< Amosi 1 >

1 Maneno ya Amosi, mmoja wa wachunga wanyama wa Tekoa: yale aliyoyaona kuhusu Israeli miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi, wakati Uzia alikuwa mfalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli.
The words of Amos, who was among the herdmen of Tekoa, which he saw concerning Israel in the days of Uzziah king of Judah, and in the days of Jeroboam the son of Joash king of Israel, two years before the earthquake.
2 Alisema: “Bwana ananguruma toka Sayuni, pia ananguruma kutoka Yerusalemu; malisho ya wachunga wanyama yanakauka, kilele cha Karmeli kinanyauka.”
And he said, The LORD will roar from Zion, and utter his voice from Jerusalem; and the habitations of the shepherds shall mourn, and the top of Carmel shall wither.
3 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Dameski, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliipura Gileadi kwa vyombo vya chuma vyenye meno.
Thus saith the LORD; For three transgressions of Damascus, and for four, I will not turn away its [punishment]; because they have threshed Gilead with threshing instruments of iron:
4 Nitatuma moto juu ya nyumba ya Hazaeli ambao utateketeza ngome za Ben-Hadadi.
But I will send a fire into the house of Hazael, which shall devour the palaces of Ben-hadad.
5 Nitalivunja lango la Dameski; nitamwangamiza mfalme aliyeko katika Bonde la Aveni, na yeye ambaye anaishika fimbo ya utawala katika Beth-Edeni. Watu wote wa Aramu watakwenda uhamishoni huko Kiri,” asema Bwana.
I will break also the bar of Damascus, and cut off the inhabitant from the plain of Aven, and him that holdeth the scepter from the house of Eden: and the people of Syria shall go into captivity to Kir, saith the LORD.
6 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Gaza, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu walichukua mateka jumuiya nzima na kuwauza kwa Edomu,
Thus saith the LORD; For three transgressions of Gaza, and for four, I will not turn away its [punishment]: because they carried away captive the whole captivity, to deliver [them] up to Edom:
7 nitatuma moto juu ya kuta za Gaza ambao utateketeza ngome zake.
But I will send a fire on the wall of Gaza, which shall devour its palaces:
8 Nitamwangamiza mfalme wa Ashdodi na yeye aishikaye fimbo ya utawala katika Ashkeloni. Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni, hadi Mfilisti wa mwisho atakapokufa,” asema Bwana Mwenyezi.
And I will cut off the inhabitant from Ashdod, and him that holdeth the scepter from Ashkelon, and I will turn my hand against Ekron: and the remnant of the Philistines shall perish, saith the Lord GOD.
9 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Tiro, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu ameuza jumuiya nzima ya mateka kwa Edomu, na kutokujali mapatano ya undugu,
Thus saith the LORD; For three transgressions of Tyre, and for four, I will not turn away its [punishment]: because they delivered up the whole captivity to Edom, and remembered not the brotherly covenant:
10 Nitatuma moto kwenye kuta za Tiro ambao utateketeza ngome zake.”
But I will send a fire on the wall of Tyre, which shall devour its palaces:
11 Hili ndilo Bwana asemalo: “Kwa dhambi tatu za Edomu, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, alikataa kuonyesha huruma yoyote, kwa sababu hasira yake kali iliendelea kupanda wakati wote na ghadhabu iliwaka bila kuzuiliwa.
Thus saith the LORD; For three transgressions of Edom, and for four, I will not turn away its [punishment]: because he pursued his brother with the sword, and cast off all pity, and his anger did tear perpetually, and [he] kept his wrath for ever:
12 Nitatuma moto juu ya Temani ambao utateketeza ngome za Bosra.”
But I will send a fire upon Teman, which shall devour the palaces of Bozrah.
13 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kwa dhambi tatu za Amoni, hata kwa dhambi nne, sitaizuia ghadhabu yangu. Kwa sababu aliwatumbua wanawake wajawazito wa Gileadi ili kuongeza mipaka yake.
Thus saith the LORD; For three transgressions of the children of Ammon, and for four, I will not turn away [their punishment]: because they have ripped up the women with child of Gilead, that they might enlarge their border:
14 Nitatuma moto kwenye kuta za Raba ambao utateketeza ngome zake katikati ya vilio vya vita katika siku ya mapigano, katikati ya upepo mkali katika siku ya dhoruba.
But I will kindle a fire in the wall of Rabbah, and it shall devour its palaces, with shouting in the day of battle, with a tempest in the day of the whirlwind:
15 Mfalme wake atakwenda uhamishoni, yeye pamoja na maafisa wake,” asema Bwana.
And their king shall go into captivity, he and his princes together, saith the LORD.

< Amosi 1 >