< Wakolosai 3 >
1 Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu.
Seid ihr nun mit Christus auferweckt, so trachtet nach dem, was droben ist, wo Christus zur Rechten Gottes sitzt;
2 Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.
Trachtet nach dem, was droben ist, und nicht nach dem, was auf Erden ist.
3 Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
Ihr seid ja gestorben, und euer Leben ist mit Christus verborgen in Gott.
4 Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
Wann Christus, unser Leben, geoffenbart wird, dann werdet ihr auch mit Ihm in Herrlichkeit offenbar werden.
5 Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
So tötet nun eure Glieder, die da irdisch sind, Hurerei, Unreinheit, Leidenschaft, böse Lust, Habsucht, die Götzendienst sind;
6 Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
Um derentwillen der Zorn Gottes über die Kinder des Unglaubens kommt;
7 Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
In denen auch ihr einst gewandelt habt, als ihr unter ihnen lebtet.
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
Nun aber legt auch ihr alles ab, Zorn, Unmut, Bosheit, Lästerung, schandbare Worte, die aus eurem Munde gehen.
9 Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
Belügt einander nicht! Zieht den alten Menschen mit seinen Werken aus;
10 nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
Und zieht den neuen an, der erneuert wird zur Erkenntnis nach dem Ebenbilde Dessen, Der ihn geschaffen hat;
11 Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.
Da gilt nicht Heide, noch Jude, noch Beschneidung, noch Vorhaut, noch Ausländer, Skythe, Knecht, noch Freier, sondern alles und in allen ist Christus.
12 Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
So zieht nun an, als Gottes Auserwählte, Heilige und Geliebte, herzliches Erbarmen, Wohlwollen, Demut, Sanftmut und Langmut.
13 Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
Seid verträglich gegeneinander und haltet einander etwas zugut, wenn einer etwas gegen den anderen zu klagen hat, wie Christus auch euch vieles vergeben hat, so tut auch ihr.
14 Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.
Über alles dieses aber
15 Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani.
Und Christi Friede herrsche in euren Herzen, wozu ihr auch berufen seid in einem Leib, und seid dankbar dafür.
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Das Wort Christi wohne reichlich unter euch in aller Weisheit, lehrt und ermahnt einander mit Psalmen, Lobgesängen und geistlichen Liedern und singt in Dankbarkeit dem Herrn in euren Herzen.
17 Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.
Und alles, was ihr tut in Wort oder Tat, das tut alles im Namen des Herrn Jesus, indem ihr Gott dem Vater durch Ihn dankt.
18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.
Ihr Weiber, seid untertan euren Männern in dem Herrn, wie es sich gebührt.
19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.
Ihr Männer, liebt eure Weiber und werdet nicht bitter gegen sie.
20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.
Ihr Kinder, gehorcht in allem euren Eltern, denn dies ist dem Herrn wohlgefällig.
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
Ihr Väter, reizt eure Kinder nicht, daß sie nicht mutlos werden.
22 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana.
Ihr Knechte, gehorcht in allen Stücken euren leiblichen Herren, nicht mit Augendienerei, als wolltet ihr Menschen gefallen, sondern in Einfalt des Herzens und aus Gottesfurcht,
23 Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu,
Und alles, was ihr tut, das tut von Herzen, als dem Herrn und nicht den Menschen.
24 kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia.
Und seid eingedenk, daß ihr von dem Herrn empfangen werdet die Vergeltung des Erbes; denn dem Herrn Christus dient ihr.
25 Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.
Wer aber Unrecht tut, der wird empfangen, was er Unrecht getan, und da findet kein Ansehen der Person statt.