< Wakolosai 3 >
1 Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu.
If you then be risen with Christ, seek those things which are above, where Christ sits on the right hand of God.
2 Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.
Set your affection on things above, not on things on the earth.
3 Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
For you are dead, and your life is hid with Christ in God.
4 Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
When Christ, who is our life, shall appear, then shall you also appear with him in glory.
5 Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
Mortify therefore your members which are on the earth; fornication, uncleanness, inordinate affection, evil concupiscence, and covetousness, which is idolatry:
6 Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
For which things’ sake the wrath of God comes on the children of disobedience:
7 Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
In the which you also walked some time, when you lived in them.
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
But now you also put off all these; anger, wrath, malice, blasphemy, filthy communication out of your mouth.
9 Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
Lie not one to another, seeing that you have put off the old man with his deeds;
10 nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
And have put on the new man, which is renewed in knowledge after the image of him that created him:
11 Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.
Where there is neither Greek nor Jew, circumcision nor uncircumcision, Barbarian, Scythian, bond nor free: but Christ is all, and in all.
12 Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
Put on therefore, as the elect of God, holy and beloved, bowels of mercies, kindness, humbleness of mind, meekness, long-suffering;
13 Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
Forbearing one another, and forgiving one another, if any man have a quarrel against any: even as Christ forgave you, so also do you.
14 Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.
And above all these things put on charity, which is the bond of perfection.
15 Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani.
And let the peace of God rule in your hearts, to the which also you are called in one body; and be you thankful.
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
Let the word of Christ dwell in you richly in all wisdom; teaching and admonishing one another in psalms and hymns and spiritual songs, singing with grace in your hearts to the Lord.
17 Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.
And whatever you do in word or deed, do all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God and the Father by him.
18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.
Wives, submit yourselves to your own husbands, as it is fit in the Lord.
19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.
Husbands, love your wives, and be not bitter against them.
20 Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.
Children, obey your parents in all things: for this is well pleasing to the Lord.
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
Fathers, provoke not your children to anger, lest they be discouraged.
22 Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana.
Servants, obey in all things your masters according to the flesh; not with eye-service, as men pleasers; but in singleness of heart, fearing God;
23 Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu,
And whatever you do, do it heartily, as to the Lord, and not to men;
24 kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia.
Knowing that of the Lord you shall receive the reward of the inheritance: for you serve the Lord Christ.
25 Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.
But he that does wrong shall receive for the wrong which he has done: and there is no respect of persons.