< Wakolosai 3 >
1 Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu.
If then God has raised you with Christ, seek the things above, where Christ is sitting at the right hand of God.
2 Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.
Think about the things above, not about the things on earth.
3 Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
For you have died, and your life is hidden with Christ in God.
4 Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
When Christ appears, who is your life, then you will also appear with him in glory.
5 Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
Put to death, then, the members that are on earth—sexual immorality, uncleanness, passion, evil desire, and greed, which is idolatry.
6 Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
It is for these things that the wrath of God is coming on the sons of disobedience.
7 Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
It is in these things that you also once walked when you lived in them.
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
But now you must get rid of all these things—wrath, anger, evil intentions, insults, and obscene speech from your mouth.
9 Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
Do not lie to one another, since you have taken off the old man with its practices,
10 nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
and you have put on the new man that is being made new in knowledge according to the image of the one who created it.
11 Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.
This is where there is no Greek and Jew, circumcision and uncircumcision, barbarian, Scythian, slave, freeman, but Christ is all, and is in all.
12 Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Therefore, as God's chosen ones, holy and beloved, put on a heart of mercy, kindness, humility, gentleness, and patience.
13 Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
Bear with one another. Be gracious to each other. If someone has a complaint against someone else, forgive in the same way that the Lord has forgiven you.
14 Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.
Above all these things, have love, which is the bond of perfection.
15 Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani.
Let the peace of Christ rule in your hearts. It was for this peace that you were called in one body. And be thankful.
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Let the word of Christ live in you richly. With all wisdom teach and admonish one another with psalms and hymns and spiritual songs. Sing with thankfulness in your hearts to God.
17 Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.
Whatever you do, in word or in deed, do all in the name of the Lord Jesus. Give thanks to God the Father through him.
18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.
Wives, submit to your husbands, as it is appropriate in the Lord.
19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.
Husbands, love your wives, and do not be bitter against them.
20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.
Children, obey your parents in all things, for this is pleasing in the Lord.
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
Fathers, do not provoke your children, so that they will not be discouraged.
22 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana.
Slaves, obey your masters according to the flesh in all things, not with eyeservice as people pleasers, but with a sincere heart. Fear the Lord.
23 Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu,
Whatever you do, work from the soul as to the Lord and not as to people.
24 kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia.
You know that you will receive from the Lord the reward of the inheritance. It is the Lord Christ whom you serve.
25 Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.
For anyone who does unrighteousness will receive the penalty for the unrighteousness that he did, and there is no favoritism.