< Wakolosai 3 >

1 Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu.
Kui te koos Kristusega olete üles äratatud, siis taotlege seda, mis on ülal, kus Kristus istub Jumala paremal käel.
2 Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.
Mõtelge sellele, mis on ülal, mitte sellele, mis on maa peal,
3 Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
sest teie olete surnud ja teie elu on Kristusega varjul Jumalas.
4 Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
Kui Kristus, kes on teie elu, saab avalikuks, siis saate ka teie koos temaga avalikuks auhiilguses.
5 Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
Seepärast surmake nüüd endas kõik maine: hoorus, räpasus, kired, kurjad himud ja ahnus, mis on ebajumalateenistus;
6 Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
nende pärast tuleb Jumala viha.
7 Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
Teiegi käisite varem nendes, kui te sellist elu elasite.
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
Nüüd aga jätke maha kõik see: viha, raev, õelus, laim, räpased sõnad oma huultelt.
9 Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
Ärge valetage üksteisele, sest te olete vana inimese tema harjumustega lahti riietanud
10 nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
ja rõivastunud uue inimesega, keda uuendatakse õigesti tunnetama oma Looja näo kohaselt.
11 Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.
Nii pole enam kreeklast ega juuti, ümberlõigatut ega ümberlõikamatut, võõramaalast ega sküüti, ei orja ega vaba, vaid kõik ja kõikides on Kristus.
12 Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Rõivastuge siis nagu sobib Jumala valitud pühale ja armastatud rahvale: kaastunde, lahkuse, alandlikkuse, leebuse ja pika meelega.
13 Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
Sallige üksteist ja andke üksteisele andeks, kui kellelgi on midagi teise vastu. Nagu Issand teile on andeks andnud, andke ka teie!
14 Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.
Aga kõige selle üle olgu armastus, mis teid täiuslikus ühtsuses kokku seob.
15 Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani.
Ja teie südameis valitsegu Kristuse rahu, sest selleks te olete ühe ihuna kutsutud. Ja olge tänulikud!
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Kristuse sõna elagu rikkalikult teie sees! Kogu tarkuses õpetage ja manitsege üksteist psalmide, hümnide ja Vaimus antud lauludega, lauldes tänuliku südamega Jumalale!
17 Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.
Ja kõik, mida iganes te teete sõna või teoga, seda tehke Issanda Jeesuse nimel, tänades Isa Jumalat tema kaudu.
18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.
Naised, alistuge meestele, nagu on kohane Issandas!
19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.
Mehed, armastage oma naisi ja ärge tehke nende elu kibedaks!
20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.
Lapsed, olge kuulekad oma vanematele igas asjas, sest see meeldib Issandale!
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
Isad, ärge kohelge oma lapsi liiga karmilt, et nad ei kaotaks julgust!
22 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana.
Orjad, kuuletuge oma maistele isandatele kõiges, mitte ainult nende silme all nagu need, kes püüavad inimestele meeldida, vaid siira südamega, kartes Issandat.
23 Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu,
Mida te iganes teete, tehke kogu südamest, nii nagu Issandale ja mitte nagu inimestele,
24 kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia.
sest te teate, et saate Issandalt tasuks pärandi. Teenige Issandat Kristust!
25 Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.
Aga sellele, kes teeb ülekohut, tasutakse tema ülekohtu järgi, ega tehta vahet isikute vahel.

< Wakolosai 3 >