< Amosi 9 >

1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
Videl sem Gospoda stati na oltarju in rekel je: »Udari vratno preklado, da se bodo podboji lahko tresli, in ureži jih na glavi, vse izmed njih in jaz bom zadnje izmed njih ubil z mečem in kdor izmed njih beži, ne bo pobegnil proč in kdor se izmed njih umika, ne bo osvobojen.
2 Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
Čeprav kopljejo v pekel, jih bo moja roka vzela od tam. Čeprav plezajo gor do nebes, jih bom od tam privedel dol. (Sheol h7585)
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
Čeprav se skrijejo na vrhu Karmela, jih poiščem in vzamem od tam. Čeprav so skriti pred mojim pogledom na dnu morja, bom tam zapovedal kači in ta jih bo pičila.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
Čeprav gredo v ujetništvo pred svojimi sovražniki, bom tja poslal meč in ta jih bo ubil in svoje oči bom naravnal nanje za zlo in ne za dobro.«
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
Gospod Bog nad bojevniki je tisti, ki se dotika dežele in ta se bo stopila in vsi, ki prebivajo v njej, bodo žalovali. In ta se bo vzdignila v celoti kakor poplava in potopljena bo kakor z egiptovsko poplavo.
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
On je tisti, ki gradi svoja nadstropja v nebesih in je utemeljil svoje krdelo na zemlji. On, ki kliče za morskimi vodami in jih izliva na obličje zemlje. Gospod je njegovo ime.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
» Ali mi niste kakor otroci Etiopijcev, oh Izraelovi otroci?« govori Gospod: »Mar nisem jaz Izraela privedel gor iz egiptovske dežele? In Filistejce iz Kaftorja in Sirce iz Kira?
8 “Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
Glejte, oči Gospoda Boga so nad grešnim kraljestvom in uničil ga bom izpred obličja zemlje; le, da ne bom popolnoma uničil Jakobove hiše, « govori Gospod.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
»Kajti glejte, zapovedal bom in Izraelovo hišo bom presejal med vse narode, kakor je žito presejano na situ, vendar niti najmanjše zrno ne bo padlo na zemljo.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
Vsi grešniki mojega ljudstva bodo umrli pod mečem, ki pravijo: ›Zlo nas ne bo dohitelo niti nas ne bo srečalo.‹
11 “Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
Na tisti dan bom vzdignil Davidovo šotorsko svetišče, ki je padlo in zaprl njegove vrzeli. In vzdignil bom njegove ruševine in zgradil ga bom kakor v dneh davnine,
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
da bodo lahko vzeli v last preostanek Edóma in vseh poganov, ki so imenovani z mojim imenom, « govori Gospod, ki to dela.
13 “Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
»Glejte, pridejo dnevi, « govori Gospod, »ko bo orač prehitel žanjca in tlačitelj grozdja tistega, ki seje seme, in gore bodo kapljale sladko vino in vsi hribi se bodo topili.
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
Ponovno bom privedel ujetništvo svojega ljudstva Izraela in zgradili bodo opustošena mesta in jih poselili, in sadili bodo vinograde in pili njihovo vino; prav tako bodo naredili vrtove in jedli njihov sad.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.
Jaz jih bom zasadil na njihovi deželi in ne bodo več potegnjeni iz svoje dežele, ki sem jim jo dal, « govori Gospod, tvoj Bog.

< Amosi 9 >