< Amosi 9 >
1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
J’ai vu le Seigneur se tenant sur l’autel, disant: Frappez le gond, et que les linteaux soient ébranlés; car l’avarice est dans la tête de tous, et je tuerai le dernier d’entre eux par le glaive; la fuite ne leur sera pas favorable. Ils fuiront, et celui d’entre eux qui aura fui ne sera pas sauvé.
2 Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol )
S’ils descendent jusqu’à l’enfer, ma main les en retirera; et s’ils montent jusqu’au ciel, je les en ferai tomber. (Sheol )
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
Et s’ils se cachent sur le sommet du Carmel, je les y chercherai et les en enlèverai; s’ils se cachent à mes yeux dans les profondeurs de la mer, là je commanderai à un serpent, et il les mordra.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
Et s’ils sont en captivité devant leurs ennemis, là, je commanderai au glaive, et il les tuera; je fixerai mes yeux sur eux pour leur mal et non pour leur bien.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
Et le Seigneur Dieu des armées touche la terre et elle se fondra, et ils seront dans le deuil, tous ceux qui y habitent; et elle montera comme le fleuve tout entière, et s’écoulera comme le fleuve d’Egypte.
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
Celui qui établit dans le ciel son élévation et qui a fondé son faisceau sur la terre; qui appelle les eaux de la mer, et les répand sur la face de la terre; le Seigneur est son nom.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
Est-ce que vous n’êtes pas pour moi comme les fils des Ethiopiens, fils d’Israël, dit le Seigneur? Est-ce que je n’ai pas fait monter Israël de la terre d’Egypte, et les Philistins de la Cappadoce, et les Syriens de Cyrène?
8 “Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
Voici que les yeux du Seigneur sont sur le royaume pécheur, je le détruirai de la face de la terre; cependant, détruisant, je ne détruirai point la maison de Jacob, dit le Seigneur.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
Car voici que moi je commanderai et j’agiterai parmi toutes les nations la maison d’Israël, comme est agité le blé dans le crible, et il ne tombera pas une seule petite pierre sur la terre.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
C’est par le glaive que mourront tous les pécheurs d’entre mon peuple, ceux qui disent: Non, il n’approchera pas, il ne viendra pas sur nous, le mal qu’on nous prédit.
11 “Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
En ce jour-là, je relèverai le tabernacle de David, qui est tombé; et je refermerai les ouvertures de ses murs, et ce qui était écroulé, je le restaurerai, et je le rebâtirai comme dans les jours anciens.
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
Afin qu’ils possèdent les restes de l’Idumée et toutes les nations, parce que mon nom a été invoqué sur eux, dit le Seigneur, qui fera ces choses.
13 “Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
Voici que des jours viennent, dit le Seigneur, et le laboureur succédera immédiatement au moissonneur, et celui qui foule le raisin à celui qui répand la semence; les montagnes distilleront la douceur, et toutes les collines seront cultivées.
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
Et je ramènerai les captifs de mon peuple d’Israël; et ils bâtiront des cités désertes et ils les habiteront; et ils planteront des vignes, et ils en boiront le vin, et ils feront des jardins, et ils en mangeront les fruits.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.
Et je les planterai dans leur propre sol et je ne les arracherai plus de leur terre que je leur ai donnée, dit le Seigneur ton Dieu.