< Wakolosai 2 >
1 Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi.
For I would that ye knew what great conflict I have for you, and [for] them at Laodicea, and [for] as many as have not seen my face in the flesh;
2 Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe,
That their hearts may be comforted, being knit together in love, and to all riches of the full assurance of understanding to the acknowledgment of the mystery of God, and of the Father, and of Christ;
3 ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa.
In whom are hid all the treasures of wisdom and knowledge.
4 Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi.
And this I say, lest any man should deceive you with enticing words.
5 Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.
For though I am absent in the flesh, yet I am with you in the spirit, joying and beholding your order, and the steadfastness of your faith in Christ.
6 Hivyo basi, kama vile mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kukaa ndani yake,
As ye have therefore received Christ Jesus the Lord, [so] walk ye in him:
7 mkiwa na mizizi, na mmejengwa ndani yake, mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa, na kufurika kwa wingi wa shukrani.
Rooted and built up in him, and established in the faith, as ye have been taught, abounding in it with thanksgiving.
8 Angalieni mtu yeyote asiwafanye ninyi mateka kwa elimu batili na madanganyo matupu yanayotegemea mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya ulimwengu badala ya Kristo.
Beware lest any man make a prey of you through philosophy and vain deceit, after the tradition of men, after the rudiments of the world, and not after Christ.
9 Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu,
For in him dwelleth all the fullness of the Godhead bodily.
10 nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye ndiye mkuu juu ya kila enzi na kila mamlaka.
And ye are complete in him, who is the head of all principality and power:
11 Katika Kristo pia mlitahiriwa kwa kutengwa mbali na asili ya dhambi, si kwa tohara inayofanywa kwa mikono ya wanadamu, bali kwa ile tohara iliyofanywa na Kristo,
In whom also ye are circumcised with the circumcision made without hands, in putting off the body of the sins of the flesh by the circumcision of Christ:
12 mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
Buried with him in baptism, in which also ye are raised with [him] through the faith of the operation of God, who hath raised him from the dead.
13 Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote,
And you, being dead in your sins and the uncircumcision of your flesh, hath he made alive together with him, having forgiven you all trespasses;
14 akiisha kuifuta ile hati yenye mashtaka yaliyokuwa yanatukabili, pamoja na maagizo yake. Aliiondoa isiwepo tena, akiigongomea kwenye msalaba wake.
Blotting out the hand-writing of ordinances that was against us, which was contrary to us, and took it out of the way, nailing it to his cross;
15 Mungu akiisha kuzivua enzi na mamlaka, alizifanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuziburura kwa ujasiri, akizishinda katika msalaba wa Kristo.
[And] having despoiled principalities and powers, he made a show of them openly, triumphing over them in it.
16 Kwa hiyo mtu asiwahukumu ninyi kuhusu vyakula au vinywaji, au kuhusu kuadhimisha sikukuu za dini, au Sikukuu za Mwezi Mwandamo au siku ya Sabato.
Let no man therefore judge you in food, or in drink, or in respect of a holy-day, or or the new-moon, or of the sabbaths:
17 Hizi zilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja, lakini ile iliyo halisi imo ndani ya Kristo.
Which are a shadow of things to come; but the body [is] of Christ.
18 Mtu yeyote asiwaondolee thawabu yenu kwa kusisitiza kunyenyekea kwake na kuabudu malaika. Mtu kama huyo hudumu katika maono yake, akijivuna bila sababu katika mawazo ya kibinadamu.
Let no man beguile you of your reward in a voluntary humility and worshiping of angels, intruding into those things which he hath not seen, vainly puffed up by his fleshly mind,
19 Yeye amepoteza ushirikiano na Kichwa, ambaye kutoka kwake mwili wote unalishwa na kushikamanishwa pamoja kwa viungo na mishipa, nao hukua kwa ukuaji utokao kwa Mungu.
And not holding the head, from which all the body by joints and bands having nourishment ministered, and knit together, increaseth with the increase of God.
20 Kwa kuwa mlikufa pamoja na Kristo, mkayaacha yale mafundisho ya msingi ya ulimwengu huu, kwa nini bado mnaishi kama ninyi ni wa ulimwengu? Kwa nini mnajitia chini ya amri:
Wherefore, if ye are dead with Christ from the rudiments of the world, why, as though living in the world, are ye subject to ordinances,
21 “Msishike! Msionje! Msiguse!”?
(Touch not; taste not; handle not;
22 Haya yote mwisho wake ni kuharibika yanapotumiwa, kwa sababu msingi wake ni katika maagizo na mafundisho ya wanadamu.
Which all are to perish with the using; ) according to the commandments and doctrines of men?
23 Kwa kweli amri kama hizo huonekana kama zina hekima, katika namna za ibada walizojitungia wenyewe, na unyenyekevu wa uongo na kuutawala mwili kwa ukali, lakini hayafai kitu katika kuzuia tamaa za mwili.
Which things have indeed a show of wisdom in will-worship, and humility, and neglecting of the body; not in any honor to the satisfying of the flesh.