< Wakolosai 2 >
1 Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi.
Albowiem chcę, abyście wiedzieli jako wielką trudność mam o was i o tych, którzy są w Laodycei i którzykolwiek nie widzieli oblicza mego w ciele;
2 Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe,
Aby pocieszone były serca ich, będąc spojone miłością, a to ku wszelkiemu bogactwu zupełnego i pewnego wyrozumienia, ku poznaniu tajemnicy Boga i Ojca, i Chrystusa,
3 ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa.
W którym skryte są wszystkie skarby mądrości i umiejętności.
4 Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi.
A toć mówię, aby was nikt fałszywemi dowodami nie oszukał przez wystawną mowę.
5 Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.
Bo aczkolwiek nie jestem obecny ciałem, ale duchem jestem z wami, radując się i widząc porządek wasz i utwierdzenie wiary waszej w Chrystusa;
6 Hivyo basi, kama vile mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kukaa ndani yake,
Przetoż jakoście przyjęli Pana Jezusa Chrystusa, tak w nim chodźcie,
7 mkiwa na mizizi, na mmejengwa ndani yake, mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa, na kufurika kwa wingi wa shukrani.
Będąc wkorzenieni i wybudowani na nim, i utwierdzeni w wierze, jakoście się nauczyli, obfitując w niej z dziękowaniem.
8 Angalieni mtu yeyote asiwafanye ninyi mateka kwa elimu batili na madanganyo matupu yanayotegemea mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya ulimwengu badala ya Kristo.
Patrzcież, żeby was kto sobie w korzyść nie obrócił przez filozofiję i przez próżne oszukanie, ucząc według ustawy ludzkiej, według żywiołów świata, a nie według Chrystusa,
9 Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu,
Gdyż w nim mieszka wszystka zupełność bóstwa cieleśnie.
10 nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye ndiye mkuu juu ya kila enzi na kila mamlaka.
I jesteście w nim dopełnieni, który jest głową wszelkiego księstwa i zwierzchności,
11 Katika Kristo pia mlitahiriwa kwa kutengwa mbali na asili ya dhambi, si kwa tohara inayofanywa kwa mikono ya wanadamu, bali kwa ile tohara iliyofanywa na Kristo,
W którym i obrzezani jesteście obrzezką nie ręką uczynioną, to jest, zewlekłszy ciało wszystkich grzechów ciała przez obrzezkę Chrystusową.
12 mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
Pogrzebieni z nim będąc w chrzcie; w którymeście też społem z nim wzbudzeni przez wiarę, którą sprawuje Bóg, który go wzbudził od umarłych.
13 Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote,
I was, gdyście byli umarłymi w grzechach i nieobrzezce ciała waszego, wespół z nim ożywił, odpuściwszy wam wszystkie grzechy.
14 akiisha kuifuta ile hati yenye mashtaka yaliyokuwa yanatukabili, pamoja na maagizo yake. Aliiondoa isiwepo tena, akiigongomea kwenye msalaba wake.
Zmazawszy on, który był przeciwko nam, cyrograf w ustawach zależący, który nam był przeciwny, zniósł go z pośrodku, przybiwszy go do krzyża;
15 Mungu akiisha kuzivua enzi na mamlaka, alizifanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuziburura kwa ujasiri, akizishinda katika msalaba wa Kristo.
I złupiwszy księstwa i mocy, wiódł je na podziw, jawnie tryumfując z nich sam przez się.
16 Kwa hiyo mtu asiwahukumu ninyi kuhusu vyakula au vinywaji, au kuhusu kuadhimisha sikukuu za dini, au Sikukuu za Mwezi Mwandamo au siku ya Sabato.
Niechajże was tedy nikt nie sądzi dla pokarmu, albo dla napoju; albo z strony święta, albo nowiu miesiąca, albo sabatów,
17 Hizi zilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja, lakini ile iliyo halisi imo ndani ya Kristo.
Które są cieniem rzeczy przyszłych, ale prawdą jest ciało Chrystusowe.
18 Mtu yeyote asiwaondolee thawabu yenu kwa kusisitiza kunyenyekea kwake na kuabudu malaika. Mtu kama huyo hudumu katika maono yake, akijivuna bila sababu katika mawazo ya kibinadamu.
Niechaj was nikt wygranego zakładu nie osądza, który się dobrowolnie w pokorę i w służbę Aniołów, których nie widział, wdaje, próżno się nadymając z umysłu ciała swego.
19 Yeye amepoteza ushirikiano na Kichwa, ambaye kutoka kwake mwili wote unalishwa na kushikamanishwa pamoja kwa viungo na mishipa, nao hukua kwa ukuaji utokao kwa Mungu.
A nie trzymając się głowy Chrystusa, z którego wszystko ciało przez stawy i związania posiłek biorąc i wespół spojone będąc, rośnie wzrostem Bożym.
20 Kwa kuwa mlikufa pamoja na Kristo, mkayaacha yale mafundisho ya msingi ya ulimwengu huu, kwa nini bado mnaishi kama ninyi ni wa ulimwengu? Kwa nini mnajitia chini ya amri:
Jeźliście tedy umarli z Chrystusem żywiołom świata tego, przeczże się, jakobyście jeszcze żyli światu, ustawami bawicie?
21 “Msishike! Msionje! Msiguse!”?
Mówią niektórzy: Nie dotykaj się, ani kosztuj, ani ruszaj;
22 Haya yote mwisho wake ni kuharibika yanapotumiwa, kwa sababu msingi wake ni katika maagizo na mafundisho ya wanadamu.
Co wszystko kazi się samem używaniem, według przykazań i nauk ludzkich;
23 Kwa kweli amri kama hizo huonekana kama zina hekima, katika namna za ibada walizojitungia wenyewe, na unyenyekevu wa uongo na kuutawala mwili kwa ukali, lakini hayafai kitu katika kuzuia tamaa za mwili.
Które mają kształt mądrości w nabożeństwie dobrowolnie obranem i w pokorze, i w niefolgowaniu ciału; wszakże nie mają żadnej wagi, tylko do nasycenia ciała służą.