< Wakolosai 1 >

1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu:
Paul, an apostle of Jesus Christ, by the will of God, and Timothy, a brother,
2 Kwa ndugu watakatifu na waaminifu katika Kristo, waishio Kolosai: Neema na amani zitokazo kwa Mungu Baba yetu ziwe nanyi.
To the saints and faithful brethren in Christ Jesus, who are at Colossa.
3 Siku zote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunapowaombea ninyi,
Grace be to you and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ. We give thanks to God, and the Father of our Lord Jesus Christ, praying always for you.
4 kwa sababu tumesikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu, na upendo wenu mlio nao kwa watakatifu wote:
Hearing your faith in Christ Jesus, and the love which you have towards all the saints.
5 imani na upendo ule utokao katika tumaini mlilowekewa akiba mbinguni, na ambalo mmesikia habari zake katika neno la kweli, yaani, ile Injili
For the hope that is laid up for you in heaven, which you have heard in the word of the truth of the gospel,
6 iliyowafikia ninyi. Duniani kote Injili hii inazaa matunda na kuenea kama ilivyokuwa kwenu tangu siku ile mlipoisikia na kuielewa neema ya Mungu katika kweli yote.
Which is come unto you, as also it is in the whole world, and bringeth forth fruit and groweth, even as it doth in you, since the day you heard and knew the grace of God in truth.
7 Mlijifunza habari zake kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu mpendwa, yeye aliye mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yenu,
As you learned of Epaphras, our most beloved fellow servant, who is for you a faithful minister of Christ Jesus;
8 ambaye pia ametuambia kuhusu upendo wenu katika Roho.
Who also hath manifested to us your love in the spirit.
9 Kwa sababu hii, tangu siku ile tuliposikia habari zenu, hatujakoma kuomba kwa ajili yenu na kumsihi Mungu awajaze ninyi maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote ya kiroho na ufahamu.
Therefore we also, from the day that we heard it, cease not to pray for you, and to beg that you may be filled with the knowledge of his will, in all wisdom, and spiritual understanding:
10 Nasi tunaomba haya ili mpate kuishi maisha yanayostahili mbele za Bwana, na mpate kumpendeza kwa kila namna: mkizaa matunda kwa kila kazi njema, mkikua katika kumjua Mungu,
That you may walk worthy of God, in all things pleasing; being fruitful in every good work, and increasing in the knowledge of God:
11 mkiwa mmetiwa nguvu kwa uwezo wote kwa kadiri ya nguvu yake yenye utukufu, ili mpate kuwa na wingi wa saburi na uvumilivu. Nanyi kwa furaha
Strengthened with all might, according to the power of his glory, in all patience and longsuffering with joy,
12 mkimshukuru Baba, ambaye amewastahilisha kushiriki katika urithi wa watakatifu katika ufalme wa nuru.
Giving thanks to God the Father, who hath made us worthy to be partakers of the lot of the saints in light:
13 Kwa maana ametuokoa kutoka ufalme wa giza na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa,
Who hath delivered us from the power of darkness, and hath translated us into the kingdom of the Son of his love,
14 ambaye katika yeye tunao ukombozi, yaani msamaha wa dhambi.
In whom we have redemption through his blood, the remission of sins;
15 Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
Who is the image of the invisible God, the firstborn of every creature:
16 Kwake yeye vitu vyote vilivyoko mbinguni na juu ya nchi viliumbwa: vitu vinavyoonekana na visivyoonekana, viwe ni viti vya enzi au falme, au wenye mamlaka au watawala; vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
For in him were all things created in heaven and on earth, visible and invisible, whether thrones, or dominations, or principalities, or powers: all things were created by him and in him.
17 Yeye alikuwepo kabla ya vitu vyote, na katika yeye vitu vyote vinashikamana pamoja.
And he is before all, and by him all things consist.
18 Yeye ndiye kichwa cha mwili, yaani kanisa, naye ndiye mwanzo na mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, ili yeye awe mkuu katika vitu vyote.
And he is the head of the body, the church, who is the beginning, the firstborn from the dead; that in all things he may hold the primacy:
19 Kwa kuwa ilimpendeza Mungu kwamba utimilifu wake wote ukae ndani yake,
Because in him, it hath well pleased the Father, that all fullness should dwell;
20 na kwa njia yake aweze kuvipatanisha vitu vyote na yeye mwenyewe, viwe ni vitu vilivyo duniani au vilivyo mbinguni, kwa kufanya amani kwa damu yake, iliyomwagika msalabani.
And through him to reconcile all things unto himself, making peace through the blood of his cross, both as to the things that are on earth, and the things that are in heaven.
21 Hapo kwanza mlikuwa mmetengana na Mungu, na mlikuwa adui zake katika nia zenu kwa sababu ya mienendo yenu mibaya.
And you, whereas you were some time alienated and enemies in mind in evil works:
22 Lakini sasa Mungu amewapatanisha ninyi kwa njia ya mwili wa Kristo kupitia mauti, ili awalete mbele zake mkiwa watakatifu, bila dosari wala lawama,
Yet now he hath reconciled in the body of his flesh through death, to present you holy and unspotted, and blameless before him:
23 ikiwa mnaendelea katika imani yenu mkiwa imara na thabiti, pasipo kuliacha tumaini lililoahidiwa katika Injili. Hii ndiyo ile Injili mliyoisikia, ambayo imehubiriwa kwa kila kiumbe chini ya mbingu, na ambayo mimi Paulo nimekuwa mtumwa wake.
If so ye continue in the faith, grounded and settled, and immoveable from the hope of the gospel which you have heard, which is preached in all the creation that is under heaven, whereof I Paul am made a minister.
24 Sasa nafurahia kule kuteseka kwangu kwa ajili yenu, na katika mwili wangu ninatimiliza yale yaliyopungua katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
Who now rejoice in my sufferings for you, and fill up those things that are wanting of the sufferings of Christ, in my flesh, for his body, which is the church:
25 Mimi nimekuwa mtumishi wa kanisa kwa wajibu alionipa Mungu ili kuwaletea ninyi Neno la Mungu kwa ukamilifu:
Whereof I am made a minister according to the dispensation of God, which is given me towards you, that I may fulfill the word of God:
26 Hii ni siri iliyokuwa imefichika tangu zamani na kwa vizazi vingi, lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu. (aiōn g165)
The mystery which hath been hidden from ages and generations, but now is manifested to his saints, (aiōn g165)
27 Kwao, Mungu amechagua kujulisha miongoni mwa watu wa Mataifa utukufu wa utajiri wa siri hii, ambayo ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu.
To whom God would make known the riches of the glory of this mystery among the Gentiles, which is Christ, in you the hope of glory.
28 Yeye ndiye tunayemtangaza, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu kwa hekima yote ili tuweze kumleta kila mmoja akiwa amekamilika katika Kristo.
Whom we preach, admonishing every man, and teaching every man in all wisdom, that we may present every man perfect in Christ Jesus.
29 Kwa ajili ya jambo hili, ninajitaabisha, nikijitahidi kwa kadiri ya nguvu zake ambazo hutenda kazi ndani yangu kwa uweza mwingi.
Wherein also I labour, striving according to his working which he worketh in me in power.

< Wakolosai 1 >