< Amosi 9 >

1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
Je vis le Seigneur debout près de l'autel, et il dit: " Frappe le chapiteau, et que les seuils soient ébranlés, et brise-les sur leurs têtes à tous! Et ce qui restera, je l'égorgerai par l'épée; pas un ne se sauvera, pas un n'échappera.
2 Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
S'ils pénètrent jusqu'au schéol, ma main les en retirera; s'ils montent aux cieux, je les en ferai descendre. (Sheol h7585)
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
S'ils se cachent au sommet du Carmel, je les y chercherai et les prendrai; et s'ils se dérobent à mes yeux au fond de la mer, là je commanderai au serpent de les mordre.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
Et s'ils s'en vont en captivité devant leurs ennemis, là je commanderai à l'épée de les égorger. Et je fixerai mon œil sur eux, pour le malheur et non pour le bien. "
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
Le Seigneur Yahweh des armées, touche la terre et elle se fond, et tous ses habitants sont en deuil; elle monte tout entière comme le Nil, et s'affaisse comme le fleuve d'Egypte.
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
Il construit ses degrés dans le ciel, et fonde sa voûte sur la terre; il appelle les eaux de la mer, et il les répand sur la face de la terre: Yahweh est son nom.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
N'êtes-vous pas pour moi comme les fils des Cuschites, enfants d'Israël, — oracle de Yahweh? N'ai-je pas fait monter Israël du pays d'Egypte, et les Philistins de Caphtor, et les Syriens de Qir?
8 “Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
Voici que les yeux du Seigneur Yahweh sont fixés sur le royaume pécheur, et je le détruirai de dessus la face de la terre; toutefois je ne détruirai pas entièrement la maison de Jacob, — oracle de Yahweh.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
Car voici que je vais donner des ordres, et je secouerai la maison d'Israël parmi toutes les nations, comme on secoue le blé avec le crible, et le bon grain ne tombera pas à terre.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
Tous les pécheurs de mon peuple périront par l'épée, eux qui disent: " Le malheur ne s'approchera pas de nous, le malheur ne nous atteindra pas. "
11 “Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
En ce jour-là, je relèverai la hutte de David qui est tombée; je réparerai ses brèches, je relèverai ses ruines, et je la rebâtirai telle qu'aux jours d'autrefois,
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
afin qu'ils possèdent le reste d'Edom, et toutes les nations sur lesquelles mon nom a été invoqué, — oracle de Yahweh, qui fait ces choses.
13 “Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
Voici que des jours viennent, — oracle de Yahweh, et le laboureur joindra le moissonneur, et celui qui foule les grappes joindra celui qui répand la semence; les montagnes dégoutteront de vin nouveau, et toutes les collines ruisselleront.
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
Je ramènerai les captifs de mon peuple d'Israël; ils bâtiront les villes dévastées et les habiteront, ils planteront les vignes et en boiront le vin, ils feront des jardins et en mangeront les fruits.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.
Et je les planterai sur leur sol, et ils ne seront plus jamais arrachés de leur terre, que je leur ai donnée, dit Yahweh, ton Dieu.

< Amosi 9 >