< Wakolosai 3 >
1 Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu.
ulwakuva kange ndeve uNguluve akavasyiluile palikimo nu Kilisite, mulondaghe isa mwne sino uKilisite ikukala uluvoko lwa ndia lwa Nguluve.
2 Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.
namungasaghaghe isa pa iisi, looli isa ku kyanya.
3 Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
ulwakuva mufwile, nu vwumi vufisilue palikimo nu Kilisite mwa Nguluve.
4 Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
unsiki ghuno uKilisite ilivoneka juno ghwe vwumi vwinu, pe pano na jumue mlivoneka palikimo nu mwene mu vwimike.
5 Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
pe lino musileke sino sili pa iisi sino lwe lufunyo lwa kihwani kya Nguluve,
6 Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
vwimila mu isi soni ing'halasi ja Nguluve jikwisa ku vano navitiki.
7 Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
mu isi najumue mukikalile palikimo navo.
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
neke lino nuloghiile muvusie isi sooni ghalasi, amasaghe mavivi, amaligho na masio malamafu ghano ghihuma mu malomo ghinu.
9 Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
namungasyanganaghe jumue kwa jumue, ulwakuva muvufulile uvumuunhu vwinu uvwa pakali na maghendele ghake.
10 nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
muvufwalile uvupia vuno vuvomvua vupia mu luhala kuhumila kwa jula juno alyavavumbile.
11 Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.
mu luhala ulu kusila muYunani nambe muYahudi, kukekua nambe kisila kukekua u mwimbi nambe juno na mwimbi um'bombi nambe juno na m'bombi, neke uYesu Kilisite ghwe sooni mu sooni.
12 Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
ndavule avimike va Nguluve, avimike avaghanike, muvufwalaghe uvumuunhu uvunono, uvuhugu, kunyenyekela, uvukoola nu lugudo.
13 Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
mutolelanilanaghe jumue kwa jumue. musaghilanaghe mweni. ndeve umuunhu alini nongua kwa junge ansaghilaghe ndavule uMutwa fino ikuvasahila umue.
14 Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.
kukila aghuo ghoni, muvisaghe nu lughano luno ghwe nsingi ghwa vunywilifu.
15 Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani.
ulutengano lwa Kilisite lwongelele mu numbula sinu. ndeve vwe vwimila vwa lutengano ulu kuuti mukavikilue mu m'bili ghumo. muvisaghe nu luhongesio.
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
ni lisio lwa Kilisite likalaghe n'kate jinu ku vutajili. mu vukoola vwoni, muvulanisianaghe na vungana jumue kwa jumueku sabuli, inyimbo, ni nyimbo sa munumbula. mwimbaghe mu luhongesio mu numbula sinu kwa Nguluve.
17 Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.
na kyokyoni kino muvomba mu masio nambe mu maghendele, vombagha soni ku litavua lya Mutwa Yesu. mu mwongesiaghe uNguluve Nhaata kukilia umwene.
18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.
vadala, vanyenyekelaghe avaghosi vinu, ndavulle lumunoghiile uMutwa.
19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.
na jumue vaghosi, muvaghanaghe avadala vinu, namungavisaghe vakali ku vanave.
20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.
vaanha, muvitikilaghe avapafi viinu mu sooni, ulwakuva lwe lukumunoghela uMutwa.
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
va baba namungavahovesiaghe avaanha viinu, neke navangisaghe kudenyeka inumbula.
22 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana.
vasung'ua, muvitikilaghe avavaha vinu mu lwa m'bili mu maghendele ghoni kisila imbombele inofu ija maaso hwene vaanhu vano vihovosia lwene. pe mu numbula ja lweli. mumwoghopaghe uNguluve. kyokyoni
23 Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu,
kino muvomba, namungavombaghe ndavule avaanhu, looli vombagha kuhuma mu numbula sinu ndavule uMutwa.
24 kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia.
mukagula kuuti mulikwupila ingigha kuhuma kwa Mutwa. ghwe Kilisite UMutwa juno mukum'bombela.
25 Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.
ulwakuva ghweni juno ivomba sino nasakyang'haani ilihighua mumaghendele ghano nagha kyang'haani ghano akavombile, kisila kubaghula.