katika kila aina ya elimu, wenye ufahamu mzuri, wepesi kuelewa, na waliofuzu kuhudumu katika jumba la kifalme. Alikuwa awafundishe lugha na maandiko ya Wakaldayo.
youths in whom was no blemish, and well favored, and skilful in all wisdom, and having knowledge and intelligence and strength, to stand as servants in the king's palace, and be taught the writing and the language of the Chaldaeans.
5 Mfalme akawaagizia kiasi cha chakula na divai ya kila siku kutoka meza ya mfalme. Walikuwa wafundishwe kwa miaka mitatu, na hatimaye waingie kwenye utumishi wa mfalme.
And the king appointed them a daily provision of the king's food, and of the wine which he drank; so nourishing them three years, that at the end thereof they might stand as servants before the king.
6 Baadhi ya hawa vijana walitoka Yuda: nao ni Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.
Now among these were, of the sons of Judah, Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah.
7 Mkuu wa maafisa akawapa majina mapya: Danieli akamwita Belteshaza, Hanania akamwita Shadraki, Mishaeli akamwita Meshaki, na Azaria akamwita Abednego.
And the prince of the eunuchs gave them other names. To Daniel he gave the name of Belteshazzar; and to Hananiah, of Shadrach; and to Mishael, of Meshach; and to Azariah, of Abednego.
8 Lakini Danieli alikusudia kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme na divai, naye akamwomba mkuu wa maafisa ruhusa ili asijinajisi kwa njia hii.
But Daniel purposed in his heart that he would not defile himself with the portion of the king's meat, nor with the wine which he drank; therefore he requested of the prince of the eunuchs that he might not defile himself.
9 Basi Mungu alikuwa amemfanya huyo mkuu wa maafisa kuonyesha upendeleo na huruma kwa Danieli,
And God gave Daniel favor and kindness from the prince of the eunuchs.
10 lakini huyo mkuu wa maafisa akamwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme, aliyeagizia chakula na kinywaji chenu. Kwa nini aone nyuso zenu zikiwa mbaya kuliko za vijana wengine wa rika lenu? Mfalme atakata kichwa changu kwa sababu yenu.”
And the prince of the eunuchs said to Daniel, I fear my lord the king, who hath appointed your meat and your drink; for he might see your faces in worse condition than the youths of your age; then shall ye make me endanger my head to the king.
11 Ndipo Danieli akamwambia mlinzi aliyeteuliwa na huyo mkuu wa maafisa kuwasimamia Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria,
Then said Daniel to the steward whom the prince of the eunuchs had set over Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah,
12 “Tafadhali wajaribu watumishi wako kwa siku kumi. Usitupe chochote ila nafaka na mboga za majani tule, na maji ya kunywa.
Try thy servants ten days, and let them give us pulse to eat, and water to drink.
13 Baadaye ulinganishe sura zetu na vijana wanaokula chakula cha mfalme, ukawatendee watumishi wako kulingana na unachoona.”
Then let our countenances be looked upon before thee, and the countenances of the youths that eat of the portion of the king's meat; and as thou seest, deal with thy servants.
14 Basi akakubali jambo hili, akawajaribu kwa siku kumi.
And he consented to them in this matter, and tried them ten days.
15 Mwisho wa zile siku kumi, walionekana kuwa na afya na kunawiri zaidi kuliko yeyote kati ya wale vijana waliokula chakula cha mfalme.
And at the end of ten days their countenances appeared fairer and fatter in flesh than all the youths who ate the portion of the king's meat.
16 Hivyo mlinzi wao akaondoa chakula chao na divai yao waliopangiwa kula na kunywa, akawapa nafaka na mboga za majani badala yake.
So the steward took away the portion of their meat, and the wine which they should drink, and gave them pulse.
17 Mungu akawapa hawa vijana wanne maarifa na ufahamu wa kila aina ya maandiko na elimu. Naye Danieli aliweza kufahamu maono na aina zote za ndoto.
And God gave these four youths knowledge and skill in all learning and wisdom; and Daniel had understanding in all visions and dreams.
18 Mwisho wa muda uliowekwa na mfalme kuwaingiza kwake, mkuu wa maafisa akawaleta mbele ya Mfalme Nebukadneza.
And at the end of the days, when the king had commanded him to bring them before him, then the prince of the eunuchs brought them in before Nebuchadnezzar.
19 Mfalme akazungumza nao, akaona hakuna aliyelingana na Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria. Hivyo wakaingia katika utumishi wa mfalme.
And the king conversed with them; and among them all was found none like Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah. Therefore they stood as servants before the king.
20 Katika kila jambo la hekima na ufahamu kuhusu kile mfalme alichowauliza, aliwaona bora mara kumi zaidi kuliko waganga na wasihiri wote katika ufalme wake wote.
And in all matters of wisdom and understanding concerning which the king inquired of them, he found them ten times better than all the scribes and magicians that were in all his realm.
21 Naye Danieli akabaki huko mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi.
And Daniel lived even to the first year of Cyrus the king.