< Amosi 9 >

1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
J'ai vu le Seigneur debout sur l'autel, et Il a dit: Frappe sur le propitiatoire, et le temple sera ébranlé; frappe ensuite sur toutes les têtes. Et ceux qui resteront, Je les ferai périr par le glaive; nul n'échappera par la fuite, nul ne sera sauvé, ni ne trouvera de salut.
2 Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
Dussent-ils se cacher en enfer, Ma main les en arracherait; dussent-ils monter aux cieux, Je les en précipiterais. (Sheol h7585)
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
Dussent-ils s'enfermer dans les grottes du Carmel, je saurai les y trouver et les prendre; dussent-ils, hors de Ma vue, plonger dans les abîmes de la mer, Je donnerais Mes ordres au dragon, et il les suivrait.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
Dussent-ils partir captifs devant leurs ennemis, là Je commanderais au glaive, et il les exterminerait tous. Et J'attacherai sur eux Mes regards pour leur malheur, et non pour leur bien.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
Et le Seigneur Maître, Dieu tout-puissant, touche la terre, et elle est ébranlée; et tous ceux qui l'habitent seront dans la douleur; et la destruction montera comme le fleuve de l'Égypte, et descendra comme lui.
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
C'est Lui qui bâtit des degrés pour monter au ciel, et affermit Sa promesse sur les fondements de la terre; c'est Lui qui appelle les eaux de la mer, et les verse sur la face de la terre; le Seigneur tout-puissant est Son Nom.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
Fils d'Israël, n'êtes-vous point pour Moi comme les fils des Éthiopiens? dit le Seigneur. N'est-ce point Moi qui ai fait venir Israël de l'Égypte, comme les Philistins de la Cappadoce, et les Syriens de la mer?
8 “Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
Voilà que le Seigneur Dieu a les yeux sur le royaume des pécheurs, et je l'effacerai de la terre. Mais Je n'enlèverai pas entièrement la maison de Jacob, dit le Seigneur.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
Car c'est Moi qui commande, et je vannerai, parmi toutes les nations, la maison d'Israël, comme on vanne le blé au van, et pas un débris ne tombera par terre.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
Tous les pécheurs de Mon peuple périront par le glaive, eux qui disent: Le malheur ne nous approchera pas, il ne viendra pas sur nous.
11 “Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
Et ce jour-là Je relèverai le tabernacle de David, qui était tombé; J'en réparerai les brèches, J'en réédifierai les ruines, et Je le restaurerai comme il était dans les anciens jours,
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
afin que le reste des hommes et tous les gentils, par qui Mon Nom a été invoqué, Me cherchent, dit le Seigneur, qui fera toutes ces choses.
13 “Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
Voilà que les jours arrivent, dit le Seigneur, où la moisson atteindra la vendange, et où la grappe noircira pendant les semailles. Et les montagnes ruisselleront de douceur, et toutes les collines seront plantées.
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
Et Je ramènerai Mon peuple Israël de la captivité, et ils réédifieront les villes détruites, et ils les habiteront; ils planteront des vignes, et ils en boiront le vin; ils cultiveront des jardins, et ils en mangeront les fruits.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.
Et Je les rétablirai dans leur héritage, et ils ne seront plus arrachés de la terre que Je leur ai donnée, dit le Seigneur Dieu tout-puissant.

< Amosi 9 >